MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Thursday, August 16, 2012

HRW YAINGILIA KATI WAISLAAM KUKAMATWA ETHIPEA

ADDISABABA
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeitaka serikali ya Ethiopia kuwaachia huru viongozi 17 wa Kiislamu waliokamatwa katika maandamano ya amani yaliyofanyika nchini humo.
Taarifa iliyotolewa na hilo la Kutetea Haki za Binadamu imesema serikali ya Ethiopia inapaswa kuwaachia huru viongozi hao 17 wa Kiislamu waliotiwa nguvuni wakati askari wa usalama wa Ethiopea walipowakandamiza kinyama wapinzani Waislamu mjini Addis Ababa.
Watu hao walitiwa nguvuni katika maandamano makubwa ya amani yaliyofanywa na Waislamu mwezi jana kupinga uingiliaji usio wa kisheria wa serikali katika masuala ya Waislamu.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesisitiza kuwa mahabusu hao wanakabiliana na hali mbaya na wanashikiliwa bila ya kujulishwa makosa yao au kuwa na wakili.
Waislamu wanaunda zaidi ya asilimia 30 ya jamii ya watu milioni 83 ya Ethiopia.

No comments:

Post a Comment