MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Sunday, August 19, 2012

SWALA YA IDD KITAIFA RUVUMA




Muft wa Tanzania Issa bin Shaaban Simba akiwa katika pozi mbalimbali aliokuwa akihudhuria swala ya IDD iliyoswaliwa kitaifa Mkoani Ruvuma.

SWALA YA IDD MASJID BAKWATA MAKAO MAKUU




Rais Jakaya Kikwete akiwa katika pozi mbalimbali alipokwenda kuswali swala ya Idd katika viwanja vya Bakwata Makao Makuu jijini Dar es Salaam.

SWALA YA IDD MNAZI MMOJA DAR ES SALAAM





Makamu wa Rais Dk Moh'd Gharib Bilal na Mzee Ali Hassan Mwinyi wakiwa katika pozi mbalimbali wakati na baada ya kuswali Idd katika Viwanja vya Mnazi Mmmoja jijini Dar es Salaam.

Friday, August 17, 2012

BREWERIES YAFUTARISHA: NI UPI UHALALI WA FUTARI HIYO, NINI HUKUMU YA MUISLAM ALIYEKUBALI KUFUTARISHWA NA KAMPUNI YA POMBE?




Baadhi ya waislaam na wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (Breweries) wakiwa katika pozi mbalimba waliposhiriki futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo jana.

Thursday, August 16, 2012

MAREKANI YAENDELEZA MAUAJI SOMALIA

MOGADISHU
Ndege za kigaidi zisizo na rubani za Marekani zimeendelea kufanya mauaji ya watu katika nchi ya Waislamu ya Somalia iliyopo Afrika.
Watu wasiopungua saba wameauwa na wengine kumi na saba wamejeruhiwa katika mashambulizi ya jana Jumatano yaliyofanywa na ndege hizo kwenye mji wa JOWHAR nje kidogo ya mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu.
Hadi sasa hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusu hasara nyingine zilizosababishwa na mashambulizi hayo ya kinyama.
Mbali na nchini Somalia, Marekani imekuwa ikitumia ndege zisizotumia rubani kufanya mashambulizi ya kigaidi katika nchi za Afghanistan, Pakistan, Yemen na imewahi kutumia pia ndege hizo nchini Libya.
Marekani inadai kuwa inashambulia wanamgambo wa AL-QAEDA na AS-SHABBAB, lakini wananchi wa kawaida ndio wahanga wakuu wa mashambulizi ya ndege hizo za kigaidi.

MAELFU WAKIMBIA MAKAZI YAO

KINSHASA
MAPIGANO ya miezi mitano sasa kati ya waasi wa kundi la M23 na Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya KONGO yamewalazimisha zaidi ya watu nusu milioni kukimbia makazi yao huko mashariki mwa nchi hiyo.
Ripoti zinasema kuwa raia wengi wa maeneo ya Kivu Kaskazini yenye utajiri mkubwa wa madini wamelazimika kukimbia makazi yao baada ya kujikuta katikati ya machafuko na mapigano ya kundi la M23 na Jeshi la serikali ya Kinshasa.
Maafa hayo yanaendelea kuwapata raia wa kawaida wa KONGO licha ya kuwepo maelfu ya askari wa Umoja wa Mataifa waliopelekwa nchini humo kwa ajili ya kulinda amani.
Mamia ya wakimbizi hao wa KONGO wamevuka mpaka na kuingia nchi jirani za RWANDA, BURUNDI na UGANDA huku Serikali ya KONGO ikitoa shutuma kali kwa nchi ya RWANDA na UGANDA kwa kuwaunga mkono waasi wa kundi la M23.
Waasi wa M23 walijitenga na jeshi la serikali ya Kinshasa wakidai kuwa serikali haijatekeleza vipengele vya makubaliano ya amani yaliyotiwa saini MACHI 23, 2009.

HRW YAINGILIA KATI WAISLAAM KUKAMATWA ETHIPEA

ADDISABABA
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeitaka serikali ya Ethiopia kuwaachia huru viongozi 17 wa Kiislamu waliokamatwa katika maandamano ya amani yaliyofanyika nchini humo.
Taarifa iliyotolewa na hilo la Kutetea Haki za Binadamu imesema serikali ya Ethiopia inapaswa kuwaachia huru viongozi hao 17 wa Kiislamu waliotiwa nguvuni wakati askari wa usalama wa Ethiopea walipowakandamiza kinyama wapinzani Waislamu mjini Addis Ababa.
Watu hao walitiwa nguvuni katika maandamano makubwa ya amani yaliyofanywa na Waislamu mwezi jana kupinga uingiliaji usio wa kisheria wa serikali katika masuala ya Waislamu.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesisitiza kuwa mahabusu hao wanakabiliana na hali mbaya na wanashikiliwa bila ya kujulishwa makosa yao au kuwa na wakili.
Waislamu wanaunda zaidi ya asilimia 30 ya jamii ya watu milioni 83 ya Ethiopia.