MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Thursday, August 16, 2012

MAELFU WAKIMBIA MAKAZI YAO

KINSHASA
MAPIGANO ya miezi mitano sasa kati ya waasi wa kundi la M23 na Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya KONGO yamewalazimisha zaidi ya watu nusu milioni kukimbia makazi yao huko mashariki mwa nchi hiyo.
Ripoti zinasema kuwa raia wengi wa maeneo ya Kivu Kaskazini yenye utajiri mkubwa wa madini wamelazimika kukimbia makazi yao baada ya kujikuta katikati ya machafuko na mapigano ya kundi la M23 na Jeshi la serikali ya Kinshasa.
Maafa hayo yanaendelea kuwapata raia wa kawaida wa KONGO licha ya kuwepo maelfu ya askari wa Umoja wa Mataifa waliopelekwa nchini humo kwa ajili ya kulinda amani.
Mamia ya wakimbizi hao wa KONGO wamevuka mpaka na kuingia nchi jirani za RWANDA, BURUNDI na UGANDA huku Serikali ya KONGO ikitoa shutuma kali kwa nchi ya RWANDA na UGANDA kwa kuwaunga mkono waasi wa kundi la M23.
Waasi wa M23 walijitenga na jeshi la serikali ya Kinshasa wakidai kuwa serikali haijatekeleza vipengele vya makubaliano ya amani yaliyotiwa saini MACHI 23, 2009.

No comments:

Post a Comment