MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Sunday, July 19, 2009

Tatizo si wakristo bali ni maaskofu

Mwandishi Wetu
MWAKA 2006 tulishuhudia machafuko na mauaji katika wa nchi jirani ya Kenya Ingawa machafuko yalikuwa ya kisiasa lakini hasa yalikuwa ya kikabila.

Machafuko na mauaji yalitokea kwa kutokana na kile kilicho0nekana kuwa kabila moja kukandamiza makabila mengine. Kwa miaka mingi makabila mengine yalivumilia, lakini ikafika siku uvumilivu ukawashinda na wote tulishuhudia mauaji ya kikatili.


Huko Yugoslavia pia mauaji yalitokea miaka ya nyuma kwa sababu ya kidini yakihusisha Wakristo na Waislamu. Maelfu na maelfu ya watu waliuawa na hasa zaidi Waislamu.
Nasi Watanzania tusipokuwa makini basi, siku si nyingi tunaweza kujikuta tukianza kuchinjana kwa sababu ya kidini.


Kwenye bajeti ya mwaka huu Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema ya kuwa mapadri watano na mashehk wawili walimfuata nyumbani kumweleza matatizo yanayowakabili kuhusu misamaha ya kodi iliyokuwa imefutwa na Serikali.

Aliwataja mapadri kwa majina lakini masheikh hawakutajwa. Hili limechukuliwa na Waislamu kama ni dharau kwao. Likazua joto kwa Waislamu. Nao hawakulisemea hili lakini wakaanza kusema mambo ya Mahakama ya Kadhi na mambo ya kujiunga na OIC.


Mimi binafsi nashindwa kuelewa mambo yanayopingwa na ndugu zetu, si wakristo lakini maaskofu kama ifuatavyo.

Kuanzishwa Mahakama ya Kadhi kunawahusu au kuwapotezea usingizi vipi kwa kuwa atakayehukumiwa ni Muislamu na si Mkristo? Vile vile mambo mengi yatakayohukumiwa ni ya mashauri ya mirathi na ndoa, si ya makosa ya jinai. Sasa kinachowasumbua wenzetu ni kipi hasa.

Hakika kwa kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi hakuwezi kuifanya nchi kugeuka ya Kiislamu.kenya na Uganda ni majirani zetu wa karibu kabisa ambazo asilimia 20 au 30 raia wao ni waislamu.

Hapa kwetu zanzibar kuna mahakama ya kadhi, je lini tumesikia kuna mtu kakatwa mkono au ameuwawa kwa kupigwa mawe na hata ikitokea basi ndiyo dini ya waislamu inavyosema.je hizo nchi za Kenya na Uganda zimegeuzwa kuwa za kiislamu. Asilimia zaidi zaidi 30 ni waislamu lakini wamepewa haki yao , sisi sembuse zaidi ya asilimia 50?

Pili, kuhusu Tanzania kujiunga na OIC. Kwanza kabisa kujiunga na IOC hakuifanyi Tanzania kuwa nchi ya Kiislamu. Je , Uganda imekuwa nchi ya Kiisalamu baada ya kujiunga na OIC ? zambia na Malawi wana asilimia 5 peke yake ya waislamu nao wamejiunga na OIC je kumekuwa na matatizo gani.


Kama kuna faida ya kujiunga na OIC kwa kupata misaada kuna tatizo gani? Watakao faidika na misaada ni Watanzania si Waislamu peke yao .

Tulipojiunga na umoja wa nchi za madola mbona mashekhe hawakupiga makelele wala kulalamika.Nchi mama wa jumia za madola ni Uingereza na Uengereza na nchi ya kikristo.
Kama nchi yetu haina itikadi ya dini basi nasisi tujitoe kwenye jumiya hiyo.


Watanzania wenye dini mbali mbali hawaoni tatizo kuwa mwanachama wa jumuiya la madola ingawa ni ya kikristo kwani wano faidika ni watanzania wote sio wakristo pekee yao , kama vile vile watakao faidika na OIC in watanzania na sio waislamu peke yao .

Mbali na kuwa mwanachama wa jumiya ya madola ingawa Tanzania haina itikadi ya dini bado Tanzania ina uhusiano wa kibalozi na Vatican ambayo kwa 100% ni mamlaka ya kanisa katholiki.Hapa anayo uongoza Vatican na mwakilishi wake nchini na Tanzania inawakilishwa na balozi wetu Italia.

Kuna siku Mh Membe alisema ya kuwa Tanzania inafikiria kujiunga na OIC, maaskofu wakaja juu na kushika mapanga kumshambulia Mh Membe Mbona sisi Waislamu tukiumwa tunakwenda kutibiwa kwenye hospitali za misheni ( za Wakristo )?

Je, baada ya kupata matibabu Waislamu hugeuka kuwa Wakristo ?. kwakweli maaskofu hawana hoja hata moja lakini wamekuwa wanataka kuyumbisha serekali. Sijui kwa faida ya nani ? au wana lengo ambalo sijalijua.

Watoto wetu vile vile wanasoma shule za misheni ikibidi hata kubadilisha jina ilimradi apate elimu. Kwa kubadilisha jina mtu hawi Mkristo au Muislamu. Mtu anaweza kuuliza je, dini kweli inaweza kubagua kingilio kwa kubagua mtoto ana dini gani mpaka aamue kubadilisha jina? Huo ni ubaguzi, na hakuna dini inayokubali ubaguzi.

Nchi yetu imekuwa na sifa kubwa kabisa ya utulivu na amani. Sifa hiyo haiwapendezi watu wengi wa nje na hasa nchi za Magharibi na Marekani. Si ajabu kuwa nchi hizo ndiyo zinazochangia vurugu hizi ili umoja wetu ututoke na sisi tuwe kama nchi nyingine za Afrika. Vurugu na fujo kila siku.


Ni mataifa haya yaliyoleta sumu ya majina kama mtu mwenye siasa kali, mujahidina. Lakini Muislamu anayeitwa siasa kali ni yule masikini anayeswali mara tano, anaye funga mwezi mtukufu wa Ramadhani anaye shika nguzo tano za dini. Wanampachika jina baya ili wengine wasimfuate kushika nguzo tano.

Kwa upande wa wenzetu mtu akishika dini sawa sawa basi anapachikwa jina la mlokole. Jina mlokole anatafsiriwa kama mtu safi sana hatendi dhambi zozote. Jamani hii kweli ni sawa.
Mtu safi anayeshika dini ya Kiislamu au ya Kikristo anatakiwa apewe heshima sawa sawa si moja mlokole (msafi) na siasa kali (mkorofi). Mambo haya yanawakera Waislamu hata kama wamekaa kimya.


Miaka ya majuzi kulikuwa na Muislamu ambaye alikuwa anajenga miskiti katika Mkoa wa Iringa. Kwa shinikizo la Marekani akakamatwa na kuvuliwa uraia wa Tanzania na kurudishwa Saudia.

Je, mbona Waislamu hawaulizi makanisa tena makubwa yanajengwa kila siku hizo pesa zinatoka wapi. Lakini misikiti ikijengwa tu basi maswali 50 yatajitokeza.

Mimi binafsi sina tatizo kabisa na kujengwa hospitali au shule za kanisa. Kwani kazi kubwa ya dini ni kufundisha utulivu na amani. Nawashanga hao wanaopinga Waislamu wanapojenga misikiti na shule.

Niseme tu ya kuwa Watanzania tusipokuwa makini tutafika pabaya. Tuchezee kila kitu, lakini tusichezee moto wa kidini. Hakuna atakayepona ukianza kuwaka.

Tunaambiwa kuwa ukizungumza maswala haya serekali itakupeleka pabaya. Lakini kwa kuwa naependa nchi yangu yenye utulivu, sina budi nikayazungumza. Waswahili wanasema “ usipoziba ufa utajenga ukuta”.

Nawaomba waheshimiwa wabunge wapime uziri na ubaya wa wakujiunga na OIC halafu watoe maamuzi yao . Kwani wao sio wawakilishi wa makanisa au misikiti, wao wamekula kiapo ya kuwatumikia nchi yao bila kujali Rangi,Dini au Kabila.