MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Thursday, August 16, 2012

MAREKANI YAENDELEZA MAUAJI SOMALIA

MOGADISHU
Ndege za kigaidi zisizo na rubani za Marekani zimeendelea kufanya mauaji ya watu katika nchi ya Waislamu ya Somalia iliyopo Afrika.
Watu wasiopungua saba wameauwa na wengine kumi na saba wamejeruhiwa katika mashambulizi ya jana Jumatano yaliyofanywa na ndege hizo kwenye mji wa JOWHAR nje kidogo ya mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
Hadi sasa hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusu hasara nyingine zilizosababishwa na mashambulizi hayo ya kinyama.
Mbali na nchini Somalia, Marekani imekuwa ikitumia ndege zisizotumia rubani kufanya mashambulizi ya kigaidi katika nchi za Afghanistan, Pakistan, Yemen na imewahi kutumia pia ndege hizo nchini Libya.
Marekani inadai kuwa inashambulia wanamgambo wa AL-QAEDA na AS-SHABBAB, lakini wananchi wa kawaida ndio wahanga wakuu wa mashambulizi ya ndege hizo za kigaidi.

No comments:

Post a Comment