MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Thursday, May 21, 2009

Shura ya Maimamu yamwaga misaada kwa waathirika wa mabomu Mbagala


Salim Said
SHURA ya Maimamu, walisimamia na kugawa msaada wa tani moja ya maharage, tani mbili na nusu za Sembe, nguo, chumvi na sabuni vyote vikiwa na thamani ya sh4.2 milioni kwa waathirika.

Ugawaji wa msaada huo kwa watu zaidi ya 500 bila ya kujali tofauti za kiimani, ulifanyika chini usimamizi wa Amiri wa Shura hiyo,Sheikh Mussa Kundecha katika viwanja vya Msikiti wa Taq-wa ulioathirika na milipuko ya mabomu hayo.

Akizunguza muda mfupi kabla ya kuanza kugawa msaada huo, Katibu wa Shura hiyo Sheikh Ponda Issa Ponda alisema, wameamuwa kugawa msaada huo kutokana na malalamiko yanayotolewa na walengwa kwamba haiwafikii.

Shehena ya samaki haramu yawa zigo kwa serikali

Salim Said

SERIKALI imekiri kulemewa na shehena ya tani zaidi ya 290 za samaki zilizokamatwa kwenye meli ya MV Tawariq 1 iliyokuwa ikifanya uvuvi haramu kwenye pwani ya Tanzania.

Imedaiwa kuwa samaki hao wanahifadhiwa kwa gharama ya Dola 80 za Marekani kwa tani moja kila siku na kampuni Bahari Foods Limited ya Dar es Salaam kuanzia Machi 8 mwaka huu.

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, John Magufuli alisema juzi Dar es Salaam kuwa, gharama hizo ni mzigo kwa serikali ambayo hadi sasa haijui hatima yake.

“Ni kweli serikali inaendelea kuumia,” alisema Magufuli bila kutaja kiwango cha gharama inayolipia shehena hiyo lakini akibainisha kuwa suala hilo lipo chini ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

“Serikali inaheshimu mahakama na wala haiwezi kuingilia kazi yake, kwa hiyo mahakama ndio itakayoamua hatma ya samaki hao,” alisema Magufuli

Alieleza kushangazwa kwake na jinsi kesi hiyo inavyocheleweshwa akitolea mfano wa mahakama katika nchi zingine za Afrika ikiwamo Namibia ambako alisema kuwa hukumu za kesi za aina hiyo hazichukui siku tano