MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Sunday, February 28, 2010

UANDIKISHAJI PEMBA: MPAKA KIELEWEKE


Jamani na sisi ni binadamu wenzenu!


Eeeh! weee! Mungu tusaidie waja wako

Dah! mnatuonea wenzenu


Tupigeni tu hizo risasi




Hizo ni baadhi ya picha zilizopigwa wakati wa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapigakura kisiwani Pemba katika wilaya ya Wete mkoa wa kaskazini Pemba jimbo la Ole. picha zote na Salim Said.

Thursday, February 25, 2010

DUH! HAKUNA SIMBA HUMU

Baadhi ya waandishi wa habari wakiingia katika Pori la Mungu eneo la Usariva mkoani Arusha kukagua chanzo cha maji kinachotumika kugaw maji safi ya kunywa na ya kumwagilia katika mashamba. Picha na Salim Said

Wednesday, February 24, 2010

ZEC yaanzisha zoezi maalum kutambua waliokuwa hawajaandikishwa

Salim Said
TUME ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) imeanzisha kazi maalum ya kuorodhesha na kutambua idadi kamili ya wazanzibari waliokosa kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa sababu ya Kitambulisho cha Mzanzibari Mkazi (Zan ID) ili kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo.

Kazi hiyo inafanyika kwa siku sita tu katika mikoa na wilaya zote za Unguja na Pemba kabla ya kuanza kwa awamu ya pili nay a mwisho ya uboreshaji wa daftari hilo, inayotarajiwa kuanza Machi 1 mwaka huu.

Akizungumza na Mwananchi jana, Mkurugenzi wa Zec Salim Kassim alisema kazi hiyo imeanza tangu Febuari 22 mwaka huu na itakamilika Febuari 28.

“Tumeamua kufanya hivi kwa sababu kumekua na malalamiko mengi kutoka kwa vyama vya siasa kwamba watu wao wengi hawajaandikishwa, tukiwauliza wangapi wanasema wengi lakini hawana idadi kamili,” alisema Kassim na kuongeza:

“Kwa hiyo kazi hii ya siku sita itatupatia orodha ya idadi kamili ya watu waliokuwa hawajaandikishwa, ili tuone kwamba ni kwa namna gani wanaweza kupata haki yao kama wana sifa, kwa sababu hawa ni wapigakura wetu.”

Alisema baada ya kukamilika kwa kazi hiyo hapo Febuari 28 hatua ya kwanza watakayochukua ni kutangaza idadi kamili ya watu hao, na baadae hatua nyengine zitafuata za kiutendaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano na Umma wa CUF Salim Bimani aliwataka wananchi wote wa Zanzibar, ambao mwaka 2005 walipiga kura katika uchaguzi mkuu na wanazo shahada zao za kupigia kura, lakini hawana Zan ID, wafike kwenye vituo vya Tume ZEC kwa wingi.

Alivitaja vituo kuwa kwa Unguja ni pamoja na Kariakoo wilaya ya Mjini, Kwerekwe ‘A’ wilaya ya Magharibi, Koani Banda la Karafuu wilaya ya Kati, Ofisi ya Wilaya Dembra wilaya ya Kusini, Gamba Banda la Karafuu wilaya ya Kaskazini ‘A’ na Mahonda Banda la Karafuu wilaya ya Kaskazini ‘B.

Kwa upande wa Kanda ya Pemba aliwataka wafike Skuli ya Micheweni wilaya ya Micheweni, Kilimo Weni wilaya ya Wete, Mtambile Banda la Karafuu wilaya ya Mkoani na kwa wilaya ya Chake Chake Wafike Skuli ya Michakaini.

Bimani aliwahimiza wananchi wote wenye sifa hizo wajitokeze kwa wingi kwenye vituo hivyo, wakizingatia kwamba kuandikishwa ndiko kutakowawezesha kupiga kura na hivyo kuwa na nguvu ya kufanya mabadiliko katika nchi yao.

“Baada ya kutambuliwa wote waliokuwa hawajaandikishwa Zec itabidi isimami kazi ya kupata Zan ID ili na wao waandikishwe katika daftari na waweze kutumia haki yao ya msingi ya kupigakura ya maoni na katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu,” alisema Bimani.

Tuesday, February 23, 2010

MAHAFALI: TUMEKOMBOKA WANAWAKE

Baadhi ya wanawake kutoka vikundi mbalimbali vya kina-mama Kata ya Mabibo jijini Dar es Salaam wakisheherekea kumaliza mafunzo ya wiki mbili ya ujasiriamali yaliyofadhiliwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM katika Kata hiyo, Mlowe Boni na Mlezi wa Jumuiya hiyo Hawa Ng'umbi.

SHIKAMOO MWALUMU

Tupo darasano tunasoma lakini vumbi linatusumbua. Hawa ni watoto wa moja ya shule za msingi katika wilaya ya Newala Mjini mkoa wa Mtwara.


HONGERA: Mkuu wa wilaya ya Newala Dk Rehema Nchinimbi, akitoa cheti kwa muhitimu wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Kitangari wilaya ya Newala mkoani Mtwara.

HATUSAFIRI: TUNAENDA KUFUA. Baadhi wa wanafunzi wa shule za msingi katika Wilaya ya Newala mkoani Mtwara wakiwa na mabegi yenye nguo chafu kwa ajili ya kwenda katika bonde la mto ruvuma kufua, takriban umbali wa Kilomita 7 kutoka wanakoishi.


TUPO KAZINI: Baadhi ya wapigapicha wakujitegemea wakihangaika kupata picha katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Kitangari wilaya ya Newala mkoani Mtwara


MGUU SAWA!: Baadhi ya wanafunzi wakiwa katika paredi ya mchana katika moja ya shule za msingi za wilaya ya Newala mkoni Mtwara, ikiwa ni siku ya Jumanne. Hali ya usafi kwa wanafunzi hao ni mtihani kutokana na uhaba mkubwa wa maji unaoikabili wilaya hiyo

Monday, February 22, 2010

HUKU NI KUDHALILISHANA WANADAMU


Mfano wa kivuli cha mtu katika skana zilizowekwa katika viwanja mbalimbali vya ndege katika nchi za Ulaya na Marekani ikiwa ni katika juhudi za nchi hizo kupambana na majaribio ya Ugaidi. Skana hizo zimepingwa na wasomi wa kiislaam kwa kuwa zinawadhalilisha na ni kinyume na haki za binaadamu.
Marekani Muslim Scholars Against Body Scanners
Saying that body scanners violate Islamic law, Muslim-American groups are supporting a "fatwa” a religious ruling that forbids Muslims from going through the scanners at airports.
The Fiqh Council of North America a body of Islamic scholars issued a fatwa this week that says going through the airport scanners would violate Islamic rules on modesty.

"It is a violation of clear Islamic teachings that men or women be seen naked by other men and women," reads the fatwa issued Tuesday. "Islam highly emphasizes haya (modesty) and considers it part of faith. The Qur'an has commanded the believers, both men and women, to cover their private parts."

The decision could complicate efforts to intensify screening of potential terrorists who are Muslim. After the Christmas Day bombing attempt in Detroit by a Muslim suspect from Nigeria, some have called for the use of body scanners at airports to find explosives and other dangerous materials carried by terrorists. Some airports are now in the process of buying and using the body scanners, which show in graphic detail the outlines of a person's body.

In the U.S., there are now forty scanners in nineteen airports and could be as many as 450 by the end of the year.

But certain Muslim groups say the scanners go against their religion. One option offered to passengers who don't want to use the scanners would be a pat down by a security guard. All passengers, regardless of faith, may opt for the optional same sex pat down. The Muslim groups are urging members to undergo those instead.

The American policy is far more lenient than the one instituted by airports in Britain, where travelers who refuse to pass through the scanners can be barred from boarding. The Council on American-Islamic Relations says it endorses the fatwa.

"We support the Fiqh Council's statement on full-body scanners and believe that the religious and privacy rights of passengers can be respected while maintaining safety and security," said Nihad Awad, national executive director of CAIR.

The Transportation Security Administration (TSA) argues that it is committed to keeping passengers safe and insisted the scanners do not represent an invasion of privacy.

"The TSA's mission is to keep the travelling public safe. Advanced imaging technologies are an important tool in a multi- layered security system to detect evolving threats such as improvised explosive devices," said a spokesman.

"Use of these technologies includes strong protections in place to safeguard passenger privacy. Screening images are automatically deleted, and the officer viewing the image will never see the passenger."

The TSA stressed that the body scanners are "optional to all passengers". Those who turn them down in the US "will receive equivalent screening that may include a physical pat-down, hand-wanding, and other technologies."

"Physical pat-downs are performed by Transportation Security Officers of the same sex as the passenger in a private screening area, if the passenger requests."

"Body scanners do not produce photos", the agency added. Rather, the images "look like chalk outlines".

Sunday, February 21, 2010

PYUZA: WATANZANIA WENGI WANAKULA UBWABWA KWA PUA'

WALI
Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Kilimanjaro (KATC) wilayani Moshi Adam Pyuza akitoa maelezo kwa waandishi wa habari hivi karibuni. picha na Salim Said.

Salim Said
MOJA ya kilio kikubwa cha wakulima wa Tanzania ni kukosekana kwa soko la uhakika la ajili ya kuuza mazao yao baada ya suluba ya kipindi chote cha kilimo.

Ili kukabiliana na tatizo au kilio hicho, serikali ilianzisha mfumo wa stakabadhi ghalani kama njia ya kuwakwamua wakulima wa mazao ya biashara lakini, licha ya nia hiyo nzuri, mfumo huo umekuwa ukipata upinzani mkubwa kutoka kwa wakulima katika baadhi ya maeneo.

Mfumo huo umeingia kwa kasi katika mikoa na wilaya zote za kanda ya kusini ya Tanzania, wakulima hutakiwa kuweka mazao yao ghalani na kupatiwa mkopo wa fedha za kujikimu, hadi hapo mazao yao yatakapouzwa na kulipwa.

Lakini kwa kanda nyingine za Tanzania, mfumo huo haujafika, wakulima wengi wanahangaika kupata soko la mazao yao, jambo ambalo husababisha kuchelewa kuanza na kumaliza kwa msimu mpya wa kilimo au kupata ugumu wa maisha kwa kukosa fedha za kujikimu.

Mathalan, katika Mkoa wa Kilimanjaro, kuna wakulima wanaozalisha kwa wingi mpunga, mahindi, alizeti na hata maharagwe kwa ajili ya chakula na biashara.

Lakini kama ilivyo katika kanda nyingine za kilimo, wakulima wa hao nao wanakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa soko la uhakika la kuuzia mazao yao hasa mpunga.

Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Kilimanjaro (KATC), Adam Pyuza anasema kuna sababu nyingi za wakulima wa mkoa huo hasa Wilaya ya Moshi kukosa soko la uhakika la mazao yao hususan mpunga ambao unazalishwa kwa wingi katika Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika ukanda wa Moshi Chini.

Anasema sababu kubwa ya kukosa soko la uhakika wa mpunga wao ni asilimia kubwa ya Watanzania kula ubwabwa (wali), kwa kutumia pua badala ya mdomo na ulimi, kwa maana wanapenda ubwabwa unaonukia.

“Asilimia kubwa ya Watanzania wanakula ubwabwa kwa pua badala ya mdomo. Ikiwa mchele wako haunukii, basi ujue kwa walaji wa Tanzania haununuliki, kwani soko kuu la mpunga linalotegemewa na wakulima nchini kote ni jiji la Dar es Salaam,” anasema Pyuza na kuongeza:

“Sifa kuu ya mchele unaolimwa katika Mkoa wa Kilimanjaro ni kwamba haunukii na hiyo ni sababu kuu ya mpunga wa wakulima wa Moshi kukosa soko, hivyo kuishia kukaa ghalani hadi hapo mpunga unapoadimika na wao ndipo hupata fursa ya kuuza.”

Anasema kutokana na sababu hiyo, wafanyabiashara wengi wakati wa mavuno hukimbilia sehemu za Mbeya, Kyela na Morogoro kuchukua mpunga na kupeleka sokoni Dar es Salaam, kwa sababu mipunga ya huko inanukia sana.
Anasema baada ya wafanyabiashara kuhakikisha kuwa wamemaliza mpunga katika maeneo hayo ndipo huamua kwenda Moshi na ambako hulazimisha kuuziwa mpunga kwa bei ya chini kabisa.

Anasema kuwa licha ya kuwa mpunga wa Moshi haunukii lakini una sifa ya kubwa ya kuvimba unapopikwa na hivyo kuufanya uwe na baraka kwa watumiaji.

Anasema kutokana na hali hiyo mchele wa Moshi hutumiwa zaidi katika hoteli, migahawa, shule za bweni na vyuo na hata kwa mama lishe kwa sababu unavimba.

“Wajanja wote wa mahoteli ya Moshi na wilaya jirani utawakuta wanautumia sana mpunga wa Moshi Chini kwa sababu wanachotaka wao ni kutengeneza faida na siyo harufu nzuri ya ubwabwa kwa kumridhisha mteja,” anasema Pyuza.
Anafafanua kuwa licha ya kupendwa na wenyeji, kutokana na ladha yake nzuri mchele wa Moshi umekuwa ukipendwa na majirani wa Tanzania hasa Kenya... “Utakuta mchele wa Moshi unauzwa sana Kenya kuliko hata Tanzania, kwa sababu Wakenya wanajua uchumi na hawaangalii sana harufu ya mchele bali cha msingi kwao ni kama una ladha nzuri na unavimba kulisha familia kubwa?”

Anasema ikiwa wakulima wa Moshi watategemea soko la ndani, basi lazima wasubiri hadi ule wa mikoa ya Mbeya na Morogoro utakapomalizika... “Kwa maana hiyo mchele wa Moshi misimu yote huuzwa mwisho kabisa.”
Anasema sifa nyingine ya mchele wa Moshi ni kutokuwa na mawe kwa kuwa unaandaliwa kwa kutumia vifaa vya kisasa vinavyotengenezwa na wahandisi wa KATC. Pyuza anasema bei ya gunia (aina ya lumbesa) moja ya mpunga wa Moshi huuzwa kwa Sh70,000 hadi Sh80,000.

Anasema mfumo wa stakabadhi ghalani haujafika Moshi kwa sababu chama cha ushirika hakijaimarika ipasavyo, kwa sababu mfumo huo huwa unasimamiwa na chama cha ushirika wa eneo husika.

Taarifa zinaonyesha kwamba Moshi kupitia mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji unaofadhiliwa na serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Jica inazalisha mchele kwa wingi tangu mwaka 1994. Katika mradi huo hekta 1,100 zinatumika kuzalishia mpunga na kila hekta ina uwezo wa kuzalisha tani 6.5 hadi nane.

Pyuza anasema chuo chake kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kupitia Shirika la Jica, kipo katika mchakato wa kusambaza mbegu mpya ya mpunga kwa Bara la Afrika (Nerica series), ambazo zimeshafanyiwa utafiti na majaribio na kujiridhisha kuwa ni bora na mchele wake unanukia vizuri na unafaa kwa soko la Tanzania.
Wakulima wanalalamika kwamba kukosekana kwa soko kumekuwa na athari kubwa kwao kwani wakati mwingine hukosa fedha za fedha kukodisha mashamba, kulimia, kulipia maji ya mradi na hata kununulia pembejeo.
“Kwa kweli kukosekana kwa soko la uhakika kunatupa changamoto kubwa sisi wakulima, kwa sababu baadhi ya wakati hata misimu inachelewa kuanza kwa sababu ya kukosa fedha za kuendeleza kilimo, kutokana na mazao yetu kukaa ndani tu,” anasema mkulima kiongozi, Hanfred Msuya.

“Kuna mchezo mchafu ambao tunafanyiwa na wachuuzi wa mpunga. Sisi huwa tunapima debe sita kwa kilo 80 katika gunia, lakini wao hulazimisha kujaza viroba viwili vya kilo gramu 50 ambavyo huwa wanakuja navyo, ukijaza utakuta gunia lina kilo 95 au 100.”

Lower Moshi: Tulianza Kilimo Kwanza tangu 1994

Salim Said
MWAKA jana, Rais Jakaya Kikwete alizindua kampeni ya kitaifa ya kuboresha kilimo nchini, iliyobatizwa jina la Kilimo Kwanza ikiwa na lengo la kuweka fungu kubwa la fedha kuhudumia sekta hiyo.

Fungu hilo ni kwa ajili ya kuwaandaa wataalamu wa kilimo na kununulia pembejeo ambazo ni matrekta, mbolea, dawa na zana nyingine za kilimo kwa kutumia teknolojia nyepesi na za bei nafuu.

Lakini wakulima wa kilimo cha umwagiliaji Moshi Chini (Lower Moshi) mkoani Kilimanjaro wanasema Kilimo Kwanza si jambo geni kwao kwani walishaanza kukitekeleza tangu mwaka 1994.

Kabla ya kuanza kilimo hicho, wakulima hao wa mpunga walipatiwa mafunzo katika Kituo cha Mafunzo ya Kilimo Kilimanjaro (KATC), ambacho awali kiliitwa Chuo cha Maendeleo ya Kilimo Kilimanjaro (KADC).

Mkuu wa chuo hicho, Adam Pyuza anasema: “Sisi watu wa Lower Moshi tumeanza kilimo kwanza kwa miaka mingi sasa. Tangu mwaka 1994! Serikali imechelewa sana kuliona hilo.”

Pyuza anasema wakulima wa ukanda wa Lower Moshi wameanza kilimo kwanza baada ya wote kupatiwa elimu ya kilimo cha umwagiliaji kwa nadharia na vitendo kuanzia mwaka huo.

“Elimu hii ya kilimo cha umwagiliaji inatolewa kupitia Ushirikiano wa Kitaalamu katika Kusaidia Mfumo wa Utoaji Huduma katika Kilimo cha Umwagiliaji (TC-SDIA) au kwa lugha ya kawaida mpango huu tunauita ‘Tanrice’ ambao unafadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Misaada Japan (Jica).”

“Wakulima tuliowapatia mafunzo wameweza kuanzisha skimu bora za kilimo cha mpunga na kupata mafanikio makubwa kwa kulima kidogo na kuzalisha zaidi. Kabla ya mradi huu, watu wa ukanda wa Lower Moshi walikuwa hata kula yao kwa mwaka ni tabu.”

“Lakini kwa sasa wakulima wameweza kuimarisha mashamba yao na hata wakulima ambao awali walikuwa hawalimi mpunga wameacha kilimo chao cha ndizi na kuingia katika mpunga baada ya kuona wenzao wamepata mafanikio makubwa.”

“Hata wale wa vijiji vya jirani ambao hawakutaka kuingia katika mradi, sasa wote wamekuja na wanalima mpunga baada ya kuona wenzao wana uhakika wa chakula kwa mwaka mzima, wanasomesha watoto wao vizuri, wanauza ziada, wamejenga nyumba nzuri za kuishi na hata maisha yao yamebadilika.”

“Faida ya kwanza ni uhakika wa chakula, kukuza kipato cha wakulima kwa kuuza kwa sababu kama unavyojua mpunga ni chakula kikuu cha pili nchini, lakini pia mpunga unaweza kulimwa nchini kote katika maeneo ya mabonde na hata ya miinuko,” anasema Pyuza.

Anasema teknolojia ya uzalishaji mpunga ipo karibu nao katika chuo cha KATC pamoja na uhakika wa kupata mbegu bora kupitia utafiti wa Jica. Kadhalika, anasema utayari wa serikali ya sasa kusaidia miradi ya kilimo hicho ni mkubwa na kwamba hayo yote yatasaidia kuongeza uzalishaji wa mpunga.

Mratibu wa Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji Moshi Chini, Mhandisi Hatib Jengo anasema kilimo cha mpunga kwa njia ya kisasa kinatoa tija kubwa kwa mkulima.

Anasema mradi huo umetengewa hekta 2,300 za ardhi na kati ya hizo, hekta 1,200 ni kwa ajili ya kilimo cha mazao mchanganyiko na hekta 1,100 ni kwa ajili ya kilimo cha mpunga. Anasema kuna hekta nyingine zaidi ya 1,000 zinazohudumiwa na mradi ingawa mwanzo hazikuwamo.

“Mradi huu unategemea maji kutoka katika vyanzo vya Njoro na Rau, maji ambayo yanapitia katika mabanio (gates) mawili makuu ya Mabogini na Rau,” anasema Mhandisi Jengo.

Anasema kwa sasa wakulima wanatumia mbegu aina ya aero 54 na 65 ambazo sifa yake kubwa ni kwamba mchele wake haunukii lakini, unavimba hivyo kupendwa zaidi katika familia kubwa, shule za bweni, hoteli na hata vyuo.
Anasema mradi huo umeleta mapinduzi makubwa ya kilimo katika ukanda huo, ukiachilia mbali kuimarika na kuboreka kwa maisha ya wakulima hao lakini, hata baadhi ya watu waliokuwa hawalimi mpunga sasa wanalima baada ya kuona mafanikio ya wenzao.

“Kabla ya mradi huu, wakulima wa Lower Moshi walikuwa hawana uwezo hata wa kunua nyama lakini kwa sasa watumishi wakifika sehemu za kuuzia nyama wakulima wameshamaliza. Hata katika elimu, sasa tuna shule tano za sekondari ambazo, hazikuwapo kabla ya mradi huu,” anasema Mhandisi Jengo.

Anasema mavuno yamepanda kutoka tani mbili hadi tatu kwa hekta kabla ya mradi na kufikia tani sita na nusu hadi nane kwa hekta moja baada ya mradi.

Jengo anasema kuwa pamoja na mafanikio yote hayo, mradi wao unakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinahatarisha maisha yake. Kubwa ni uharibifu wa miundombinu unaosababishwa na kuibuka kwa biashara ya chuma chakavu. Baadhi ya wananchi wasio waaminifu wanaiba mabanio ya mifereji ya maji, bomba na vifaa vingine vya mifereji.

“Tabia hiyo imekuwa ikiugharimu mradi mamilioni ya shilingi. Hivi sasa wanahitaji fedha kutoka serikali kuu na halmashauri ili kukarabati miundombinu hiyo.”

Anasema ili kudhibiti uharibifu huo wameanzisha mpango wa ulinzi shirikishi kati yao, wakulima na Chama cha Wakulima wa Kilimo cha Umwagiliaji Moshi Chini (Lomia).

Changamoto nyingine ni kutofautiana kwa ratiba ya upandaji wa mpunga, jambo ambalo linasababisha matatizo katika ugawaji wa maji... “Kwa sasa kwa kushirikiana na Lomia na Chama cha Wakulima wa Mpunga Moshi (Chawampu) tunatoa elimu ili tuwe na ratiba moja ya upandaji wa mpunga na hata uvunaji kwa lengo la kurahisisha ugawaji wa maji.”

Anasema Lomia inajumuisha vijiji saba vya wakulima ambavyo baadhi vimo katika mradi na vingine havimo lakini vinalima kilimo cha mpunga kwa njia ya umwagiliaji na vinategemea maji hayo hayo ya mradi. Anavitaja vijiji hivyo kuwa ni Kaloleni, Madokamnoni, Mabogini, Rau, Njoro, Oria na Chekereni.

Pia kuna uhaba mkubwa wa maji. Baadhi ya misimu hulazimika kuacha baadhi ya hekta za ardhi kwa kuwa maji hayawezi kuhudumia hekta zote 2,300 za mradi na zile ambazo hazimo katika mradi kwa pamoja.

“Kutokana na hali hiyo baadhi ya wakati misimu huchelewa kuanza au kumalizika. Kwa kawaida sisi tuna misimu mitatu kwa mwaka, wa kwanza huanzia Januari hadi Mei, wa pili Mei hadi Septemba na wa mwisho Septemba hadi Januari,” anasema Jengo.

Katika jitihada za kutatua tatizo hilo, mwaka 1995 ulifanyika upembuzi yakinifu uliofadhiliwa na Jica ili mradi huo uchukue maji ya mita za ujazo tisa kwa sekunde wakati wa masika na kubiki mita tano kwa sekunde wakati wa kiangazi kutoka Mto Kikuletwa.

Lakini wizara husika wakati huo ilikataa na badala yake ikapendekeza kutoa mita za ujazo 3.5 za maji kwa sekunde.
“Kwa hiyo ikashindikana, kwa sababu gharama ya kuyachukua maji hayo ilikuwa ni kubwa ikilinganishwa na kiwango cha maji yenyewe,” anasema Jengo.

Anasema changamoto nyingine ni uhaba wa matrekta. Mradi huo ulipata matrekta 30 kutoka Jica mwaka 1985 ambayo yalitumika hadi 1995 na kuharibika na baadaye kupata mengine 16 mwaka 1996 ambayo yamepigwa mnada pamoja na vifaa vingine mwaka jana bada ya ziara ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

“Unajua Hazina ndiyo inapiga mnada kwa hiyo hata fedha za mnada huo huenda huko. Hatujui zimepatikana shilingi ngapi, lakini tumeiandikia barua Septemba mwaka jana kuomba fedha tununulie matrekta japo mawili.”

“Ingawa wakulima wetu wa Lower Moshi hawajawahi kutumia jembe la mkono katika mradi huu, lakini kwa sasa tunategemea matrekta manne na power-tellers nne za kukodi kutoka Chawampu.”

Jingo anasema hawajawahi kuvamiwa na magonjwa ya mazao hadi sasa katika ukanda huo, ingawa baadhi ya wakati hutokea wadudu waharibifu ikiwa ni pamoja na nzige, senene, kwelea kwelea na viwavijeshi vilivyotokea mwaka 1994.

HAYA KIMBIA: USAFIRI VIJIJINI

Kijana wa mashamba ya mpunga Leki Tatu, eneo la Usariver mkoani Arusha akiwa katika gari linalokokotwa na ng'ombe wanne likiwa na magunia ya mpunga kutoka katika mashamba ya kilimo cha umwagiliaji kwenda katika ghala hivi karibuni. Picha na Salim Said.

HIVI NDIVYO MBOLEA INAVYOMWAGWA



Mahamoud Pandu kutoka Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Kizimbani Zanzibar (KATC) akionyesha namna ya kumwaga mbolea aina ya Yurea katika mpunga kwenye mashamba ya Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Kilimanjaro (KATC), wilayani Moshi hivi karibuni. Picha na Salim Said.

KILIMO KWANZA:

Baadhi ya wakulima wa Mtwango znz wakiwa katika shamba darasa kwenye Chuo cha Mafunzo ya Kilimo Kilimanjaro (KATC) kilichopo Moshi mkoani Kilimanjaro katika mafunzo maalum ya wiki mbili. picha na salim said

Tuesday, February 9, 2010

CUF: ziara ya JK Dar ilikuwa kampeni

Salim Said

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimemshukia Mwenyekiti wa Chama Cha Mapnduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete kwamba, ziara yake jijini Dar es Salaam ililenga kujipigia kampeni na kwamba ni matumizi mabaya ya madaraka ya umma.

Rais Kikwete alifanya ziara ya siku tatu jijini hapa, ambapo wachambuzi wa mambo wameihusisha na kampeni zake za kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010 huku akitarajiwa kuwa mgombea wa urais kupitia CCM.

Mkurugenzi wa Siasa wa CUF Mbarallah Maharagande, alisema CUF inasikitishwa na matumizi mabaya ya madaraka yaliyofanywa na Rais katika ziara zake zilizofanyika wiki iliyopita.

Maharagande alisema mwenyekiti huyo wa CCM alitumia ziara hiyo ya kichama kutoa ahadi mbali mbali za kiserikali huku baadhi ya wakati akitoa kauli za kutishia kuwawajibisha watendaji wa Serikali, ili kujisafishia njia.

“Katika ziara hiyo, pamoja na kuongozana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam William Lukuvi, ambapo si sahihi kabisa katika ziara za kichama lakini, Kikwete alitumia ziara hiyo ya kichama kutoa ahadi mbalimbali za kiserikali, huku akitoa kauli za kutishia kuwawajibisha watendaji wa Serikali, ili kujisafishia njia,” alisema Maharagande.

Alisema CUF inalaani vikali ziara hiyo ambayo alidai ni matumizi mabaya ya madaraka, kwa kutumia nafasi ambazo ni za kuchaguliwa kwa kura za wananchi wenye itikadi tofauti na wasio na itikadi kwa maslahi ya CCM.

“CUF tunawaomba watanzania kuwa makini na viongozi wa Serikali ambao ni wasanii hususan katika kipindi hiki cha uchaguzi ambapo, hujitokeza kwa ahadi zisizotekelezeka ambazo, ni kiini macho kwa nia ya kuwalaghai watananzania,” alisema Maharagande.

Wakati huohuo Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano ya Umma wa CUF, Ashura Mustafa alisema kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari jana kwamba, chama chake hakikushangazwa na matokeo mabovu ya kidato cha nne katika shule za sekondari za Kata mkoani Dar es Salaam.

“Haya ni matokeo ya mipango na sera mbovu za CCM na serikali yake kwa kurejesha tena mfumo wa ualimu pasipo na elimu (UPE) katika ngazi ya Sekondari,” alisema katika taarifa yake.

Alisema pamoja na wadau wengi wa elimu nchini, kupigia kelele kuhusu madhara ya shule za sekondari za kata, lakini serikali ya CCM imekaidi na kudai kuwa ni mchakato bila ya kujua kuwa wanafunzi wa shule hizo hawasimami kusoma wanaenda sambamba na shule nyingine zenye ubora wa waalimu na vifaa vya kisasa.

“Pia wanaotunga mitihani hawajali kuwa shule za kata ziko katika mchakato na hazina maabara, maktaba na zina waalimu waliopata mafunzo ya wiki tatu na pia hawakufanya vizuri katika mitihani yao ya kumaliza kidato cha sita,” alisema Mustafa.

“CUF inaitaka serikali ya CCM kuacha kuwahadaa watanzania katika sekta ya elimu ili, kutimiza malengo yao ya kupigiwa kura katika chaguzi mbalimbali kwa kuwajengea shule za kata ambazo, hazina mwelekeo wa kutoa elimu bora kwa watoto masikini wa kitanzania,” alisema.

Fataki atinga bungeni

Salim Said

MBUNGE wa Sumbawanga (CCM), Paul Kimiti jana alizua kicheko kwa wabunge wenzake baada ya kuitaka serikali kuliangalia upya jina la watu wanaowapachika mimba wanafunzi la Fataki, kwa madai kuwa jina hilo ni la babu yake.

Kimiti ambaye ni mmoja kati ya wabunge waliokaa bungeni kwa muda mrefu na mwenye umri mkubwa, alitangaza kuachana na ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa ubunge, urais na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kimiti alimuomba Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza kuliangalia upya jina hilo kwa sababu huwa anaumia akisikia wanaitwa watu wanaowapachika mimba wanafunzi kwa kuwa ni jina la babu yake.

“Mheshimiwa Spika naomba serikali iliangalie upya jina la Fataki kwa watu hao kwa sababu ni jina la babu yangu,” alisema Kimiti bila ya kufafanua.

Kimiti hakufafanua iwapo babu yake anatumia jina hilo kama la utani au iwapo ni jina lake halisi alilopewa na wazazi wake.

Baada ya mbunge Kimiti kutoa hoja hiyo, Spika wa Bunge Samuel Sitta alihoji kwa utani iwapo babu yake alikuwa Fataki kweli au la.

“Lakini Mheshimiwa Kimiti hakutufafanulia iwapo babu yake alikuwa Fataki kweli au vipi,” alisema Spika Sitta huku wabunge wengine wakiangua kicheko.

Akijibu suala hilo, Mahiza alisema wizara yake itawatafutia jina jingine waharibifu hao ili kuepukana na kumkwaza mbunge Kimiti.

“Mheshimiwa Spika tutawatafutia jina jingine mafataki wa elimu nchini,” alijibu kwa ufupi Mahiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Ananilea Nkya alikiri kuwa jina hilo linaweza kuleta maumivu makali ikiwa ni jina halisi la mtu fulani katika jamii.

“Kwa kweli ikiwa ni jina halisi la mtu ni kweli linaweza kuleta maumivu makali, lakini hii ni changamoto kubwa katika sanaa zetu kuangalia kwanza kama majina tunayoyatumia hayataumiza baadhi ya watu,” alisema Nkya.

“Kwa kweli hata kama ni baba yangu au baba yako ndugu mwandishi usingefurahi kutokana na maana ya jina lile, ungejisikia vibaya hata mimi pia kama ni baba yangu ningejisikia vibaya.”

Hata hivyo, Nkya alisema ni vigumu kwa sasa kulifuta jina hilo katika nyoyo za watu kwa kuwa limeleta athari kubwa na kwamba lina maslahi ya umma.

“Kwa vile jina hili lina maslahi ya umma na limeleta athari sana katika sekta ya elimu, mheshimiwa Kimiti angejaribu kumuelewesha babu yake aone kama vile yeye ni msanii anatumia jina hilo, lakini sio sifa yake kwa sababu kitaaluma na kimaadili huwezi kumnusuru mtu mmoja kwa kuwaumiza wengi,” alisema Nkya.

Fataki ni tangazo lililobuniwa na wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kitengo cha kuzuia Ukimwi.

Membe: Ama zao ama zetu waliohusika rada

Salim Said

SAKATA la kashfa ya ununuzi wa rada ya kijeshi nchini, limeingia katika sura mpya baada ya serikali kuahidi lazima iwashughulikie watuhumiwa wote waliohusika katika kashfa hiyo, ili kulinda heshma ya nchi katika sura ya kimataifa.

Hivi karibuni kampuni ya BAE Systems inayodaiwa kumlipa dalali zaidi ya Sh12 bilioni kwa kufanikisha kwake serikali ya Tanzania kununua rada ya kijeshi ya Plessey Commander Fighter Control System kwa Sh 40 bilioni, imekiri makosa na kuahidi kurudisha fedha kwa serikali ya Tanzania.

Wiki iliyopita BAE System ilikiri kufanya makosa kwa kulipa rushwa katika mkataba wa kuiuzia serikali ya Tanzania rada hiyo ya kijeshi, chini ya Sheria ya Mikataba ya Makampuni ya mwaka 1985.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC), mjini Dodoma jana Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema lazima serikali isafishe wale wote waliohusika na kashfa hiyo kwa kulinda heshma ya nchi.

Alisema kashfa ya sakata la rada imefikia katika ukingo wake, baada ya BAE System kukiri makosa na kukubali kujisafisha kutokana na makosa hayo.

“BAE imejisafisha, imekiri makosa na imekubali kujisafisha na ule ndio uaminifu, wanakwenda wanafanya uchunguzi, wanagundua udhaifu, wanakiri makosa na wanajisafisha,” alisema Membe.

Membe alifafanua kuwa baada ya BAE System kukubali kujisafisha kwa kuirudishia Tanzania "chenji" yake, kazi kubwa iliyobaki ni kwa serikali kuhakikisha inawashughulikia wahusika.

Alisema, “…..lakini la pili ambalo sihitaji ushauri wala utaalamu kulisemea, ni kwamba safari hii ya sakata la rada imefikia ukingoni, wenzetu wameshajisafisha na sisi hatuna budi kujisafisha katika sura ya dunia,”.

“Kwa hiyo sasa shughuli ni kwetu sisi, mimi nina uhakika kabisa zile nchi zilizoguswa na kashfa hii zitachukuliwa kutoka pale, ili zisafishwe na sisi Watanzania sasa lazima tujiweke sawa tujisafishe katika sura ya kimataifa, yaani katika ngazi ya kimataifa ya nchi zinazoheshimika katika utawala bora,” alisisitiza Membe.

Membe alifafanua kuwa, “Lazima tulifikishe suala hili katika hitimisho lake, yani lazima tujisafishe, tukae vizuri ili tuonekane kwamba mashimo yote ya rushwa yamefukiwa na kama kuna mtu yeyote amehusika katika kashfa hii, hiki ndicho kipindi ambacho, utawala bora wa Tanzania unatakiwa kuimarishwa.”

Membe alisistiza kuwa suala la rada nchini halitopita hivihivi bila ya kuchukuliwa hatua za kisheria ili Tanzania ijionyeshe katika sura ya dunia kwamba inawajibika.

“Suala hili halitoisha hivihivi kwa sababu tumesemwa sana na lazima tujionyeshe katika serikali za dunia na katika uhusiano wa kimataifa kwamba na sisi tuko ‘responsive’ (tunawajibika) kwa maana tunajibu mapigo,” alisema Membe na kusisitiza;

“Kama hili limetokea na tumepata ushahidi, lazima tusafishane humu ndani kwa heshima ya nchi,”.

Juzi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Sofia Simba alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa hadi sasa hakuna taarifa rasmi ambayo serikali imepokea kuhusu sakata la kashfa ya rada, isipokuwa wamekuwa wakisoma katika magazeti na katika mitandao ya kimataifa.

Hata hivyo, aliahidi kuwa, watakaohusika katika kashfa hiyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Katika moja ya ziara zake nchini Uingereza, Rais Jakaya Kikwete aliambia Serikali ya Wingereza kwamba kama kuna fedha imezidi katika ununuzi wa rada anaomba chenji yao.

Membe alisema jana kuwa, hatimaye sasa chenji hiyo inarudi na kwa maana hiyo Tanzania imeula kwa kurudishiwa fedha hiyo takribani paundi 28 milioni kwani miradi mingi itafanikiwa.

“Tanzania tumeula na tunasema Alhamdulillaahi, nilisema na narudia tena kwa vile tunarudishiwa chenji yetu tumeula, miradi yetu itakwenda vizuri, kilimo kwanza kitakwenda vizuri, elimu yetu itakwenda vizuri na masuala mengine yatakwenda vizuri,” alisema Membe.

Wanaotuhumiwa na kashfa ya rada ni Mwanasheria Mkuu wa wakati huo Andrew Chenge, Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Dk Idrisa Rashid na dalali mwenye asili ya Asia, Saileth Vithlani.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni mtu alioongoza wanaharakati katika kufichua sakata la ununuzi wa rada na ndege ya rais tangu wakati wa rais Mkapa, alisema anashangazwa na kigugumizi cha serikali kuchangamkia fedha hizo.

“Nastaajabu sana ufisadi ndani ya nchi hii, nyinyi mmetapeliwa na taarifa zimo katika vyombo vya habari vya uhakika, lakini waziri anaulizwa anasema serikali haijapata taarifa rasmi, si ufuatilie,” alihoji Lipumba.

Alisema kigugumizi cha serikali kwenda kudai fedha hizo kinakuwapo kwa sababu, waliohusika na kashfa hiyo wapo madarakani na hivyo wanaogopa kuwajibika.