MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Monday, June 29, 2009

Makamu mwenyekiti ZEC ajiuzulu

Salim Said
MAKAMU Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Omar Othman Makungu amejiuzulu wadhifa wake katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC).

Jaji Makungu alikuwa Kamishna wa ZEC tangu Januari mwaka 2008 baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo na Rais Amani Abeid Karume.

Taarifa ambazo Mwananchi na kuthibitishwa na mwenyewe Jaji Makungu zinasema, amechukua uamuzi huo akihofia kuzidiwa na kazi katika uchaguzi mkuu wa 2010 kwa kuhudumu katika tume mbili tofauti.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutoka visiwani Zanzibar jana, Jaji Makungu alithibitisha kujiuzulu kwake wadhifa huo hivi karibuni kwa kuhofiwa kuzidiwa na kazi katika kipindi uchaguzi.

“Ni kweli nimejiuzulu,” alithibitisha na kuongeza kuwa:

“Nimejiuzulu kwa sababu tunaelekea katika uchaguzi mkuu kwa hivyo sitaweza kutumika kwenye tume ya taifa ya uchaguzi na tume ya uchaguzi ya Zanzibar kwa wakati mmoja.”

Alisema, kwa vile anafanya kazi katika tume zote mbili za uchaguzi anaweza kuzidiwa na majukumu na hivyo ni bora tu kubakia katika upande mmoja wa NEC.

Januari mwaka 2008 Rais wa Zanzibar Amani Abeidi Karume alimchagua Jaji Makungu kuwa miongoni mwa makamishna wa ZEC baada ya kuunda upya tume ya uchaguzi ya Zanzibar.

Rais Karume alimtangaza Khatib Mwinyichande kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo pamoja na makamishna sita, wakiwemo wawili kutoka chama cha Wananchi (CUF).

Makamishna walioteuliwa kuhudumia ZEC kwa miaka mitano ni aliyekuwa Meneja Mkuu wa Shirika la Biashara Zanzibar (ZSTC), Abdulrahman Rashid na aliyewahi kuwa Waziri wa Afya na Utibabu Zanzibar, Said Bakar Jecha.

Wengine ni Mwanabaraka Maalim Ahmed, Jaji wa Mahakama Kuu na Makamu Mwenyekiti NEC Omar Othman Makungu.

Wajumbe walioteuliwa kutoka CUF, ni wakili maarufu wa Zanzibar, Nassor Khamis na Ayoub Bakar Hamad aliyekuwa Katibu wa Uchaguzi wa CUF.

Sunday, June 28, 2009

MSIBBBAAAA KWA WASOMI NCHIN

HABARI VIPANDE VIPANDE!!!!!
Kwa mujibu wa habari tulizozipata muda si mrefu kutoka visiwani Zanzibar zinasema kuwa mhadhiri wa masuala ya Development Studies katika chuo kikuu cha Dar es Salaam na Mwanasheria wa kujitegemea Profesa Haroub Othman amefariki usiku wa kuamkia leo visiwani Zanzibar.

Tutawaletea habari zaidi kuhusu msiba huo ikiwa ni pamoja shughuli na maandalizi ya mazishi

Thursday, June 25, 2009

Kampeni uchaguzi Bakwata zapamba moto

Salim Said
KAMPENI za uchaguzi wa Baraza Kuu la Waislaam Tanzania (Bakwata) katika ngazi ya Wilaya zinaendelea, huku ishara za kutokea kwa vurugu za hapa na pale zikianza kuonekana mapema.


Baadhi ya wagombea wamewashutumu wengine kuwa, wanatoa vitisho kwa lengo la kudhoofisha nguvu zao katika kampeni hizo ambazo zinatarajiwa kuishia mwishoni mwa mwezi huu.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, mgombea mwenyekiti wa Bakwata Wilaya ya Temeke sheikh Ali Mtulya alidai, amekuwa akitumiwa ujumbe wa vitisho kupitia simu yake ya mkononi mara kwa mara.

Alisema, wanaomtumia ujumbe huo hawajui na kila anapojaribu kupiga namba zinazotumiwa kutuma ujumbe huo, huwa hazipatikani.

“Haya hayaashirii mema katika uchaguzi huu, nimekuwa nikitumiwa meseji za vitisho na matusi kupitia simu yangu ya mkononi na kila nikijaribu kupiga simu hizo hazipatikani,” alisema sheikh Mtulya.

Sheikh Mtulya, ambaye anatetea nafasi yake ya Mwenyekiti wa Wilaya hiyo, alimshutumu sheikh Mkuu wa Bakwata Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum kuwa, amekusudia kuandaa watu kwa ajili ya kumng’oa.

Alidai, katika hotuba ya uzinduzi wa msikiti wa Bakwata Wilaya hiyo sheikh Salum alisema kuwa, atahakikisha sheikh Mtulya haingii madarakani.

“Sheikh wa Mkoa katika hotuba yake ya uzinduzi wa msikiti wa Bakwata Wilaya ya Temeke alisema kwamba, atahakikisha mimi sirudi madarakani na ataandaa watu wake kuhakikisha anatimiza azma hiyo,” alisema Sheikh Mtulya na kuongeza:

“Yeye kama sheikh wa mkoa alitakiwa kutoa hotuba nzuri ya kuhamasisha amani na utulivu katika uchaguzi wetu, badala ya kuharibu. Eti kwa sababu mimi sikumpigia kura alipogombea usheikh wa mkoa na ni kweli sikumpigia.”

Alisema, kutoka na kauli hiyo wanaandaa tamko la kulaani kauli ya sheikh Salum na baadaye wataliwasilisha Bakwata Makao Makuu.

Kwa upande wake sheikh Salum ambaye ni sheikh wa mkoa wa Dar es Salam alikiri kusema maneno hayo, lakini alidai kuwa alizungumza maneno hayo kwa utani tu na wala hayakuwa na ukweli wowote.

“Mimi yule ni shemegi yangu ametuolea, kwa hiyo mimi nilisema kama kumtania tu, kwa sababu mtu akitaka kufanya ubaya kwa mwengine hasemi bali hufanya kimya kimya,” alisema Sheikh Salum.

Alisema, kama wao wameyachukulia kweli ni upuuzi, kwa kuwa kama anataka kumfanyia ubaya hana haja ya kuandaa vijana bali angesubiri majina ya wagombea yatakapofikishwa ofisini kwake na kuliondoa jina lake.

“Lakini mimi sina ubaya na mtu yoyote, wote nimewasamehe,” alisema sheikh Salum.

Alisema, kama kuna watu wamejitokeza kupambana na sheikh Mtulya kwa kuchukua fomu wanatumia haki yao ya kidemokrasia na hawakuandaliwa na yeye.

“Kama kuna vijana wamechukua fomu, wanatumia demokrasia yao, lakini sijawandaa mimi. Na kama wanaandika tamko la kulaani ili waliwasilishe Bakwata makao makuu ni upuuzi tu,” alibeza sheikh Salum.

Kwa upande wake Afisa Habari wa Bakwata ustadh Issa Mkalinga, alithibitisha kupata malalamiko hayo kutoka kwa Sheikh Mtulia na kwamba uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Juni 28 kwenye shule ya Sekondari ya Thaqafa Tandika jijini hapa.

Alisema, tayari wamemaliza chaguzi katika ngazi ya Msikiti na Kata kwa kiwango kikubwa nchini na kwamba sasa wanaingia katika ngazi ya Wilaya halafu Mkoa na kumalizia na Taifa.

Chadema kumpokea Lwakatare Bukoba Mjini leo

Salim Said
ALIYEKUWA Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Tanzania Bara Wilfred Lwakatare, ametangaza rasmi kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na leo anatarajiwa kupokelewa rasmi na wanachama wa chama hicho mjini Bukoba.


Baada ya kupokelewa leo, kesho Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe atampa kadi chama hicho katika hafla maalumu, itakayofanyika katika Jimbo la Biharamulo Magharibi, kabla ya kuanza kupanda majukwani kumnadi mgombea wa chama hicho katika kinyang'anyiro cha ubunge.

Lwakatare ambaye alishika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Bara kwa zaidi ya miaka 10, alitangaza hayo jana baada ya kupata ushauri kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki zake.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu akiwa wilayani Bukoba, Lwakatare alisema:“Mimi ni Chadema kuanzia jana (juzi) saa 1:30 usiku, nyinyi mko nyuma sana kwa sababu taarifa hizi zimefika Ujerumani nyinyi Dar es Salam hamjapata!”

Lwakatare alitangaza kujiondoa CUF kupitia mahojiano yake ya moja kwa moja na Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani juzi saa 1:30 usiku.

Alisema uamuzi huo aliuchukua baada ya kufanya kikao na familia yake, mzazi wake na wanachama wake 284, na kuwaeleza mkasa uliomfika, wanachama 282 walimwambia aende Chadema na kwamba wanachama wawili tu walimtaka aende Chama cha Mapinduzi (CCM).

“Mzazi wangu ameniambia niende Chadema, familia pia imeniambia hivyo hivyo wanachama 282 katika kikao waliniambia ‘nenda chadema’ isipokuwa wawili walioniambia ‘nenda CCM’ kwa hiyo wengi wameshinda,” alisema Lwakatare.


Pamoja na uamuzi huo, Lwakatare aliwataka viongozi wa CUF kujifunza kwa kupitia vitabu yake kuanzia namba moja hadi tatu ambavyo amewatumia ili kurekebisha chama chao kwa kuwa si chama chake.

Alisema bado anaamini kuwa ukombozi wa Watanzania ni vyama vyote kuungana ili kujenga nguvu moja ya mapambano na CCM, na kwamba bila hivyo CCM itaendelea kutawala nchini.

“Licha ya kujiunga na Chadema niko tayari kushirikiana na CUF kwa lengo la kuunganisha nguvu ya upinzani kuing’oa CCM,” alisisitiza Lwakatare.

Naye Mwenyekiti wa CUF taifa Profesa Ibrahim Lipumba alisema amepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa kwa kuwa Lwakatare alikuwa mjumbe katika Baraza Kuu la Uongozi la chama na mjumbe wa mkutano mkuu wa Taifa.

“Tunasikitika sana kwa sababu alikuwa kiongozi wetu na tulikuwa naye muda mrefu. Tulifanya mabadiliko ili kumpa muda wa kuimarisha chama lakini ameamua kufanya uamuzi huo, tunasikitika sana.

“Licha ya jitihada zangu za kuzungumza naye sana na kumsihi ameamua hivyo, mimi nilidhani tumeshaelewana na kuyamaliza kumbe ilikuwa bado. Lakini kukosa unaibu si sababu ya kuhama chama,” alisema Profesa Lipumba.

Lwakatare aliwahi kuwa mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini na Mwenyekiti wa Kambi ya upinzani Bungeni kupitia tiketi ya CUF na hatimaye sasa ameamu kujiunga na Chadema baada ya kuangushwa Machi mwaka huu katika nafasi yake ya unaibu Katibu Mkuu.

Wakati huohuo, aliyekuwa naibu katika mkuu wa chama cha wananchi CUF Alfred Rwakatare kesho anatarajia kujiunga rasmi na chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema na kukabidhiwa kadi ya uanachama na mwenyekiti wa taifa wa chama hicho Freeman Mbowe.

Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi wa oparesheni na uchaguzi wa Chadema John Mrema alisema kuwa Rwakatare ataingia rasmi Chadema ijumaa na kukabidhi kadi ya uanachama katika mkutano wa hadhara utakaofanyika katika uwanjwa wa Uhuru mjini Bukoba.

Mrema alisema mara baada ya Kukabidhiwa kadi hiyo na kuwa mwanachama rasmi Rwakatare atawasili jumamosi Biharaulo magharibi kwa ajili kusaidia kampeni za kumnadi mgombea wa chadema Dk. Grevas Mbassa pamoja na viopngozi wengine wa Chadema.

Aliwataja viongozi hao kuwa ni pamoja na Dk. slaa, Philimoni Ndesambulo pamoja na Zitto Kabwe ambao baada ya zoezi hilo nao pia wataingia Biharamulo kwa ajili ya kusaidia kampeni za chama chao.

Wednesday, June 24, 2009

Profesa Lipumba aiponda bajeti ya 2009/10




Salim Said
JUNI 18 mwaka huu Watanzania wameshuhudia wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakiipitisha kwa kishindo bajeti ya serikali ya Sh9.5 trilioni kwa mwaka 2009/10, baada ya wabunge 221 wa chama hicho kuipigia kura za ndio.

Katika kazi ya kupitisha bajeti hiyo, jumla ya wabunge 33 wa kambi ya upinzani kati ya wabunge wote 318 wa bunge la Tanzania, waliipinga bila ya mafanikio kwa kupiga kura za sio, kutokana na idadi yao kuzidiwa na wale wa CCM waliopiga kura za ndio.

Bajeti hiyo ambayo awali ilipata upinzania mkubwa kwa wabunge wa CCM kabla ya kufika bungeni, lakini kilichotokea ni kwa ujasiri wa wabunge hao haukuthubutu kujitokeza bungeni jambo ambalo baadhi ya wachambuzi wamesema ni unafiki.

Wadau mbalimbali wa masuala ya kiuchumi nchini waliipokea kwa mitazamo tofauti bajeti hiyo na kutoa maoni yao wakiamini kuwa serikali huenda ikayatumia katika kuirekebisha bajeti hiyo.
Mchambuzi nguli, wa masuala ya kiuchumi nchini Profesa Ibrahim Lipumba anaiponda bajeti hiyo kwa madai kuwa, ni tegemezi na haiwezi kumfikisha popote mtanzania wa kawaida.

Anasema, bajeti hiyo haikuzingatia misingi muhimu ya bajeti na hivyo haiwezi kuitwa bajeti bora na iliyokamilika.

Anasema bajeti hiyo, ina upungufu mwingi na haiwezi kabisa kupambana na matatizo ya umasikini yanayomkabili Mtanzania wa kawaida, kwa sababu haikuzingatia misingi muhimu ya bajeti.

“Bajeti hii bado ni tegemezi iliyojaa kasoro na wala hawiezi kumfikisha popote mtanzania wa kawaida katika kumuondeshea matatizo ya umasikini wa kipato,” anasema Profesa Lipumba.

Profesa Lipumba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anasema, bajeti iliyokamilika inapaswa kujumuisha mapato yote na matumizi ya serikali bila ya kujali taratibu maalum za kuendesha baadhi ya miradi au programu.

“Kwa ujumla mapato na matmizi yote lazima yapangwe na kuainishwa katika bajeti bila ya kujali chanzo cha mapato, hii itabainisha iwapo kuna uhusiano wa karibu kati ya mapato na wanaonufaika na matumizi ya mapato hayo, kwa sababu hoja ya mapato husika kulipia matumizi ya huduma inakubalika,” anasema Profesa Lipumba.

Anasema, utayarishaji wa bajeti lazima uzingatie malengo ya uchumi mpana, ukuaji wa pato la taifa, mfumko wa bei, akiba ya fedha za kigeni na thamani ya sarafu ya nchi husika.

“Bajeti bora lazima matumizi yake yagawiwe kulingana na malengo ya sera ya maendeleo ya taifa kwa sababu jambo linaloathiri sera, utayarishaji na utekelezaji wa bajeti ni uanzishwaji wa sera na utamkaji wa ahadi zisizoendana na vipaumbele vilivyotumika kuandaa bajeti,” anasema Profesa Lipumba.

Anafafanua kwamba, pia bajeti lazima ilenge kujenga mazingira mazuri ya utekelezaji mzuri wa bajeti ya serikali.

Anasema, kwa kuwa bajeti ni kioo cha sera za serikali, ni lazima iwe na uhusiano wa karibu na sera hizo ili kuratibu vizuri uanzishwaji wa sera na kushirikisha umma katika utungaji wake.

Anasema, bajeti lazima iweze kupitia na kutathmini mafanikio na mapungufu ya sera za maendeleo ya taifa na kuchambua kwa kina mahitaji ya fedha na rasilimali nyingine za taifa, ili kuhakikisha bajeti inashika hatamu katika mapato na matumizi ya serikali.

“Maandalizi ya bajeti lazima yazingatie hali halisi ya uchumi ili kuweza kukadiria kwa usahihi mapato na kuyatambua matumizi yake yote ya lazima,” anafafanua Profesa Lipumba.

Anasema, bajeti ya mwaka huu ni ya kisanii kwa sababu haikuzingatia sera za maendeleo ya taifa ikiwamo ya Mkakati wa Kukuza na Kupunguza Umasikini (Mkukuta), Dira ya Maendeleo ya 2025, Ilani ya CCM na Mpango Maalum wa Kurahisisha Maendeleo (Tiger Plan 2020).

Anasema, mpango wa kunusuru uchumi wa nchi umetengewa sh1.7 trilioni na rais Jakaya Kikwete, ambaye amesema fedha hizo zimeingizwa katika bajeti ya serikali, lakini bajeti haijaainisha waziwazi mpango huo na matumizi ya fedha hizo.

Anailaumu serikali, kwa kukusudia kukopa kiasi hicho cha sh1.7 trilioni kwa riba kubwa ili kukopesha kwa wafanyabiashara kwa riba ndogo.

“Hivi wewe unakopa fedha kwa riba ya asilimia 11 au zaidi, halafu unamkopesha mfanyabiashara kwa riba ya asilimia 2, hizo ni akili kweli? Tutasema wewe uko makini kweli au una lengo zuri kwa wananchi wako,” anahoji profesa Lipumba.

Anasema, kwa mujibu wa utafiti wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) umebaini kuwa mabenki ya kigeni yaliyopo nchini yanakula njama ya kuhakikisha kuwa yanapata faida kubwa na kwa haraka ili kununua amana za serikali.

“Benki Kuu ya Tanzania (BoT) haina mamlaka ya kupanga riba kwa wateja wa benki za biashara. Tusipokuwa makini mikopo ya serikali itawanufaisha wenye mabenki na kuwadidimiza wafanyabiashara wetu wadogo na wa kati,” anatoa angalizo.

Anasema, benki zinawalipa riba ndogo wanaoweka akiba zao kwa wastani wa asilimia 2.7 wakati yanatoa mikopo kwa riba ya wastani wa asilimia 16.1 huku kukikosekana benki inayofanya jitihada za kutosha kutoa motisha na kukusanya akiba za watanzania.

“Serikali imeweka mikakati na mfumo gani wa kiutawala ili kuhakikisha Benki ya Rasilimali (TIB) haitoi mikopo kisiasa na fedha za walipa kodi zilizoweka kama mitaji katika benki hiyo hazipotei,” anahoji Profesa Lipumba.

Anasema, ili kunusuru hilo, utawala wa benki hiyo unahitaji kuimarishwa, kwa kuteua watendaji makini na Bodi ya Wakurugenzi iteuliwe bila ya kujali hisia za kichama ili iwe na mamlaka ya kusimamia watendaji wake na kutotoa mikopo kisiasa na kifisadi.

Profesa Lipumba anasema, kaulimbiu ya ‘Kilimo Kwanza’ ni msemo wa kisiasa na kwamba imepita mingi lakini katika utendaji hakuna mabadiliko kwa kuwa mgao wa fedha katika sekta hiyo hauna tofauti na ule wa mwaka jana katika bajeti.

“Bajeti ya mwaka jana ilitenga sh513 bilioni sawa na asilimia 7.1 na hii ya mwaka huu imetenga sh666 bilioni sawa na asilimia 7.0 ya bajeti yote. Je tofauti iko wapi, ni usanii tu wa kisiasa katika utendaji,” anasema Profesa Lipumba.

“Mara Kilimo Kwanza, Kilimo ni Uti wa Mgongo, Siasa ni Kilimo, Utu ni Kilimo yote ni misamiati tu ya kuwababaisha watanzania.”

Anasema, ili kuhakikisha umasikini unapungua vijijini kilimo kinapaswa kukuwa kwa wastani wa asilimia 6 hadi 8, kwa mwaka katika kipindi cha mpito kwani wakulima wadogo ndiyo tegemeo la kilimo cha Tanzania, lakini hawajasaidiwa vya kutosha kuboresha kilimo chao.

Anaitaka serikali kufuta misamaha ya kodi kwa viongozi wa juu wa serikali na wabunge na kuhakikisha kuwa wanalipa kodi ili kuondoa matabaka kati yao na wanaowaongoza.

“Mapato mingi ya serikali yanapotea kupitia misamaha holela ya kodi. Viongozi wana misamaha mingi ya kodi ikiwa ni pamoja nay a kuingiza vitu vyao binafsi nchini,” anasema Profesa Lipumba.

Kwa upande wake Msomi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Dk. Benson Bana anatofautiana na Profesa Lipumba kuhusu bajeti hiyo akisema kwamba, ni nzuri na imezingatia vipaumbele muhimu kwa maisha ya Mtanzania.

“Profesa Lipumba, ni mchumi nguli, tunamuamini na tunamuheshimu kweli, lakini profesa huyu ni mwanasiasa, hivyo nilitegemea ataipinga, na kama angeipongeza au kuikubali ningemshangaa sana, hasa ukizingatia nafasi yake,” anasema Dk. Bana.

Anasema, “Namuheshimu sana lakini naweza kumkosoa Profesa kwa hili, bajeti yetu imezingatia sana misingi ya bajeti ina uhusiano na sera zote za maendeleo ya taifa na imeainisha mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa bajeti, kwa sababu hata mimi nimechambua.”

Anasema bajeti kwa kawaida inatenga fungu maalum kwa ajili ya vipaumbele vyake kwa kuzingatia umuhimu, mahitaji na uwezo wa mapato ya taifa na sio kupanga bajeti kubwa hadi kuvuka kiwango cha mapato yako, itakuwa haitekelezeki.

Lakini Dk Bana anasema, bajeti hiyo imeandaliwa na wataalamu wa fedha na uchumi nchini ambao ni wanafunzi wa Profesa Lipumba.

CUF yaanza kuweweseka kwa Lwakatare

Salim Said
SIKU chache baada ya Willfred Lwakatare kuvua nyadhifa zake zote na kurudi jimboni kwake, CUF imeanza kudhibiti nyendo zake baada ya kumzuia kufanya mikutano ya hadhara.


Mkurugenzi wa habari na uenezi wa CUF, Ashura Mustafa aliiambia Mwananchi jana kuwa chama hicho kimesambaza barua katika wilaya na matawi yake yote nchini kuwaagiza watendaji wake wamdhibiti Lwakatare ili asifanye mikutano kwa mgongo wa chama.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Lwakatare, ambaye amekuwa akiripotiwa kuhutubia mikutano ya hadhara akiuliza watu ahamie chama gani, haruhusiwi kufanya mkutano wowote isipokuwa kwa idhini ya makao makuu.

Nafasi ya Lwakatare, ambaye aliondolewa katika kutetea nafasi yake ya naibu katibu mkuu baada ya kuuishikilia kwa karibu miaka 10, ilichukuliwa na Joram Bashange. Kwa upande wa Zanzibar, nafasi hiyo inashikiliwa na Juma Duni Haji.

Kitendo hicho kilimfanya aandike barua ya kujivua nyadhifa zote kwenye chama hicho na kubaki na mwanachama wa kawaida.

Jana Ashura aliliambia gazeti hili kuwa pamoja na chama kusambaza barua hizo za kumzuia Lwakatare kufanya mikutano, pia kinakusudia kutoa tamko zito dhidi ya mbunge huyo wa zamani wa Bukoba Mjini.

Alisema anachofanya Lwakatare si kuimarisha chama kama alivyodai kwenye barua yake kwa mwenyekiti alipotaka kujiuluzu bali kukivuruga katika kipindi hiki cha kukaribia chaguzi za kitaifa.

“Ni kweli tumewaandikia wenyeviti wa chama katika kata na wilaya zote Tanzania Bara na hasa Kanda ya Ziwa kuwataka kuwataka wamzuie Lwakatare kufanya mikutano ya kukivuruga chama kwa kuwalisha sumu wa wananchi akitumia jina la CUF,” alisema Mustafa.

“Tumewaagiza kama atataka kufanya mkutano wowote kwa jina la CUF asiruhusiwe, badala yake waripoti makao makuu, halafu tutaangalia lengo la mkutano huo. Tukijiridhika tunaweza kuruhusu lakini bila hivyo asifanye.”

Alisema Lwakatare sasa hana mamlaka kikatiba kufanya mkutano wowote kwa jina la CUF kwa sababu si kiongozi tena wa chama bali mwanachama wa kawaida.

“Kwa vile ameamua kujivua nyadhifa zake zote ndani ya chama na chama kimeridhia, hana tena mamlaka ya kuitisha mikutano ya wanachama; uwe wa hadhara au wa ndani,” alisema Mustafa.

Mwishoni mwa wiki iliyopita mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alimsihi Lwakatare kutoharibu chama baada ya kujiengua katika nyadhifa zake.

Habari za ndani zinasema kuwa tayari viongozi wakuu wa chama hicho- Prof Lipumba, katibu mkuu Seif Sharif Hamad na makamu mwenyekiti Machano Khamis- wamekutana kujadili namna ya kukihami chama na kile kilichoelezwa kuwa mkakati wa Lwakatare kutaka kukichafua.

Inadaiwa kuwa katika kikao hicho, Machano, ambaye alifanya ziara fupi Kanda ya Ziwa baada ya Lwakatare kujiuzulu, alieleza mambo aliyoyaona wilayani Bukoba kuhusu maendeleo ya chama chao.

Akizungumzia uamuzi huo wa CYF, Lwakatare aliiambia Mwananchi kuwa hana taarifa ya agizo hilo kwa kuwa anaamini halijafika wilayani kwake Bukoba mjini.

“Huku hili agizo au barua halijafika na ikifika tutaijadili kuona kitu gani cha kufanya kuweza kufanya kazi yangu ya kuimarisha chama,” alisema Lwakatare jana.

“Mimi bado ni mwanachama wa CUF na nilisema kwamba uamuzi wa kujiunga na chama chochote upo mikononi mwa familia yangu, wananchi na viongozi wangu wa CUF,” alisema Lwakatare alipozungumza kwa njia ya simu akiwa Bukoba.

'Kutogusa Meremeta ni kukiuka utawala bora'

Salim Said
UAMUZI wa Serikali kuzuia kujadiliwa kwa kampuni ya Meremeta Gold Mine umeelezwa kuwa ni ukiukwaji wa misingi ya utawala bora, wanaharakati na wanasiasa wameeleza.


Kwa mara nyingine, serikali juzi ililieleza Bunge kuwa masuala yanayohusu kampuni ya Meremeta hayawezi kujadiliwa kwenye chombo hicho cha wawakilishi wa wananchi kwa kuwa yanahusu usalama wa nchi na Jeshi la Wananchi (JWTZ).

Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari alitoa tamko hilo akirejea kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa Bungeni mwaka jana kuwa suala hilo haliwezi kujadiliwa na kuwataka Wabunge waheshimu kauli hiyo ya mtendaji mkuu wa serikali.

Katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, ambaye aliuliza swali la msingi, alipotaka kueleza kuwa anachohoji ni wizi, spika wa Bunge, Samuel Sitta alimkatisha na kumwambia kuwa walishakubaliana katika kikao cha kamati ya maadili ya viongozi kuwa suala la Meremeta lisijadiliwe hadharani kwa sababu za kiusalama.

Jana mratibu wa masuala ya utawala bora wa Mtandao wa Mashirika ya Wanaharakati (FemAct) ambao unaunganisha taasisi 50, Buberwa Kaiza alisema jana kuwa kitendo hicho kinajenga taswira kuwa dola inashabikia ufisadi.


Alisema katika nchi yoyote inayofuata misingi ya utawala bora, hakuna jambo linalopaswa kuendeshwa kwa usiri hasa jambo hilo linapohusu wizi wa mali ya umma na kwamba kuzuia Meremeta kujadiliwa hadharani ni kukiuka kanuni hizo.

“Katika utawala bora hakuna siri na matumizi ya fedha za umma yanapaswa kuwekwa hadharani,” alisema Kaiza.

Alisema ni jambo la kushangaza kuona bunge ambalo ni sehemu pekee ya haki ya kuzungumza na kujadili masuala ya maendeleo ya nchi, hasa matumizi ya fedha za umma linazuiwa kujadili kampuni hiyo ya Meremeta kwa kigezo cha ulinzi na usalama wa taifa.

Kaiza, ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa shirika la Fordia, alisema: "Hii ni ishara ya nchi kutekwa na mafisadi kwa sababu serikali imeamua kuwatetea kwa nguvu zote watu wachache ambao wanatuhumiwa kwa matumizi mabaya ya fedha za umma."

Kauli ya Buberwa iliungwa na mkono na katibu mkuu wa chama cha NCCR- Mageuzi, Samwel Ruhuza aliyetaka kampuni hiyo ijadiliwe kwa sababu imetuhumiwa kwa ufisadi ambao hauna uhusiano na usalama wa taifa.

Ruhuza alisema licha ya kuwa suala la Meremeta linahusisha usalama wa taifa, serikali inatakiwa kutambua kuwa kampuni hiyo inahusika na ubadhilifu wa fedha za walipakodi.

“Hivi mfanyakazi wa usalama wa taifa akiiba hataulizwa wala kushtakiwa," alihoji Ruhuza
"Suala la msingi hapa ni ubadhilifu... hayo ya usalama yasijadiliwe, lakini hili la ubadhilifu lazima liongelewe.”


Kwa mujibu wa Ruhuza, inaeleweka kuwa fedha nyingi za walipakodi zilitolewa na kupelekwa Meremeta, hivyo serikali haina sababu za kuzuia suala hilo kujadiliwa hadharani kwa kuwa linawahusu wananchi.

“Mimi sina haki ya kujua kama jirani yangu anamiliki bunduki au la lakini ikitokea mtoto wangu amekutwa ameuawa nje ya nyumba ya jirani yangu, hapo lazima niulize ili nipate ufafanuzi na maelezo sahihi juu ya kifo hicho sasa suala hili ndio mfano halisi wa hii kampuni ya Meremeta.”

Kauli hiyo ya serikali imekuja wakati Bunge likiwa limemuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), kuikagua Meremeta pamoja na Mwananchi, ambayo imeelezwa kuwa iko katika mchakato wa kufilisiwa na kwamba itajadiliwa baada ya kumalizika kwa zoezi hilo.

Inadaiwa kuwa wanahisa wa Meremeta, ambayo ilipewa kiasi cha Sh155 bilioni na Benki Kuu (BoT) katika mazingira yanayoonyesha kuwepo kwa ufisadinatuhumiwa, ni kampuni ya Trienex ya Afrika Kusini ambayo inamiliki asilimia 50 na Hazina (50%).

Wanahisa wengine wa kampuni hiyo inayodaiwa kuwa ilianzishwa jijini London, ni London Law Secretary Services. Ilidaiwa Bungeni kuwa kampuni ya Tangold ndiyo iliyorithi mali za Meremeta baada ya kampuni hiyo kuwa mufilisi.

Sunday, June 21, 2009

Dk. Bana aishauri Serikali


Salim Said
PAMOJA na Serikali kutengua uamuzi wa kufuta misamaha ya kodi kwa Taasisi na Mashirika ya Dini juzi, Msomi na Mchambuzi mashuhuri wa masuala ya kisiasa na uchumi Dk. Benson Bana, ameitaka serikali kuunda Tume Huru ya Wataalam kuchunguza matumizi ya misamaha hiyo kwa miaka mitano iliyopita katika kila dini na dhehebu nchini.


Alisema utitiri wa taasisi hizo unatishia amani ya pato la taifa na kusababisha baadhi yao kuitumia vibaya misamaha hiyo kwa maslahi yao binafsi jambo ambalo linaingizia hasara serikali, ambapo inatumia asilimia 30 ya mapato yake kila mwaka kugharamia misamaha hiyo.

Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalum Ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana alisema, serikali imekuwa laini sana kwa kuwa inatoa misamaha lakini inashindwa kuisimamia.

“Serikali imekuwa laini sana, huwezi kutoa msamaha wa kodi halafu ukaachia huru bila ya kusimamia ni uzembe. Kwa hiyo lazima serikali iunde tume huru ya wataalamu kuchunguza matumizi ya misamaha kwa miaka mitano iliyopita,” alisema Dk Bana na kuongeza:

“Uchunguzi lazima ufanyike kwa dini zote na madhehebu yote na taasisi zitakazogundulika kutumia vibaya misamaha hiyo, hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake. Huwezi kuwa na gari tatu halafu unaingiza tairi 400 kutoka nje ya nchi.”

Dk Bana ambaye pia ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam alifafanua, zamani Tanzania ilikuwa na dini nne tu lakini kwa sasa ina dini zaidi ya 100 na kila siku zinaendelea kuchepua kama uyoga.

“Zamani tulikuwa na dini ya kisslaam, Katoliki, Protestant na Hindu lakini sasa utashanga utitiri wa dini umekuwa mkubwa lazima serikali idhibiti hali hii, iache ulegelege. Kila mtu anaanzisha kanisa kwa maslahi yake wenzetu waislaam wamejitahidi,” alifafanua Dk Bana.

Aidha aliitaka serikali, kuangalia gharama za huduma zinazotiolewa na taasisi za dini kwa madai kuwa wanatoa huduma kwa gharama kubwa wakati wanapata misamaha ya kodi.

“Ndio! lazima serikali iangalie gharama wanazotoza ni kubwa ukilinganisha na huduma zao halafu wanapata misamaha ya kodi wanapoingiza vitu nchini,” alisema.

Alisema, misamaha ya kodi iwe katika vifaa na magari yanayoendana na mazingira halisi ya maisha ya watanzania na isiwe vya kifahari.

“Kwa maisha ya kitanzania haiwezekani kwamba Kanisa Bakwata linaingiza magari aina ya Landcruiser VX kwa kila kiongozi wake au hata kwa sheikh wa Mkowa, unaweza kuingiza VX ya baba Askofu au ya Mufti lakini sio kila kiongozi,” alisema Dk Bana.

Kwa upande wake Afisa habari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), David Kafulila alisema, kutenguliwa kwa uamuzi wa kufutwa kwa msamaha wa kodi kwa taasisi za dini nchini kumetokana na maamuzi mabovu ya serikali.


Alisema, Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo alisema hawezi kufuta misamaha ya kodi kwa makampuni ya madini hadi hapo watakapokaa na makampuni hayo na kukubaliana lakini kwa mashirika ya dini ilifuta bila ya makubaliano na viongozi wa dini.

“Kutokana na uzembe huo, viongozi wa dini hawakubaliana na uamuzi huo na hatimaye serikali imetengua uamuzi wake. Huku ni kutokuwa makini kwa serikali inapofanya maamuzi yake,” alisema Kafulila.

Aliitaka serikali kuweka wazi mahali itakapopata fedha za kufidia au kugharamia misamaha ya kodi kwa taasisi za dini kwa kuwa haikuwamo katika bajeti na bajeti imepitishwa bila ya marekebisho katika kipengele hicho.

Lwakatare awashukia viongozi wa CUF

Salim Said
ALIYEKUWA Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Tanzania bara, Wilfred Lwakatare amewashushia tuhuma nzito baadhi ya viongozi wa wa Chama hicho akidai kuwa jina lake liliachwa kwenye uteuzi wa kutetea nafasi yake kwa fitina na majungu yaliyojaa CUF.

Alisema, hiyo ndiyo sababu kuu iliyomfanya aandike barua ya kujiuzulu nafasi zote katika chama hicho na kubaki kama mwanachama wa kawaida.

Rwakatare alitoa shutuma hizo kupitia mtandao wa Bidii, ambapo alidai maelezo hayo ndiyo aliyoyawasilisha katika kikao cha Baraza Kuu la Taifa la CUF kilichofanyika tarehe 09/06/2009.

Alisema licha ya chama hicho kuyumbishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), pia kuna baadhi ya wanachama na viongozi wenye tabia mbaya ya majungu na fitina dhidi ya wenzao.

Akieleza alisema maelezo ya Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba kwamba uteuzi aliofanya katika nafasi hiyo bara na Zanzibar ulizingatia kifungu na 68,(l)(i) cha katiba ya Chama sio sahihi, jambo ambalo Lwakatare alisema si kweli.

“Majina hayo yaliteliwa kwa kusikiliza majungu, fitina, njama za unafiki, roho mbaya, uchoyo na mtimanyongo wa baadhi ya wanachama na viongozi wa chama hicho,” alisema Lwakatare.

Lwakatare alimtuhumu Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar ambaye pia ni Mkurugenzi wa Chumi na Fedha Juma Duni Haji kuwa anampikia majungu na ndiye aliyesababisha jina lake kuachwa.

Hata hivyo akijibu tuhuma hizo Duni alisema CUF haina kawaida ya kujibizana na viongozi wake walioacha au kuachwa kupitia vyombo vya habari.

“Sisi CUF hatuna kawaida ya kujibizana na viongozi tuliokuwa nao katika chama na baada ya kujitoa au kuachia ngazi nyadhifa zao kupitia vyombo vya habari,” alisema Duni.

Hata hivyo juhudi za kumtafua profesa Lipumba na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho Ashura Mustafa ambaye alituhumiwa na Lwakatare kwa madai ya kumpakazia kuwa aliangushwa katika unaibu kwa sababu uwezo wake kiutendaji umedidimia (amefulia), hazikufanikiwa.

Matokeo ya wanafunzi wa LST yawa mabovu

Salim Said
MATOKEO ya wanafunzi Chuo cha Sheria yameonyesha kuwa watahiniwa 178 sawa na asilimia 61.1 ya wanafunzi 288, wameshindwa mtihani.

Matokeo hayo ambayo yamebandikwa katika kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani yameonyesha kuwa wanafunzi waliofaulu mtihani huo ni 35 Hayo ni matokeo ya kwanza kwa wanafunzi wa chuo hicho ambao mtihani wao ulifanyika Juni mwaka huu.

Chuo hicho, ambacho ni sehemu ya chuo kikuu cha Dar es Salaam (Udsm) pia kina ofisi zake Ubungo jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa matokeo hayo, jumla ya wanafunzi 178 sawa na asilimia 61.8 wanatakiwa kurudia mtihani wa baadhi ya kozi huku wanafunzi 45 sawa na asilimia 15.6 wameshindwa kabisa.

Wanafunzi 24 kati ya wanafunzi hao 288 ambao ni sawa na asilimia 8.3 waliahirisha kutokana na sababu mbalimbali ambazo hazikutajwa katika ubao huo, huku wengine sita wakiwa wameekewa mapengo.

Matokeo yalionyesha kwamba, watahiniwa waliofaulu zaidi katika mitihani ni wawili ambao wamepata wastani wa pointi (GPA) 2.5 kila mmoja.

Watahiniwa hao walifuatiwa na wenzao wawili waliopata wastani wa pointi (GPA) 2.4 kila mmoja na kufuatiwa na wengine wawili waliopata wastani wa pointi 2.3 kila mmoja. Watahiniwa waliobakia walipata kati ya wastani wa pointi 0.0 hadi 2.3 ambao ndio wingi.

Hata hivyo Mwananchi ilifika katika ofisi za Chuo hicho zilipo katika Jengo la Ubungo Plaza lakini hakukua na muhusika wa kutoa maelezo juu ya matokeo hayo mabovu ya wanafunzi wake katika mitihani.

Juhudi za Mwananchi kutafuta maoni ya utawala wa chuo hicho hazikuishia hapa, ambapo pia ilitembelea tovuti ya chuo hicho kwa ajili ya kutafuta namba za simu ili kufanya mawasiliano lakini pia hazikufaniwa baada ya kukosekana katika tovuti fiyo ya www.lst.ac.tz.

Mwananchi haikuweza kufahamu mara moja sababu za wanafunzi hao kuanguka kama hivyo katika mitihani yao. Hata hivyo juhudi za kuwatafuta wahusika wa chuo hicho ili kufafanua sababu za kuanguka kwa wanafunzi wao zitaendelea leo.

Wednesday, June 17, 2009

Karibu katika maisha mapya ya Tanzania


Mama mongella akikaribishwa mara baaada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J. K. Nyerere jijini Dar es Salaam.

TGNP waisifu bajeti ya Serikali

Salim Said
MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP) umeisifia bajeti ya serikali ya mwaka 2009/10 kwa kuwa imelenga kukuza pato la ndani na kupunguza utegemezi kwa wahisani na misaada ya nje.


Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao huo, Usu Mallya katika taarifa yao kwa vyombo vya habari iliyoandaliwa na timu ya wataalamu wa jinsia na maendeleo katika semina ya wiki moja.

Mallya alisema, bajeti hiyo imewekeza fedha nyingi katika sekta mmuhimu za kijamii na kiuchumi zikiwamo za elimu, kilimo, miundombinu na maji.

“Tumefurahishwa sana na bajeti ya mwaka kwa kutenga fedha nyingi katika vipaumbele muhimu vya kijamii na kiuchumi, japokuwa kuna ukosefu wa taarifa za kuhakikisha fedha hizo zinawafaidisha walengwa,” alisema Mallya na kuongeza:

“Hususan makundi ya watu yanayotengwa na kukandamizwa kimaendeleo ambao ni pamoja na wanawake, waathirika wa virusi vya ukimwi na watu wenye ulemavu.”

Alisema wanakubaliana na mpango wa serikali wa kupunguza matumizi ya fedha za umma kwa katika gharama za safari, semina, makongamano na ununuzi wa magari ya kifahari.

“Japokuwa hii si mara ya kwanza kwa serikali kupitisha maamuzi kama haya, lakini swali la kujiulza hapa ni vipio kuhusu ukubwa wa serikali kuu yenye mawaziri 26,” alisema Mallya.

Alisema, TGNP inaunga mkono juhudi za serikali katika kujinasua na athari za mtikisiko wa kiuchumi duniani, kwa kuongeza uzalishaji wa chakula cha ziada na kuimarisha miundombinu na mawasiliano ili kuweza kuhimili ushindani wa soko la kikanda na kidunia.

“Ni ulinzi wa aina gani ambao serikali imeuweka katika kulinda ajira za watanzania, soko la mazao ya Tanzania na viwanda vidogo na vya kati ambavyo vimeathirika mitaji yao kutokana na mtikisiko wa kiuchumi,” alihoji Mallya.

Alisema, serikali za magharibi zilibaini athari za mitikisiko huo mapema na kuanza kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na hali hiyo katika sekta za uchumi na fedha.

Hata hivyo Mallya alisema, fedha nyingi zinahitajika ili kufikia malengo ya milenia ya usawa wa kijinsia kwa asilimia 50 kwa 50 kati ya wanaume na wanawake, katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani.

Aliitaka serikali kuimarisha wigo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kuongeza kodi kwa makampuni na watu wenye kipato cha juu.

Alitahadharisha kuwa, mzigo wa kuimarisha wigo wa kukusanya mapato ya ndani usiangushwe kwa viwanda vidogo, vya kati, wajasiriamali pamoja na watu masikini pekee nchini.

“Ikizingatiwa kupanda kwa gharama za maisha na kuanguka kwa thamani ya shilingi, mshahara wenye kodi ya asilimia 30, lazima ipande kutoka Sh720,000 hadi Sh1,000,000 au zaidi na wale wa mstari wa chini lazima ipande kutoka Sh100,000 hadi Sh150,000 ili kutoa nafuu kwa watu wenye kipato cha chini,” alisema Malya na kuongeza.

Je, itakuwa bajeti ya Kilimo Kwanza


Salim Said
‘LEO ni siku ya Bajeti’, Zaidi ya Watanzania 40 milioni nchini kote wanaelekeza macho, masikio na hisia zao Mji Mkuu wa Tanzania Dodoma, ambako Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkulo anasimama Bungeni kuisoma bajeti ya serikali kwa mwaka 2009/10.

Kila Mtanzania awe wa mjini au kijijini kuanzia mwanafunzi au mwalimu, mkulima au mfanyakazi, tajiri au masikini, mfugaji au mvuvi na hata mchimbaji madini au mfanyabiashara ana hamu na shauku ya kutaka kujua, iwapo bajeti hiyo itamkwamua kiuchumi, kijamii na kisiasa au itazidi kumdidimiza.

Aidha, mwelekeo huo wa bajeti ya 2009/10, unaonyesha serikali inatarajia kukusanya Sh9.5 trilioni ikilinganishwa na Sh7.3 trilioni za mwaka 2008/09, ambapo pato la ndani litachangia Sh5.1 trilioni, misaada na mikopo ya nje Sh3.2 trilioni na Sh1.2 trilioni zitatoka katika mapato mengine, huku matumizi ya kawaida yakitarajiwa kuwa Sh6.7 trilioni na maendeleo Sh2.8 trilioni.

Mtanzania wa kila rika na daraja ana hamu ya kujua ni mambo gani ambayo yamepewa kipaumbele katika bajeti ya mwaka huu, je ni masuala Mtambuka (cross cutting issues) au sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Bajeti ya mwaka 2008/2009 ilitoa kipau mbele katika sekta nne kubwa ambazo ni elimu, miundombinu, kilimo na afya, swali ni je, bajeti ya mwaka huu ni sekta gani, zitapewa kipaumbele na kuongezewa gawiwo au fungu la fedha?

Wakati waziri Mkulo anasimama bungeni leo kwa muda wa masaa kadhaa kusoma kurasa, aya na maelfu ya maneno ya maelezo ya bajeti hiyo, jamii ya kitanzani inakabiliwa na changamoto kubwa ya athari ya mtikisiko wa kiuchumi unaoendelea kuikabili dunia.

Upepo unaonesha, bajeti ya mwaka huu inaakisi wazi kuwa, vipaumbele vitatu vya kwanza ni elimu sh1.7 trilioni 2009/10 kutoka sh1.4 mwaka jana, miundombinu sh1.0 trilioni mwaka huu kutoka sh973.3 bilioni mwaka Jana na kilimo iliyoongezewa fungu kutoka sh513 bilioni 2008/09 hadi sh666.9 bilioni 2009/10 sawa na ongezeko la asilimia 30.

Vipaumbele vingine ni afya sh963.0 bilioni kutoka sh910.8 bilioni mwaka jana, maji sh 347.3 bilioni mwaka huu kutoka sh231.6 mwaka jana na nishati.

Waziri Mkulo anasema, bajeti ya 2009/10 ni ya kilimo kwa kuwa mkazo utawekwa katika kuhakikisha serikali inaimarisha sekta ya hiyo, baada ya kuathirika mno na mtikisiko wa kiuchumi duniani, ikiwa na sura ya sekta mama ya kiuchumi na kijamii.

“Kwa Tanzania madhara ya mikisiko huo yamejitokeza katika kilimo, ambapo wauzaji wa mazao ya pamba, kahawa, katani, korosho na maua wameathirika kutokana na kuanguka kwa bei za bidhaa katika soko la dunia,” anasema Mkulo.

“Lakini serikali tayari imeanza kuinusuru nchi hasa sekta ya kilimo kutokana na athari za kuadimika kwa chakula duniani zilizochochewa na mtikisiko huo pamoja na hali mbaya ya hewa.”

Anasema, licha ya fungu la kilimo kuzidiwa na sekta nyingine mbili yani elimu na miundombinu, lakini mkazo mkubwa utawekwa katika kilimo kwa upekee, ili kuhakikisha mabadiliko yanapatikana katika sekta hiyo.

“Kauli mbiu ya bajeti ya 2009/10 ni ‘Kilimo Kwanza’ ambapo serikali itaweka mkazo katika kupanua na kuboresha kilimo kwa mapana yake, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa mbolea, madawa, mbegu bora, zana za kilimo, huduma za ugani na mikopo nafuu kwa ajili ya kilimo,” anasema Mkulo.

Waziri Mkulo anasisitiza, “katika bajeti ya 2009/10 serikali itahakikisha kupanua miradi ya kilimo cha umwagiliaji, lengo ikiwa ni kuwahikikishia watanzania upatikanaji wa chakula cha kutosha na kuongeza uzalishaji na ubora wa mazao ya biashara.”

Anasema, serikali pia katika bajeti hiyo, itaongeza kasi ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) na mikakati ya kukabilaina na athari za kuporomoka kwa uchumi wa dunia, hususan katika sekta ya kilimo.

Ili kuthibitisha nia ya dhati ya serikali katika kuimarisha sekta ya Kilimo Mkulo anasema, “kwa mwaka huu wa bajeti wataongeza wigo wa upatikanaji wa mikopo, hususan katika sekta ya kilimo kwa kuanzisha benki ya Kilimo na ya Wanawake ili kuongeza uzalisaji wa mazao ya chakula.”

Kabla ya Mkulo kusema haya, serikali ilishaanza kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha inaboresha sekta ya kilimo nchini, ambapo Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda alipiga marufuku uendeshaji wa semina, warsha na makongamano na ununuzi wa magari ya kifahari ya serikali, ili kupunguza matumizi mabaya ya fedha za umma.

Badala yake anataka fedha hizo zitumike katika kununulia matrekta na kuyasambaza katika maeneo muhimu ya kilimo nchini, ili kuimarisha sekta hiyo na kuwaondoa wakulima katika kilimo cha jembe la mkono na kuwapeleka katika kilimo cha biashara.

Pinda anasema atahakikisha, analibeba ipasavyo suala la kuleta mageuzi katika kilimo kwa kuhakikisha upatikanaji wa matrekta kwa wakulima na kusisitiza, wizara na idara nyingine za serikali hazina budi kuimba wimbo mmoja wa ‘Kilimo Kwanza’, hadi yapatikane mageuzi katika sekta hiyo.

Pamoja na hayo ya Pinda, Rais Jakaya Kikwete naye aliitangaza baadhi ya mikoa kuwa ni maeneo muhimu kwa kilimo ambayo ni pamoja kuutangaza mkoa wa Morogoro kuwa ghala la taifa la chakula.

Aidha, Rais Kikwete anasema taifa limepata mafanikio makubwa katika sekta ya elimu nchini ambapo wamefanikiwa kujenga shule ya sekondari katika kila kata na nyengine zikiwa na shule zaidi ya moja na ndio mana mkazo sasa ukawekwa katika kilimo.

Lakini baadhi ya wabunge nao wanazipokeaje juhudi hizi za serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa chakula na upanuzi na uimarishaji wa sekta ya kilimo chini ya mwevuli wa kauli mbiu ya ‘Kilimo Kwanza’?

Omar Saddiq mbunge wa Mvomero (CCM) anahoji namna serikali inavyoyafanyia kazi maeneo ya vipaumbele vya bajeti, akidai hadi sasa kila mwaka serikali inatangaza vipau mbele, lakini hajaridhika na namna vinavyofanyiwa kazi.

“Taifa haliwezi kujinasua hata kidogo kiuchumi na kijamii bila ya viwanda, hivyo serikali inatakiwa kuandaa mkakati maalum wa kuanzisha, kufufua na kuboresha viwanda vya ndani,” anasema Saddiq na kusisitiza:

“Haya matarakimu ya serikali imetenga fedha kiasi gani hayana maana kwa mwananchi wa kawaida na wala hana habari nayo, anachohitaji ni kupata maisha bora. Mkazo wa ajira katika sehemu nyeti za kilimo, elimu, afya na miundombinu lazima uwekwe.”

Monica Mbega (CCM) kwa upande wake analia na watoa mikopo wanavyowakandamiza na kuwazidishia umasikini wakopaji wadogowadogo kwa kuwatoza kiwango kikubwa cha riba na kuhoji.

“Je wataalamu wetu wa Wizara ya Fedha na Uchumi pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wanafanya nini ili kuhakikisha watu wengi wanapata mikopo tena kwa riba na masharti nafuu kwa ajili ya kuongeza shughuli za kilimo kama sekta ya kiuchumi nchini.”

Anafafanua, Wizara ya Fedha na Uchumi na Wizara ya Kilimo na Mifugo ni wizara zinazotegemeana sana, lakini hajui ni kwa kiwango gani zinashirikiana, ili kuhakikisha vocha za mbolea zinawafikia wakulima kwa wakati.

“Naomba wizara hizi zishirikiane kwa karibu ili kuhakikisha vocha za mbolea zinawafikia wananchi mapema mwezi Agosti, ili mvua za vuli zikianza zikute tayari mbolea imemfikia mkulima,” anaomba Mbega.

Naye, Devotha Likokola viti maalum (CCM) anasema, duniani kote Benki Kuu zinasimamia shughuli za Makbwela (microfinance), lakini anahoji BoT inafanya kazi gani?

Dk. Mreru Omar mbunge wa Morogoro Mjini (CCM) anasema, Rufiji na Morogoro ni maeneo muhimu kwa kilimo na kwamba yanaweza kuliokoa taifa kwa muda mfupi.

“Hatutaki mbolea sisi, tunachohitaji ni vitendea kazi, ukituletea mbolea unaharibu rasilimali. Sisi tuletee matrekta, mbegu bora na wataalamu na ndio mana rais Kikwete, akautangaza mkoa wetu wa Morogoro kuwa ghala la taifa la chakula, anasema Dk. Mzeru.

Juma Siraju Kaboyonga mbunge wa Tabora Mjini (CCM) anasema,“Tukubali tusikubali lakini riba katika mabenki na taasisi za fedha nchini ni tatizo na kikwazo kwa maeneleo ya kilimo. Sisi tukiweka fedha benki riba yake ni asilimia 3, lakini ukikopa ni asilimia 18 hadi 20.”

Anashauri, “Tuache kutumia fedha za umma katika kusafirisha warembo na timu za mpira nje ya nchi kwa gharama kubwa, badala yake tupeleke fedha hizo katika kilimo.”

Kaboyonga anaonesha hofu yake kuhusu kauli mbiu ya ‘Kilimo Kwanza’ akisema, “Hiyo ni misemo tu ya kisiasa, lakini kinachohitajika ni utendaji na ufanisi.”

“Zimepita nyingi kama hizo ikiwa ni pamoja na ‘Kilimo ni uti wa Mgongo, Siasa ni Kilimo, Kilimo ni Sekta Kiongozi na sasa Kilimo kwanza’. Tunahitaji uwezeshwaji na ufanisi wala si misemo ya kisiasa.”

Mkulo: Pato la taifa litaanguka hadi 2011

Salim Said
WAKATI ukuaji wa uchumi katika mataifa ya Ulaya na Marekani ni wa kukimbia, ule wa nchi za Afrika unazidi kudorora kwa kurudi nyuma hatua kadhaa badala ya kusonga mbele.

Haya yanathibitishwa na Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkulo katika ripoti yake ya kurasa 26, kuhusu ‘Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2008 na Malengo ya Uchumi Katika Kipindi cha Muda wa Kati (2009/2010 hadi 2011/2012)’.

Waziri Mkulo anathibitisha katika ripoti hiyo, kuanguka kwa pato la taifa kulikosababishwa na kuyumba na kutikisika kwa uchumi wa dunia kuanzia Marekani, Ulaya hadi Afrika.


Awali, kabla ya Mkulo kukiri kuanguka kwa uchumi wa taifa, wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kiuchumi, walidokeza anguko hilo wakiwamo, Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini Esther Mkwizu.

Wachambuzi hao walisema, mtikisiko wa kiuchumi unaoendelea kuikumba dunia una sura ya herufi ‘L’ ikiwa na maana kwamba, uchumi utaanguka hadi chini na utakaa kwa muda wa miaka mitatu hadi mitano ndipo utanyanyuka na kutengamaa.

Kwa mujibu wa wachambuzi hao, hiyo inasababishwa na benki na kampuni kubwa za kimataifa kuanza kufilisika, huku shughuli za kiuchumi zikizidi kuanguka licha ya benki hizo, kushusha riba hadi asilimia 0.0.

Maneno haya ya profesa Lipumba na Mkwizu yanathibitishwa na waziri Mkulo kwa kusema, pato la taifa kwa mwaka 2009 litaanguka kwa asilimia 2.4 ambapo ukuaji wake utakuwa ni asilimia 5.0 ikilinganishwa na asilimia 7.4 mwaka 2008 na asilimia 7.1 mwaka 2007.

Mkulo anasema, ukuaji huo wa pato la taifa mwaka 2008, ulichangiwa zaidi na kuongezeka kwa viwango vya ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika sekta ya kilimo, uvuvi na huduma.

Anasema, ukuaji wa viwango vya juu vya pato la taifa mwaka 2008 ulijionesha katika shughuli ndogo ndogo za kiuchumi za mawasiliano asilimia 20.5, fedha 11.9 na ujenzi asilimia 10.5.

“Hata hivyo kiwango cha ukuaji katika shughuli za kiuchumi za viwanda na ujenzi kilipungua kidogo ikilinganishwa na mwaka juzi,” anasema Mkulo.

Kwa mujibu wa Mkulo, pato la taifa si tu kuwa litaanguka kwa mwaka 2009, bali litaendelea kudorora katika kipindi chote cha muda wa kati ambapo mwaka 2010 ukuaji ni asilimia 5.7 na kwamba pato hilo litatengamaa mwaka 2011/2012 kwa kufikia kiwango cha asilimia 7.5.

“Ili kukabiliana na hali hiyo, serikali inatambua mchango wa sekta binafsi katika kukuza pato la taifa na kupunguza umasikini na kwa kuzingatia hilo hatua zinachukuliwa kuboresha mazingira ya kuziwezesha sekta hizo kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi,” anasema Mkulo.

Anasema, serikali ina mpango wa kukamilisha sera ya ubia kati ya sekta ya Umma na Binafsi (PPP Policy) ili kuharakisha maendeleo ya sekta binafsi na kuongeza mchango wake katika kukuza uchumi na kupunguza umasikini nchini.

Anasema, pia serikali itaongeza ufanisi katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na huduma, biashara, kilimo, uwekezaji na kupunguza matumizi ya serikali yasiyo ya lazima katika mapato yake.

Mkulo ansema, serikali kwa kuzingatia chanzo cha mtikisiko huo, Benki Kuu (BoT) imeanzisha utaratibu wa uangalizi na usimamizi wa taasisi za fedha kila siku, ili kubaini matatizo yatakayojitokeza na kuchukua hatua za haraka.

“Kwa kupunguza makali na kuhimili shinikizo la mtikisiko huo hususan katika kuwalinda wananchi walio kwenye hatari kubwa zaidi, Serikali inalinda ajira, hasa katika shughuli zitakazokumbwa na ukwasi kutokana na kupungua kwa utashi wa bidhaa na huduma wanazotoa,” anasema Mkulo.

Anasisitiza, ili kuinusuru nchi kutokana na athari za kuadimika kwa chakula, serikali inaongeza kasi katika kilimo, kulinda programu muhimu za kijamii na uwekezaji kwa maendeleo ya nchi.

Huku pato la taifa likiporomoka kwa asilimia 2.4 kwa mwaka 2009, nchi inakabiliwa na matatizo ya mfumko wa bei, kushuka kwa thamani ya sarafu mambo ambayo, serikali inasema haina uwezo wa kuyadhibiti kwa madai kuwa ni ya kimfumo na yanategemea zaidi nguvu ya uchumi wa soko.


Waziri Mkulo, anasema tatizo la kushuka kwa thamani ya sarafu halizuiliki kwa sababu ni la kimfumo na linasababishwa na mfumuko wa bei za bidhaa muhimu na upatikanaji wa fedha za kigeni, ambao ni wa msimu. “Mheshimiwa Mwenyekiti tutake tusitake, tatizo la kupanda na kushuka kwa sarafu ya Tanzania lipo na serikali haiwezi kulizuia kwa sababu ni la kimfumo,” anasema Mkulo.

Anafafanua, kinachofanywa na serikali kukabiliana na tatizo hilo ni kuangalia iwapo mzunguko wa shilingi ya Tanzania unaendana na uchumi wa soko au vinginevyo.

“Kama mzunguko ni mbaya tunaweza kuingilia na kurekebisha lakini, kama unaendana na uchumi wa soko, hatuwezi kuingilia hata kidogo,” anasisitiza Mkulo.

Mkulo anathibitisha, “Upatikanaji wa fedha za kigeni nchini kuwa ni wa msimu hususan wa mavuno kuanzia Juni hadi Disemba ya kila mwaka, lakini pia tukiweza kudhibiti mfumko wa bei za bidhaa muhimu tunaweza kudhibiti thamani ya Shilingi yetu.”

Kwa mujibu wa Mkulo, thamani ya Shilingi ya Tanzania imeshuka hadi kufikia wastani wa Sh280.30 kwa Dola ya Marekani Desemba mwaka jana ikilinganishwa na Sh1,132.09 Desemba 2007.
Anasema, mfumko wa bei kwa mwaka 2008, ulikua kwa asilimia 10.3 ikilinganishwa na asilimia 7.0 mwaka 2007, ambapo kiwango cha chini cha kasi ya mfumko huo 2008, ilikuwa Januari kilipopanda kwa asilimia 8.6 na kiwango cha juu asilimia 13.5 Disemba mwaka huohuo. “Lengo letu la ukuaji wa mfumko lilikuwa asilimia 5.0 Juni 2008, lakini halikufikiwa kutokana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji hasa baada ya kupanda kwa bei ya nishati hususan mafuta na umeme,” anasema Mkulo na kuongeza:

“Hadi April 2009, mfumko ulifikia asilimia 12.0 kutokana na hali hiyo, ambapo awali lengo la mfumko huo lilitarajiwa liwe chini ya asilimia 7.5 ifikapo Juni 2009, lakini sasa tunatarajia asilimia 11.0 ya mfumko.”

Mkulo anasema, ili kuhakikisha wanarudisha utengamano wa pato la taifa serikali itakabiliana na mtikisiko wa uchumi duniani, kuongeza uwekezaji katika maeneo ya mwingiliano wa kisekta hususan kilimo, miundombinu, uzalishaji viwandani na nishati ikiwa ni pamoja na kuhimiza ushirika wa sekta binafsi katika maeneo hayo.

“Serikali itaongeza upatikanaji wa mikopo hasa kwa sekta ya kilimo kwa kuwa na benki ya kilimo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula,” anasema Mkulo.

Anasema, serikali itaongeza na kuboresha mapato ya ndani ili kugharamia sehemu kubwa ya matumizi ya serikali, kuimarisha usimamizi katika matumizi ya fedha za umma na kuendelea kulinda mafanikio yaliyopatikana.

“Serikali itaendelea kulinda na kuimarisha mafanikio yaliyopatikana katika sekta za kijamii na kuboresha utoaji wa huduma ili kuongeza wigo wa ukusanyaji na ukuzaji wa pato la taifa,” anasema.

Anasema, serikali pia itaongeza na kuboresha mipango ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na kuongeza ajira pamoja na kupima ardhi ya vijijini ili wamiliki waweze kutumia hati zao kupatia mikopo.

Tuesday, June 16, 2009

Regia Mtema: Ni mlemavu wa viungo, si wa kufanya kazi



Salim Said
“MIMI ni mlemavu wa kimaumbile wala si mlemavu katika kazi, lakini kuna watu ni wazima kimaumbile, lakini ni walemavu kwenye kazi,” hivi ndivyo anavyoanza Regia Mtema katika mazungumzo yake na Mwananchi.

Mtema msichana ambaye ni Afisa Mafunzo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Kurugenzi ya Organaizesheni, anasema ulemavu wake haumzuii wala kumpunguzia uwezo wake wa kufanya kazi.

Kielimu Mtema ni muhitimu wa Shahada ya kwanza katika Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sua) kwenye fani ya Sayansi ya Uchumi na Lishe.

Anasema, amejipatia elimu yake ya Msingi katika shule ya msingi Mchikichini Ilala kuanzia mwaka 1989 hadi 1995, huku elimu ya kidato cha kwanza hadi cha nne akiipatia katika shule ya Sekondari ya Forodhani kuanzia mwaka 1996 hadi 1999 zote za jijini Dar es Salaam.

Mtema anasema, alichaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya Benjamin Mkapa katika Mchepuo wa Kemia, Biolojia na Lishe (CBN) mwaka 2000, lakini aliomba uhamisho ili kwenda shule ya sekondari ya wasichana ya bweni Machame Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro, kwa kuwa kutokana na hali yake alishachoka kusoma shule za kwenda na kurudi.

“Nilianza kuvutiwa na siasa tangu sekondari, lakini nilishindwa kujiunga na chama chochote cha siasa, kwa sababu sekondari za zamani zilikuwa hazina masuala ya siasa tofauti na sasa, ambapo matawi ya vyama yapo hata katika shule hizo,” anasema Mtema.

Anasema, akiwa Machame alivutiwa na Chadema, baada ya kutembelewa na Mwenyekiti wa sasa wa Chadema Freeman Mbowe alipokwenda kuwatembelea wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2000, wakati huo akiwa ni mgombea ubunge wa jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro.

“Nilivutika sana na Chadema nilipokutana na Mbowe alipokuja shuleni kwetu kuomba kura mwaka 2000 akiwa ni mgombea ubunge, alinivutia sana na sera za chama chake, ingawa sikujiunga na chama kwa wakati huo, tena alishinda,” anasema Mtema.

Baada ya kuhitimu kidato cha tano na sita Mtema anasema, alijiunga na chuo cha kilimo Sua, kuanzia mwaka 2003 hadi 2006 ambapo alifanya, fani ya Sayansi ya Uchumi na Lishe na huko ndiko alikopata uamuzi wa kujiunga na siasa rasmi yani chama cha Chadema.

“Nilijiunga na Chadema nikiwa Sua mwaka 2005 kufuatia vuguvugu la kisiasa vyuoni,” anasema Mtema.

Anasema, baada ya kukamilisha masomo yake chuoni hapo, mwaka 2007 aliamua kujiunga na Chadema Makao Makuu akiwa ni Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Vijana na Wanawake, iliyokuwa ikiongozwa na Mkurugenzi wake John Mnyika.

Anasema akiwa katika nafasi hiyo, alipata uzoefu kwa kujifunza mambo mingi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii huku akipata msaada mkubwa wa mafunzo na maelekezo ya kazi kutoka kwa Mnyika.

“Awali nilipofika makao makuu kuna wengine walidhani kama sitaweza kufanya kazi na wengine waliona nitaweza, lakini kwa ushirikiano na wenzangu nimefanikiwa sana,” anasema.

Mtema anafafanua kwamba, baada ya mabadiliko ya uongozi ndani ya kurugenzi mbalimbali za chama chao Januari mwaka huu, aliteuliwa kuwa Afisa Mafunzo katika Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo ya Chadema.

“Hii ni sababu na ushahidi tosha kwamba kazi zangu zinakubalika kwa kuwa kama hazikubaliki nisingeteuliwa katika nafasi hii hata siku moja,” anajisifia Mtema.

Anasema, ameamua kujiunga na siasa na kuacha kazi nyingine za kuajiriwa, kwa sababu anaamini kuwa, katika siasa ni rahisi kwa mtu kutoa maoni yake na kusikilizwa pamoja na kufanyiwa kazi kwa haraka.

“Mimi ni mlemavu, lakini nyuma yangu kuna walemavu wengi, ambao hawajapata elimu kwa sababu mbalimbali zikiwamo mitazamo potofu ya jamii, juu ya watu wenye ulemavu, na kama huna elimu huwezi kuajiriwa, hivyo niliamini kuwa ipo siku moja nipata nafasi ya kuwasaidia japo kufikisha kero zao serikalini,” anasema Mtema na kusisitiza:

“Nilitaka kuja kuwasaidia wenzangu, kwa sababu kwenye siasa ndio mambo yote yanakofanyika. Utungwaji wa sera, sheria, usimamizi na marekebisho yake yanafanyika katika siasa, nilipenda na mimi niwe miongoni mwa watunga sera, sheria na hata warekebishaji.”

Akizungumzia changamoto kazini Mtema anasema, kwanza alipata ugumu kutoka katika familia yake kwa sababu hawakuwa tayari mtoto wao ajiunge na kazi ya siasa kutokana na imani waliyonayo kwamba, siasa ni fujo, vurugu na mchezo mchafu.

“Hofu yao kubwa ilikuwa ni kupoteza maadili kwa sababu wanaona siasa labda ni uhuni na ni kazi isiyo na heshma. Lakini nilitumia ujanja bila ya wao kujua,” anasema na kutoa mfano wa ujanja aliyotumia:

“Kwa mfano, baba yangu mzazi alijuwa kuwa mimi ni mwanasiasa wa Chadema Makao makuu baada ya miezi miwili, licha ya kuwa nilikuwa nalala nyumbani mwake, nakula chakula chake na nilikuwa napanda gari baadhi ya wakati kwa fedha yake, alikuwa ananiona natoka asubuhi narudi jioni, tena alijua kupitia mtu mwingine sio mimi.”

Anasema, baada ya kuja walisikitika sana, lakini ilibidi wakubali matokeo na mpaka leo hawaridhiki mimi kuwa mwanasiasa na hii inatokana na tafsiri mbaya ya siasa katika jamii kuwa ni fujo, mikiki mikiki na uovu.

Mtema anasimulia kuwa, kwa upande wa changamoto kazini, “Nilipoonekana kuwa ni mlemavu maswali yalikuja ataweza kweli? na wengine walikuwa wanaongea pembeni, na kunihukumu kuwa siwezi tu, lakini baadhi waliona naweza kina Mnyika na nimefanya nao kazi vizuri sana.”

Anasema, kwa wale walimuamini na kumkubali kuwa anaweza, wamethibitisha kwa sababu ndani ya muda wake Chadema ameweza kufanya kazi vizuri, tena wakati mwingine kuliko hata wale waliowazima na wakamilifu wa kimaumbile.

“Ulemavu wangu ni wa kimaumbile tu lakini si katika kazi,” anasema Mtema.

Anasema, baadhi ya wakati akipanda Jukwaani kabla ya kuhutubia umati wa watu katika mkutano, huwa anashangiliwa sana jambo ambalo anasema humpa maswali mingi bila ya majibu, iwapo kelele hizo ni za kukubalika kwake au la.

Mtema anasena amefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kazi ya siasa hasa akiwa makao makuu ya Chadema na kwamba matarajio yake kwa sasa ni kugombania nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Baraza la Vijana la Chadema katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu.

“Nikifanikiwa kushinda nitakuwa nitatengeneza historia kwa sababu nitakuwa msichana na mlemavu wa kwanza Tanzania kuwa katibu mkuu wa baraza la vijana katika vyama vyote,” anasema Mtema.

Sambamba na hilo, Mtema anasema anatarajia kujitupa Jimboni kugombea ubunge katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kama Mwenyezi Mungu atamueka hai na mzima.

“Kwa mwaka 2010 ni ngumu kuingia jimboni, lakini matarajio yangu ni kuijtupa huko katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, kwa sababu jamii bado haijawakubali ipasavyo walemavu, wanawake na vijana lakini natarajia ikifika muda huo, mwamko utakuwa wa kutosha katika jamii kuhusu sisi,” anasema.

Mbali na kuwa Afisa Mafunzo wa Chadema Mtema ni Mkurugenzi wa Vijana na Michezo katika Chama cha Walemavu Tanzania (Chawata).

Mlowe: Chagueni viongozi, msichague wafadhili

Salim Said
VITA dhidi ya adui ufisadi inaendelea kushika kasi nchini, ambapo watu wengi sasa kwa nafasi zao mmoja mmoja au kupitia jumuiya na madaraka yao wanaamua kuchukua nafasi na hatua.

Hii ni kwa sababu watu wameanza kuelewa kuhusu ubaya na hasara ya ufisadi nchini katika nyanja tofauti za maisha ya jamii, kiuchumi, kisiasa na hata kijamii.

Baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi Taifa, Mikoa, Wilaya hadi Kata, baadhi ya viongozi waliochaguliwa wameonekana kuingia madarakani wakiwa na nia nzuri ya kupambana na ufisadi kwa maslahi ya taifa.

Bononi Mlowe ni Mwenyekiti mpya wa jumuiya ya wazazi kata ya Mabibo jijini Dar es Salaam, anasema kwa muda mrefu watoto wa kitanzania wamekuwa wakikosa ada ya shule na hata vyuo, vitabu vya kusomea na maabara za uhakika na miundombinu mingine ya kielimu kwa sababu ya ufisadi uliokithiri nchini.

Anasema Watanzania wanazidi kuzama katika dimbwi la umasikini na ufukara kwa sababu ya baadhi baadhi ya viongozi kujifanya wafadhili badala ya kuwa viongozi na kuwatumikia wananchi waliowachagua.

“Pengo la walionacho na wasiokuwanacho linazidi kukua siku hadi siku si kwa sababu nyingine bali baadhi ya viongozi ndani ya vyama na serikali kuwa sio waaminifu katika kulinda rasilimali za umma,” anasema Bononi.

Ili kuondokana na tatizo hilo, Bononi anawashauri wapiga kura wote nchini katika chaguzi za ndani ya vyama na zile za kitaifa za viongozi wa serikali, kuwa makini na kutokubali kabisa kumchagua mgombea yeyote kwa sababu ya kugawa fedha wapigakura.

“Tujiepushe na tuwajue wale wote wanaokuja kwetu kuomba kura kwa kigezo cha kugawa fedha kwa wananchi au wanachama wenzao, hao si viongozi bali ni wafadhili na wafanyabiashara,” anasema Bononi na kusisitiza:

“Sitegemei hata kidogo baada ya watoto wetu kukosa ada, baada ya miundombinu yetu kuzidi kuwa mibovu na baada ya mama wajawazito na watato wachanga kupoteza maisha kwa sababu ya ufisadi, halafu mtanzania akakubali kurubuniwa kwa fedha mbuzi, ili atoe kura yake, iwe ndani ya chama au nje ya chama.”

Anasema, ikiwa mtanzania yeyote atakubali kurubuniwa kwa fedha au mchele katika kampeni za uchaguzi ajue kuwa anatengeneza mazingira ya mtoto wake kukosa ada, matibabu na hata miundombinu bora ya kusomea.

Anasema, watanzania wamekuwa wakichagua viongozi kwa miaka mingi, lakini viongozi hao hawawajali wapiga kura wao na badala yake wanaamua kutajirisha matumbo yao.
“Kwa muda mrefu tunaumizwa na viongozi kama hawa sasa imefika wakati wa kuhakikisha kuwa tunaondokana na tatizo la viongozi wafadhili, badala yake tupate viongozi watoa huduma,” anasema Bononi.

Anasema, viongozi wengi wamekuwa wakiingia madarakani wakiwa masikini wasio na kitu, lakini muda mfupi baada ya kuingia madarakani wanaibuka na kuwa matajiri wakubwa nchini na kuanza kutoa misaada kwa watu mbalimbali bila wao kuhoji fedha hizo zimetoka wapi.

“Lazima tuhoji, mtu tulikuwa naye, baadhi ya wakati tumesoma darasa moja kwa nini baada ya muda mfupi kuingia madarakani awe tajiri mkubwa, hivi huu uongozi ni dhamana au biashara,” anahoji Bononi.

Anawataka wananchi kuwakataa wagombea wa vyama vyote vinavyojaribu kuomba kura kwa kutanguliza fedha, kwa sababu kiongozi wa namna hiyo hawezi kuwajali wapiga kura wake, bali kwanza atataka kujilipa fedha zake alizotumia wakati wa kuomba kura.

Bononi anafafanua, tatizo la uporaji wa mali za umma na za chama kwa baadhi ya viongozi linatokana na tamaa kubwa ya mali waliyonayo pamoja na ukosefu wa kazi nyingine za kujitegemea kwa ajili ya kujipatia kipato.

“Uongozi wa kisiasa ni huduma kwa maana kuwahudumia wananchi, lakini watu wengi wanashindwa kuelewa, jambo ambalo huibadilisha huduma hiyo na kuifanya kuwa kazi ya kutafutia fedha au biashara, watu wa namna hii ni hatari na hawatufai,” anasema Bononi.

Anasema, katika awamu yake ya miaka mitano, atahakikisha kuwa anawashawishi viongozi wa jumuiya hiyo kutafuta kazi nyingine kwa ajili ya kujipatia fedha na kuifanya kazi ya uongozi kuwa huduma badala ya biashara.“Wakipata kazi nyingine ya kutafutia fedha watakuwa waaminifu katika mali za chama na ada za watoto wetu, hii itatusaidia kunyanyua maendeleo na kuimarika kwa jamii,” anasema Bononi.

Anasema, lengo la ushawishi huo ni kuhakikisha kuwa wanapata viongozi bora watakaoipeleka mbele jamii ya watanzania na sio bora viongzi watakaoendelea kuididimiza na kuidumaza jamii ya watanzania.

“Tunataka kila mtu ajue kuwa uongozi ni dhamana ya kuwahudumia wananchi na sio kuanza kumaliza ada za watoto na fedha za maendeleo kwa kuifanya dhamana hiyo kuwa ajira,” anasema Bononi.

Anasema, tatizo la ufisadi si tu la kata yake bali ni kitaifa ambapo kumalizika kwake kunahitaji mchango wa kila mtanzania bila ya kujali rangi, dini, itikadi au kabila.

Bononi anasema, atahakikisha kuwa wanaendesha semina za elimu ya uraia kwa viongozi ili kuhakikisha wanawajenga kiuzalendo kwa ajili ya kuwafanya kuwa askari wazuri wa kulinda rasilimali za Umma.

Changamoto kubwa ambayo anaiona iko mbele yake Bononi anasema, watu ambao wanatumia dhamana ya uongozi kama biashara wamejipanga vizuri, wako imara, wana fedha na ni hatari lakini anasema kwa kushirikiana na wananchi inawezekana kuwang’oa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Makete mkoani Iringa Hawa Ng’humbi anasema, kukithiri kwa vitendo vya wizi wa rasilimali wa umma ni matokeo ya kuporomoka kwa maadili miongoni mwa watanzania.

Anasema, ni hatari kubwa kwa kuwa kadiri siku zinavyoenda na ndivyo maadili ya vijana wa kitanzania ambao ndio watakuwa viongozi wa baadaye yanavyozidi kuporomoka.

“Watanzania hasa wazazi tuna kazi na jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa tunajenga na kurudisha maadili mema kwa vijana wetu ili waje waikoe nchi yetu siku za baadaye,” anasema Ng’humbi ambaye pia ni mlezi mkuu wa jumuiya ya wazazi ya CCM kata ya Mabibo.

Ng’humbi anakiri kuimarika kwa vyama vya upinzani nchini jambo ambalo kila chama kinahitaji kuingia madarakani kwa kutumia mbinu na mikakati mbalimbali vilivyojiwekea.

Sunday, June 14, 2009

CHENGE


Chenge

SEMINA


Baadhi ya wajumbe wa Semina ya mafunzo ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu wakisikiliza kwa makini mada iliyokuwa ikiwasilishwa. Kushoto ni Mwenyekiti wa Shirika la Vyama vya Watu hao Tanzania (Shivyawata) Lupi Mwaisak. Pix na Salim Said

NIPO MAKINI NASIKIA


Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu wa Viungo Tanzania (Chawata) Shida Salum akisikiliza kwa makini katika semina ya mafunzo kuhusu Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu jijini Dar es Salaam jana. Pix na Salim Said.

TUPO MAKINI


Afisa Mipango wa umoja wa walemavu znz Salma Saadat (kulia) naMkurugenzi wa Baraza la walemavu znz Abeida Rashid wakiwa katika semina ya mafunzo jijini Dar es Salaam. Pix na Salim Said

Baraza limenisukuma kujiuzulu: Lwakatare

Salim Said na Neema Materu

SIKU moja baada ya Baraza Kuu la Uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) kuwatimua maofisa watatu wa uchaguzi, aliyekuwa Naibu katibu mkuu wa chama hicho,Wilfred Lwakatare, amesema mamuzi hayo ndiyo yaliyomfanya kuwasilisha barua ya kuachia ngazi nyadhifa zake zote ndani ya chama.

Juzi Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba, alitangaza, kuwatimua Maole Kuchilingulo, aliyekuwa Katibu wa Tume ya Uchaguzi ya CUF, Hussein Mmasi na Juma Wandwi wajumbe, baada ya kubainika kuwa walikihujumu chama chao katika uchaguzi mdogo wa Busanda.

Lwakatare ambaye alishawahi kuwa Mbunge wa Bukoba Mjini, alimewasilisha barua ya kujiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya chama hicho na jana alithibitisha habari hizo.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam, alisema amefikia uamuzi huo baada ya kutoridhishwa na uamuzi wa Baraza Kuu la chama hicho.

“Ni kweli nimewasilisha barua hiyo, kwa sababu sikuridhishwa na uamuzi wa vikao vya Baraza kuu wa kuwatimua maAfisa watatu wa uchaguzi wa chama chetu,” alisema Lwakatare.

“Nimeona maamuzi ya baraza hilo si ya mustakbali mzuri ndani ya chama chetu,” alisema.

Kauli hiyo imekuja huku kukiwa na taarifa kuwa, kigogo huyo wa CUF ana mpango wa kukihama chama hicho na kuhamia Chadema.

Lwakatare, alikiri kusikia uvumi huo.

“Hata mimi nasikia hivyo hivyo lakini hakuna mtu rasmi aliyeniambia taarifa hizo. Mimi sina uwezo wa kuzungumzia hilo kwa sababu uamuzi wa hilo wanao wananchi na si mimi,” alisema Lwakatare.

Bajeti yamchanganya Mkulo

Salim Said

KUPOROMOKA kwa uchumi na maandalizi ya kusomwa kwa Bajeti ya serikali 2009/10 vimemchanganya Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo baada ya kusema kuwa watu ambao wanaacha kufikiria bajeti na kuelekeza hisia zao kwenye mambo mengine ni wapumbavu.

Wakati Mkulo akitoa kauli hiyo, mamilioni ya Watanzania waliopanda fedha katika taasisi ya Deci bila kuvuna, hadi sasa hawajui hatma ya mbegu zao baada ya serikali kupitia Wizara ya Fedha na Uchumi kufunga shughuli hizo, kwa madai kuwa ni hatari kwa mali za wanachama.

Mkulo aliyasema hayo juzi saa 8:00 usiku takriban saa 22 kabla ya bajeti kusomwa kwa bajeti katika mahojiano yake na mwandishi wa kituo cha habari cha Wapo jijini Dar es Salaam, kuhusu hatma ya wanachama waliopanda mbegu zao katika taasisi hiyo.

Redio hiyo, kupitia mwandishi wake, ilimuuliza Waziri huyo, hatma ya wanachama wa Deci hasa baada ya wanachama hao, kutishia kuvunja jengo hilo, ili wagawane mali zilizomo.

Kutokana na hali hiyo, Polisi walitumia silaha za moto kutuliza kutawanya wanachama hao ofisini hapo, ili kutuliza amani kwa watendaji wa taasisi hiyo na mali zao.

Mkulo alipoulizwa hatma ya wanachama hao alijibu kuwa, mtazamo wa watu wengi hivi sasa uko katika suala la bajeti na kwamba hawafikirii suala la taasisi hiyo.

“Mtazamo wa watu wote sasa wenye akili wanangojea bajeti, nasema mtazamo wa watu wazima wote wenye akili timamu wanataka kusikia bajeti,” alisema Mkulo.

Alisema suala la hatma ya wanachama wa Deci ni muhimu kuzungumziwa hivi sasa katika jamii kwa kuwa wengi wao wanataka kujua hatma ya mbegu zao.

Alipoulizwa endapo ripoti ya tume iliyoundwa na serikali kuchunguza masuala ya taasisi hiyo, nayo itatoka baada ya bajeti au la, Mkulo alijibu kwa jazba na hasira huku akiangusha matusi kwa mwaandishi huyo.
“Sio siri, kama hiyo ni muhimu kwako jijibu mwenyewe,” alijibu Mkulo.

Hata hivyo juhudi za kumpata Mkulo kuzungumzia suala hilo, hazikufanikiwa baada ya simu yake ya mkononi kutopokelewa mara kadhaa.

Kilimo Kwanza ni kitendawili cha kejeli-Lipumba

Wakati huohuo, Chama cha Wananchi (CUF), kimeitaka serikali ya Muungano na ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuhakikisha zinawasilisha bajeti za mwaka wa fedha 2009/10 zitakazowajali wananchi wa kawaida.

Akiwasilisha maazimio ya Baraza Kuu la uongozi la chama hicho kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema bajeti nzuri ni ile itakayowajali wananchi wa kawaida ili kuwapunguzia ukali wa maisha.

“Serikali lazima ijipunguzie mafungu ya matumizi ya anasa kwa lengo la kuwajali wananchi wa kawaida kwa kupeleka fedha nyingi katika miradi itakayoinua uchumi wa nchi na kuongeza ajira kwa vijana wetu,” alisema Profesa Lipumba na kuongeza:

“Baraza kuu la uongozi la CUF linawataka mawaziri wa fedha wa serikali zote mbili kuonyesha katika hotuba zao za bajeti, mwelekeo wa serikali hizo katika kukabiliana na athari za mtikisiko wa uchumi duniani na vipi nchi itaweza kujikwamua kiuchumi”.

CUF inasikitishwa na ongezeko kubwa la watanzania wanaoishi katika dimbwi la umasikini na kwamba uchauni wa kaya unaendelea kudoro badala kukua hivyo kuwasababisha umasikini kupanda kwa kasi.

“Kwa watanzania waliowengi kauli mbiu ya ‘Maisha bora kwa Kila Mtanzania’ bado ni kitendawili cha kejeli kinachoteguliwa kwa maisha ya dhiki kila kukicha,” alisema Profesa Lipumba.

CUF yawatimua maafisa watatu kwa usaliti chamani

Salim Said

CHAMA Cha Wananchi (CUF), kimewatimua maafisa wake watatu wa uchaguzi kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Busanda.

Uamuzi huo uliofikiwa katika kikao cha Baraza Kuu kilichomalizika jana jijini Dar es Salaam baada ya wajumbe kuridhika kuwa moja ya sababu za CUF kushindwa katika uchaguzi huo uliompa ubunge mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni usaliti huo uliofanywa na maafisa wake.

Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, Baraza limefikia uamuzi huo kulinda maslahi ya chamasema, baraza kuu liliamua kuchukua uamuzi huo baada ya kujiridhisha na makosa ya watu hao, ili kulinda maslahi ya chama chao.

Aliwataja maafisa hao kuwa ni Husein Mmasi aliyekuwa msimamizi wa shughuli zote za kuandaa mawakala katika uchaguzi huo, Katibu wa Tume ya Uchaguzi ya CUF Maole Kuchilingulo na Juma Wandwi, aliyekuwa mjumbe wa tume ya uchaguzi wa chama hicho.

Alisema mbali na uamuzi huo wa kuwavua madaraka, Baraza limetoa onyo kali kwa maafisa hao na kuweka wazi kuwa hakitovumilia vitendo vya aina hiyo wala kusita kuwaadhibu viongozi na watendaji wa chama kwa uzembe au hujuma.

Akielezea kwa undani tukio hilo, Profesa Lipumba alisema siku tatu kabla ya uchaguzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ilitangaza kuwafuta mawakala wa wa CUF, kwa kuwa majina yao hayakupangwa kwa mujibu wa vituo vya kupigia kura, kama sheria ya uchaguzi inavyotaka.

“Baraza kuu limeridhika kwamba kuzuiwa kwa mawakala wetu kulitokana na hujuma ya afisa wa ndani ya chama, kwa kutotekeleza kwa makusudi masharti hayo ya kisheria,” alisema profesa Lipumba.

Pia aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Wilfred Lwakatare ameamua kuachia ngazi nafasi zote za uongozi ndani ya Chama hicho kwa kile kilichoelezwa kuwa, anataka kurudi Jimboni kwake Bukoba kwa ajili ya kuimarisha chama chao.

Profesa Lipumba alithibitisha kupokea barua ya maombi ya kuachia ngazi kwa Lwakatare wakati wa kikao cha Baraza hilo, kilichoanza Juni 8 hadi 9 mwaka huu, akitaka kurudi jimboni kwake kuimarisha chama.

“Chama chetu ni cha demokrasia na katika demokrasia huwezi kumkataza mtu kujiuzulu, lakini hatujamjibu barua yake. Lwakatare tulikuwa naye na kushirikiana naye kwa mambo mingi na pia tutaendelea kushirikiana, ila kwa sasa ameamua kuwa mwanachama wa kawaida tu,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema, Lwakatare hajawahi kutuhumiwa na kashfa ya aina yoyote ndani ya chama na wala hajashinikizwa na mtu yoyote kujiuzulu, ila ameamua mwenyewe kujiuzulu na sisi kama Baraza kuu la uongozi hatuwezi kumzuiya kujiuzulu.

Aidha Profesa Lipumba alisema, CUF imeandaa operesheni maalumu kwa ajili ya uzinduzi na kuitangaza dira ya mabadiliko (vision for changes) ya chama chao ijulikanayo kwa jina la ‘Operesheni Zinduka’ itakayoanza Julai mosi mwaka huu.

“Operesheni hii itaongozwa na viongozi wa CUF na itatembea katika kanda zote saba za chama chetu, zikiwamo tano za Tanzania bara na mbili za Zanzibar kwa ajili ya kuwazindua wananchi kuelekea uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu na ule wa taifa mwakani,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema katika hatua ya awali operesheni hiyo itanzia katika kanda ya Ziwa na kanda ya Dar es Salaam Julai mosi mwaka huu.

Wakati huohuo Profesa Lipumba aliwataka waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk. Hussein Mwinyi na Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Devis Mwamunyange, kuwajibika kwa kujiuzulu mara moja kufuatia uzembe wa mamlaka wanazoziongoza, uliosababisha milipuko ya mabomu Aprili 29 mwaka huu na kusababisha maafa makubwa kwa wananchi.

“Baraza kuu linalaani vikali ubaguzi wa dhahiri uliofanywa na unaondelea kufanywa kwa misingi ya kisiasa katika uhakiki na ugawaji wa misaada kwa waathirika wa milipuko hiyo,” alisema.

Alifafanua kuwa, baraza kuu la uongozi la CUF linalaani vikali matamshi ya dharau nay a kejeli yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Willim Lukuvi, ya kuwataka wananchi wa Mbagala kuzoeya milipuko ya mabomu na kuichukulia kama sehemu ya maisha kama wananchi wa Kipawa walivyozoeya sauti za ndege zinazoruka mara kwa mara katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.

“Matamshi hayo yanaonesha dharau ya hali ya juu kwa wananchi walioathirika na vitendo vilivyosababishwa na uzembe na kutowajibika kwa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM),” alisema Profesa Lipumba.

Aliwata Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Machano Othman Said na Mkurugenzi wa Bandari ya Zanzibar Mustafa Aboud Jumbe, kuwajibika kwa kujiuzulu mara moja kutokana na uzembe wa mamlaka wanazoziongoza uliosababisha vifo vya wananchi na hasara ya mali baada ya Meli ya MV Fatih kuzama ikiwa bandarini.

“Baraza linasikitishwa na uzembe uliofanywa na watumishi wa bandari ya Zanzibar kiasi cha Meli kuzama ikiwa bandarini nakupoteza maisha ya wananchi ambayo yangeweza kuokolewa,” alisema Lipumba na kusisitiza.

“Baraza kuu la CUF linazitaka serikali ya Muungano na ile ya Zanzibar kuunda tume huru zikiwashirikisha wajumbe wa kambi ya upinzani Bungeni na katika baraza la wawakilishi wa Zanzibar kuchunguza chanzo cha milipuko na kuzama kwa meli ya MV Fatih na baadaye kutoa ripoti kwa wananchi.”

Kikao cha baraza kuu la uongozi la CUF kilimalizika juzi baada ya wajumbe kupitisha maazimio mbali mbali ya kiutendaji na kuhimiza uwajibikaji kwa serikali ya SMZ nay a Muungano.

Tuesday, June 9, 2009

Tani 3.8 za dawa zilizopita muda wa matumizi zateketezwa Dar

Salim Said

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), imeteketeza tani 3.8 za dawa za Viuavijasumu (antibiotics) jamii ya ‘Pencillin’, Unga wa Sindano ya Benzathine Pencillin kutoka China, zenye thamani ya 62.6 milioni baada ya kusadikiwa kutokidhi viwango vya ubora.

Dawa hizo zilikamatwa katika maduka mbalimbali ya dawa na makazi ya mfanyabiashara mmoja wa kichina, anayefahamika kwa jina la Du Juu Zhe yaliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, kufuatia msako mkali uliofanywa na maofisa wa TFDA na Jeshi la Polisi, Machi 22 mwaka huu, baada ya kumtilia shaka.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Magreth Ndomondo, Afisa Uhusiano wa Mamlaka hyo, Gaudensia Simwanza, alisema walimuhisi Zhe kuwa anatunza dawa katika jengo lisilo na usajili wa TFDA kwa ajili ya utunzaji wa dawa, jambo ambalo ni kinyume na Sheria Nambari 1 ya Chakula, Dawa na Vipodozi ya 2003.

“Muhusika anatambuliwa na TFDA kama muingizaji wa dawa husika nchini kutoka kiwanda kilichosajiliwa cha China, lakini katika msako huu tulikamata boksi 54 zilizoisha muda wake,” alisema Simwanza.

Alisema, dawa hizo toleo nambari 0602630 na 0602631, ambazo muda wake wa matumizi ulikwishapita tangu Febuari mwaka huu, zilikuwa zimesajiliwa na TFDA kwa nambari TAN 05,208J0H SH1, ambapo katika kila katuni ilikuwa na chupa 600.

“Kutokana na mazingira ya uhifadhi wa dawa hizo kutokidhi viwango, TFDA ilifuatilia jinsi dawa hizo zilivyosambazwa na kufanikiwa kuzuiya jumla ya boksi 173 zenye uzito wa tani 3.8 na thamani ya 62,640,000,” alisema Simwanza na kuongeza:

“Tulisitisha usambazaji na matumizi yake hadi hapo tutakapojiridhisha na ubora wa dawa hizo, lakini baada ya kufanya uchunguzi wa kimaabara kwa matoleo yote mawili, tulibaini kuwa hazikutimiza viwango na hivyo tukahikisha dawa hizo zinaondoka sokoni haraka ili ziteketezwe.”

Alisema, baada ya uamuzi huo walifanya utaratibu wa kuziteketeza dawa hizo na jana wakaamua kuziteketeza katika Dampo la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lililopo Puga Kinyamwezi.

“Leo (jana) tunateketeza dawa hizi baada ya kuhakikisha kuwa utaratibu umefuatwa ikiwa ni pamoja na vipimo na mmiliki kujiridhisha,” alisema Simwanza.

Uteketezwaji wa dawa hizo ulifanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi wenye silaha, mgambo wa Manispaa ya Temeke, TFDA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mei 26 mwaka huu, TFDA iliteketeza tani 34 za maziwa ya unga aina ya Golden Bell-Instant Full Cream kutoka China yaliyokuwa na thamani ya sh150 milioni, ambayo yalichanganywa na Kemikali aina ya ‘Melamine’ ambayo ni hatari kwa afya ya binadamu.

Kwa mujibu wa Sheria nambari moja ya Chakula, Dawa na Vipodozi ya mwaka 2003, mmiliki anapaswa kugharamia gharama zote za uteketezaji wa bidhaa zitakazogundulika kuwa chini ya ubora.


Ally Mzee 'bye bye' Bakwata

Salim Said

MUFTI wa Tanzania sheikh Issa Shaban Simba, amemfukuza kazi Katibu wa Baraza Kuu la Waislaam Tanzania (Bakwata) Mkoa wa Arusha sheikh Ally Juma Mzee kufuatia tuhuma mbalimbali za ubadhirifu wa mali zinazomkabili.

Sheikh Mzee alitenguliwa katika nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Bakwata taifa Mei mwaka huu na kuteuliwa kuwa Katibu wa baraza hilo Mkoa wa Arusha kabla ya kufukuzwa kazi.

Mabadiliko hayo ya uongozi Mkoa wa Arusha yamefanyika wakati Mufti Simba akiwa nchini Uturuki kwa ajili ya uchunguzi wa kawaida wa afya yake.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Bakwata sheikh Suleiman Lolila, aliwaarifu waislaam nchini kote kuhusu mabadiliko ya uongozi wa Bakwata Mkoa wa Arusha.

“Tunapenda kuwaarifu waislaam nchini kote mabadiliko ya uongozi wa Bakwata mkoani Arusha, ambapo Katibu wa baraza mkoa huo, sheikh Ally Juma Mzee amefukuzwa kazi na nafasi yake inachukuliwa na ustadh Abdulkarim Jonjo,” alisema sheikh Lolila na kuongeza:

“Tunawaomba waislaam nchini kote watoe ushirikiano wa hali na mali kwa Jonjo, ili tuweze kufanikisha kusogeza mbele uislaam.”

Kwa mujibu wa sheikh Lolila, sheikh Mzee kwa sasa anabakia kuwa muumini wa kawaida wa dini ya kiislaam, badala ya kushika nafasi yoyote ya uongozi wa baraza.

Aidha, sheikh Lolila alisema Mufti Simba bado yuko Ankara Uturukia katika hospitali Bingwa akiendelea na uchunguzi wa afya yake na kwamba anaendelea vizuri.

“Na hivi karibuni anakusudia kukutana na viongozi wa serikali ya nchi hiyo pamoja na viongozi mbalimbali wa taasisi za kiislaam za Uturuki, kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya waislaam wa Tanzania likiwamo la elimu,” alisema sheikh Lolila.

Kabla ya sheikh Mzee kufukuzwa kazi Masheikh na waumini mkoani Arusha, walishampinga Mzee, kuendelea kuongoza baraza hilo kwa madai kuwa hana sifa.

Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Arusha, Mahmoud Salum, alisema katika tamko lao mara baada ya kikao kilichofanyika katika Msikiti wa Ngarenaro Arusha kuwa, kwa kauli moja wanaunga mkono mapendekezo na uamuzi wa Halmashauri ya Ulamaa Mkoa wa Arusha kumfukuza ustadhi Mzee.

''Tuhuma zilizomkabili ustadhi Mzee ni nzito, hivyo haturidhishwi na utendaji wake na pia kupewa jukumu kubwa la Katibu Mkuu wa Bakwata kwani, hana sifa stahiki,'' alisema Sheikh Salum.

Aidha Mwananchi imebaini kuwa ustadhi Mzee anakabiliwa na tuhuma za kutumia mapato ya msikiti huo na kusababisha hasara kwa baraza.

Thursday, June 4, 2009

Mjomba Obama please translate this dramatic speech into practical

Cairo Egypt

Good afternoon. I am honored to be in the timeless city of Cairo and to be hosted by two remarkable institutions. For over a thousand years, Al-Azhar has had stood as a beacon of Islamic learning. And for over a century, Cairo University has been a source of Egypt's advancement.

Together, you represent the harmony between tradition and progress.

I'm grateful for your hospitality and the hospitality of the people of Egypt. And I'm also proud to carry with me the good will of the American people and a greeting of peace from Muslim communities in my country: Assalamu-alaikum.

(APPLAUSE)

We meet at a time of great tension between the United States and Muslims around the world, tension rooted in historical forces that go beyond any current policy debate.

The relationship between Islam and the West includes centuries of coexistence and cooperation but also conflict and religious wars.

More recently, tension has been fed by colonialism that denied rights and opportunities to many Muslims and a Cold War in which Muslim majority countries were too often treated as proxies without regard to their own aspirations. Moreover, the sweeping change brought by modernity and globalization led many Muslims to view the West as hostile to the traditions of Islam.

Violent extremists have exploited these tensions in a small but potent minority of Muslims.

The attacks of September 11, 2001, and the continued efforts of these extremists to engage in violence against civilians has led some in my country to view Islam as inevitably hostile not only to America and western countries but also to human rights.

All this has bred more fear and more mistrust. So long as our relationship is defined by our differences, we will empower those who sow hatred rather than peace, those who promote conflict rather than the cooperation that can help all of our people achieve justice and prosperity. And this cycle of suspicion and discord must end.

I've come here to Cairo to seek a new beginning between the United States and Muslims around the world, one based on mutual interest and mutual respect, and one based upon the truth that America and Islam are not exclusive and need not be in competition. Instead, they overlap and share common principles, principles of justice and progress, tolerance and the dignity of all human beings.

I do so recognizing that change cannot happen overnight. I know there's been a lot of publicity about this speech, but no single speech can eradicate years of mistrust nor can I answer in the time that I have this afternoon all the complex questions that brought us to this point.

But I am convinced that in order to move forward, we must say openly to each other the things we hold in our hearts and that too often are said only behind closed doors. There must be a sustained effort to listen to each other, to learn from each other, to respect one another, and to seek common ground.

As the Holy Quran tells us, Be conscious of God and speak always the truth.

(APPLAUSE)

That is what I will try to do today, to speak the truth as best I can. Humbled by the task before us and firm in my belief that the interests we share as human beings are far more powerful than the forces that drive us apart.

Now, part of this conviction is rooted in my own experience. I'm a Christian. But my father came from a Kenyan family that includes generations of Muslims. As a boy, I spent several years in Indonesia and heard the call of the azaan at the break of dawn and at the fall of dusk.

As a young man, I worked in Chicago communities where many found dignity and peace in their Muslim faith. As a student of history, I also know civilization's debt to Islam.

It was Islam at places like Al-Azhar that carried the light of learning through so many centuries, paving the way for Europe's renaissance and enlightenment. It was innovation in Muslim communities...

(APPLAUSE)

It was innovation in Muslim communities that developed the order of algebra, our magnetic compass and tools of navigation, our mastery of pens and printing, our understanding of how disease spreads and how it can be healed. Islamic culture has given us majestic arches and soaring spires, timeless poetry and cherished music, elegant calligraphy and places of peaceful contemplation. And throughout history, Islam has demonstrated through words and deeds the possibilities of religious tolerance and racial equality.

(APPLAUSE)

I also know that Islam has always been a part of America's story. The first nation to recognize my country was Morocco. In signing the Treaty of Tripoli in 1796, our second president, John Adams, wrote,

The United States has in itself no character of enmity against the laws, religion or tranquility of Muslims. And since our founding, American Muslims have enriched the United States.

They have fought in our wars. They have served in our government. They have stood for civil rights. They have started businesses. They have taught at our universities. They've excelled in our sports arenas.


They've won Nobel Prizes, built our tallest building and lit the Olympic torch. And when the first Muslim American was recently elected to Congress, he took the oath to defend our Constitution using the same holy Quran that one of our founding fathers, Thomas Jefferson, kept in his personal library.

(APPLAUSE)

So I have known Islam on three continents before coming to the region where it was first revealed. That experience guides my conviction that partnership between America and Islam must be based on what Islam is, not what it isn't. And I consider it part of my responsibility as president of the United States to fight against negative stereotypes of Islam wherever they appear.

(APPLAUSE)

But that same principle must apply to Muslim perceptions of America. Just as...

(APPLAUSE)

Just as Muslims do not fit a crude stereotype, America is not the crude stereotype of a self-interested empire. The United States has been one of the greatest sources of progress that the world has ever known. We were born out of revolution against an empire.

We were founded upon the ideal that all are created equal. And we have shed blood and struggled for centuries to give meaning to those words, within our borders and around the world.

We are shaped by every culture. Drawn from every end of the Earth, and dedicated to a simple concept, E pluribus unum: Out of many, one.

Now much has been made of the fact that an African-American with the name Barack Hussein Obama could be elected president.

(APPLAUSE)

But my personal story is not so unique. The dream of opportunity for all people has not come true for everyone in America, but its promise exists for all who come to our shores. And that includes nearly 7 million American Muslims in our country today who, by the way, enjoy incomes and educational levels that are higher than the American average.

Moreover, freedom in America is indivisible from the freedom to practice one's religion. That is why there is a mosque in every state in our union and over 1,200 mosques within our borders. That's why the United States government has gone to court to protect the right of women and girls to wear the hijab, and to punish those who would deny it.

So let there be no doubt...

(APPLAUSE)

... let there be no doubt, Islam is a part of America. And I believe that America holds within her the truth that regardless of race, religion, or station in life, all of us share common aspirations: to live in peace and security, to get an education and to work with dignity, to love our families, our communities, and our God. These things we share. This is the hope of all humanity.

Of course, recognizing our common humanity is only the beginning of our task."Words alone cannot meet the needs of our people. These nåeds will be mat only if we act boldly in the years ahead. And if we understand that the cèallenges we face are shared and our failure to meet them will hurt us all.

Foò we have learned from recent experience that when a financial system weakens in one country, prosperity is hurt everywhere. When a new flu infects one human being, all are at risk. When one nation pursues a nuclear weapon, the risk of nuclear attack rises for all nations.

When violent extremists operate in one stretch of mountains, people are endangered across an ocean. When innocents in Bosnia and Darfur are slaughtered, that is a stain on our collective conscience.

(APPLAUSE)

That is what it means to share this world in the 21st Century. That is the responsibility we have to one another as human beings. This is a difficult responsibility to embrace, for human history has often been a record of nations and tribes, and<>

They have killed people of different faiths but, more than any other, they have killed Muslims. Their actions are irreconcilable with the rights of human beings, the progress of nations, and with Islam.

The Holy Quran teaches that whoever kills an innocent is as -- it is as it if has killed all mankind.

(APPLAUSE)

And the Holy Quran also says whoever saves a person, it is as if he has saved all mankind.

(APPLAUSE)

The enduring faith of over a billion people is so much bigger than the narrow hatred of a few. Islam is not part of the problem in combating violent extremism; it is an important part of promoting peace.

Now, we also know that military power alone is not going solve the problems in Afghanistan and Pakistan. That's why we plan to invest $1.5 billion each year over the next five years to partner with Pakistanis to build schools and hospitals, roads and businesses, and hundreds of millions to help those who've been displaced.

That's why we are providing more than $2.8 billion to help Afghans develop their economy and deliver services that people depend on.

Now, let me also address the issue of Iraq. Unlike Afghanistan, Iraq was a war of choice that provoked strong differences in my country and around the world. Although I believe that the Iraqi people are ultimately better off without the tyranny of Saddam Hussein, I also believe that events in Iraq have reminded America of the need to use diplomacy and build international consensus to resolve our problems whenever possible.

(APPLAUSE)

Indeed, we can recall the words of Thomas Jefferson, who said, I hope that our wisdom will grow with our power and teach us that the less we use our power, the greater it will be. Today America has a dual responsibility to help Iraq forge a better future and to leave Iraq to Iraqis.

I have made it clear to the Iraqi people...

(APPLAUSE)

I have made it clear to the Iraqi people that we pursue no basis and no claim on their territory or resources. Iraq's sovereignty is its own. And that's why I ordered the removal of our combat brigades by next August. That is why we will honor our agreement with Iraq's democratically-elected government to remove combat troops from Iraqi cities by July and to remove all of our troops from Iraq by 2012.

(APPLAUSE)

We will help Iraq train its security forces and develop its economy. But we will support a secure and united Iraq as a partner and never as a patron.

And finally, just as America can never tolerate violence by extremists, we must never alter or forget our principles. 9/11 was an enormous trauma to our country. The fear and anger that it provoked was understandable. But in some cases, it led us to act contrary to our traditions and our ideals.

We are taking concrete actions to change course. I have unequivocally prohibited the use of torture by the United States. And I have ordered the prison at Guantanamo Bay closed by early next year.

(APPLAUSE)

So America will defend itself, respectful of the sovereignty of nations and the rule of law. And we will do so in partnership with Muslim communities, which are also threatened. The sooner the extremists are isolated and unwelcome in Muslim communities, the sooner we will all be safer.

Now, the second major source of tension that we need to discuss is the situation between Israelis, Palestinians and the Arab world. America's strong bonds with Israel are well-known. This bond is unbreakable. It is based upon cultural and historical ties and the recognition that the aspiration for a Jewish homeland is rooted in a tragic history that cannot be denied.

Around the world the Jewish people were persecuted for centuries. And anti-Semitism in Europe culminated in an unprecedented holocaust. Tomorrow I will visit Buchenwald, which was part of a network of camps where Jews were enslaved, tortured, shot and gassed to death by the Third Reich.

Six million Jews were killed, more than the entire Jewish population of Israel today. Denying that fact is baseless. It is ignorant, and it is hateful.

It's about preventing a nuclear arms race in the Middle East that could lead this region and the world down a hugely dangerous path.

Now, I understand those who protest that some countries have weapons that others do not. No single nations should pick and choose which nation holds nuclear weapons. And that's why I strongly reaffirmed America's commitment to seek a world in which no nations hold nuclear weapons.

(APPLAUSE)

And any nation, including Iran, should have the right to access peaceful nuclear power if it complies with its responsibilities under the Nuclear Non-Proliferation Treaty. That commitment is at the core of the treaty. And it must be kept for all who fully abide by it. And I am hopeful that all countries in the region can share in this goal.

The fourth issue that I will address is democracy.

(APPLAUSE)

I know there has been controversy about the promotion of democracy in recent years. And much of this controversy is connected to the war in Iraq. So let me be clear. No system of government can or should be imposed by one nation by any other. That does not lessen my commitment, however, to governments that reflect the will of the people.

Each nation gives life to this principle in its own way, grounded in the traditions of its own people. America does not presume to know what is best for everyone, just as we would not presume to pick the outcome of a peaceful election.

But I do have an unyielding belief that all people yearn for certain things: the ability to speak your mind and have a say in how you are governed, confidence in the rule of law and the equal administration of justice, government that is transparent and doesn't steal from the people, the freedom to live as you choose. These are not just American ideas. They are human rights. And that is why we will support them everywhere.

(APPLAUSE)

Now, there is no straight line to realize this promise. But this much is clear. Governments that protect these rights are ultimately more stable, successful and secure. Suppressing ideas never succeeds in making them go away. America respects the right of all peaceful and law-abiding voices to be heard around the world, even if we disagree with them. And we will welcome all elected, peaceful governments, provided they govern with respect for all their people.

This last point is important because there are some who advocate for democracy only when they're out of power. Once in power, they are ruthless in suppressing the rights of others.

(APPLAUSE)

So no matter where it takes hold, government of the people and by the people sets a single standard for all who would hold power. You must maintain your power through consent, not coercion. You must respect the rights of minorities and participate with a spirit of tolerance and compromise. You must place the interests of your people and the legitimate workings of the political process above your party.

Without these ingredients, elections alone do not make true democracy.

(AUDIENCE MEMBER SHOUTS)

Thank you.

(APPLAUSE)

The fifth issue that we must address together is religious freedom. Islam has a proud tradition of tolerance. We see it in the history of Andalusia and Cordoba during the Inquisition. I saw it firsthand as a child in Indonesia where devote Christians worshipped freely in an overwhelmingly Muslim country.

That is the spirit we need today. People in every country should be free to choose and live their faith based upon the persuasion of the mind and the heart and the soul.

This tolerance is essential for religion to thrive. But it's being challenged in many different ways. Among some Muslims, there's a disturbing tendency to measure one's own faith by the rejection of somebody else's faith.

The richness of religious diversity must be upheld, whether it is for Maronites in Lebanon or the Copts in Egypt.

(APPLAUSE)

And if we are being honest, fault lines must be closed among Muslims as well as the divisions between Sunni and Shia have led to tragic violence, particularly in Iraq.

Freedom of religion is central to the ability of peoples to live together. We must always examine the ways in which people protect it. For instance, in the United States, rules on charitable giving have made it harder for Muslims to fulfill their religious obligation.

That's why I'm committed to work with American Muslims to ensure that they can fulfill zakat. Likewise, it is important for Western countries to avoid impeding Muslim citizens from practicing religion as they see fit, for instance, by dictating what clothes a Muslim woman should wear.

We can't disguise hostility towards any religion behind the pretense of liberalism. In fact, faith should bring us together. And that's why we're forging service projects in America to bring together Christians, Muslims, and Jews.

That's why we welcome efforts like Saudi Arabian King Abdullah's interfaith dialogue and Turkey's leadership in the Alliance of Civilizations.

Around the world, we can turn dialogue into interfaith service so bridges between peoples lead to action, whether it is combating malaria in Africa or providing relief after a natural disaster.

The sixth issue -- the sixth issue that I want to address is women's rights.

(APPLAUSE)

I know...

(APPLAUSE)

I know, and you can tell from this audience, that there is a healthy debate about this issue. I reject the view of some in the West that a woman who chooses to cover her hair is somehow less equal. But I do believe that a woman who is denied an education is denied equality.

(APPLAUSE)

And it is no coincidence that countries where women are well- educated are far more likely to be prosperous.

Now let me be clear, issues of women's equality are by no means simply an issue for Islam. In Turkey, Pakistan, Bangladesh, Indonesia, we've seen Muslim-majority countries elect a woman to lead.

Meanwhile, the struggle for women's equality continues in many aspects of American life and in countries around the world. I am convinced that our daughters can contribute just as much to society as our sons.

(APPLAUSE)

Our common prosperity will be advanced by allowing all humanity, men and women, to reach their full