MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Tuesday, June 9, 2009

Tani 3.8 za dawa zilizopita muda wa matumizi zateketezwa Dar

Salim Said

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), imeteketeza tani 3.8 za dawa za Viuavijasumu (antibiotics) jamii ya ‘Pencillin’, Unga wa Sindano ya Benzathine Pencillin kutoka China, zenye thamani ya 62.6 milioni baada ya kusadikiwa kutokidhi viwango vya ubora.

Dawa hizo zilikamatwa katika maduka mbalimbali ya dawa na makazi ya mfanyabiashara mmoja wa kichina, anayefahamika kwa jina la Du Juu Zhe yaliyopo Kariakoo Jijini Dar es Salaam, kufuatia msako mkali uliofanywa na maofisa wa TFDA na Jeshi la Polisi, Machi 22 mwaka huu, baada ya kumtilia shaka.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Magreth Ndomondo, Afisa Uhusiano wa Mamlaka hyo, Gaudensia Simwanza, alisema walimuhisi Zhe kuwa anatunza dawa katika jengo lisilo na usajili wa TFDA kwa ajili ya utunzaji wa dawa, jambo ambalo ni kinyume na Sheria Nambari 1 ya Chakula, Dawa na Vipodozi ya 2003.

“Muhusika anatambuliwa na TFDA kama muingizaji wa dawa husika nchini kutoka kiwanda kilichosajiliwa cha China, lakini katika msako huu tulikamata boksi 54 zilizoisha muda wake,” alisema Simwanza.

Alisema, dawa hizo toleo nambari 0602630 na 0602631, ambazo muda wake wa matumizi ulikwishapita tangu Febuari mwaka huu, zilikuwa zimesajiliwa na TFDA kwa nambari TAN 05,208J0H SH1, ambapo katika kila katuni ilikuwa na chupa 600.

“Kutokana na mazingira ya uhifadhi wa dawa hizo kutokidhi viwango, TFDA ilifuatilia jinsi dawa hizo zilivyosambazwa na kufanikiwa kuzuiya jumla ya boksi 173 zenye uzito wa tani 3.8 na thamani ya 62,640,000,” alisema Simwanza na kuongeza:

“Tulisitisha usambazaji na matumizi yake hadi hapo tutakapojiridhisha na ubora wa dawa hizo, lakini baada ya kufanya uchunguzi wa kimaabara kwa matoleo yote mawili, tulibaini kuwa hazikutimiza viwango na hivyo tukahikisha dawa hizo zinaondoka sokoni haraka ili ziteketezwe.”

Alisema, baada ya uamuzi huo walifanya utaratibu wa kuziteketeza dawa hizo na jana wakaamua kuziteketeza katika Dampo la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lililopo Puga Kinyamwezi.

“Leo (jana) tunateketeza dawa hizi baada ya kuhakikisha kuwa utaratibu umefuatwa ikiwa ni pamoja na vipimo na mmiliki kujiridhisha,” alisema Simwanza.

Uteketezwaji wa dawa hizo ulifanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi wenye silaha, mgambo wa Manispaa ya Temeke, TFDA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mei 26 mwaka huu, TFDA iliteketeza tani 34 za maziwa ya unga aina ya Golden Bell-Instant Full Cream kutoka China yaliyokuwa na thamani ya sh150 milioni, ambayo yalichanganywa na Kemikali aina ya ‘Melamine’ ambayo ni hatari kwa afya ya binadamu.

Kwa mujibu wa Sheria nambari moja ya Chakula, Dawa na Vipodozi ya mwaka 2003, mmiliki anapaswa kugharamia gharama zote za uteketezaji wa bidhaa zitakazogundulika kuwa chini ya ubora.


Ally Mzee 'bye bye' Bakwata

Salim Said

MUFTI wa Tanzania sheikh Issa Shaban Simba, amemfukuza kazi Katibu wa Baraza Kuu la Waislaam Tanzania (Bakwata) Mkoa wa Arusha sheikh Ally Juma Mzee kufuatia tuhuma mbalimbali za ubadhirifu wa mali zinazomkabili.

Sheikh Mzee alitenguliwa katika nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Bakwata taifa Mei mwaka huu na kuteuliwa kuwa Katibu wa baraza hilo Mkoa wa Arusha kabla ya kufukuzwa kazi.

Mabadiliko hayo ya uongozi Mkoa wa Arusha yamefanyika wakati Mufti Simba akiwa nchini Uturuki kwa ajili ya uchunguzi wa kawaida wa afya yake.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Bakwata sheikh Suleiman Lolila, aliwaarifu waislaam nchini kote kuhusu mabadiliko ya uongozi wa Bakwata Mkoa wa Arusha.

“Tunapenda kuwaarifu waislaam nchini kote mabadiliko ya uongozi wa Bakwata mkoani Arusha, ambapo Katibu wa baraza mkoa huo, sheikh Ally Juma Mzee amefukuzwa kazi na nafasi yake inachukuliwa na ustadh Abdulkarim Jonjo,” alisema sheikh Lolila na kuongeza:

“Tunawaomba waislaam nchini kote watoe ushirikiano wa hali na mali kwa Jonjo, ili tuweze kufanikisha kusogeza mbele uislaam.”

Kwa mujibu wa sheikh Lolila, sheikh Mzee kwa sasa anabakia kuwa muumini wa kawaida wa dini ya kiislaam, badala ya kushika nafasi yoyote ya uongozi wa baraza.

Aidha, sheikh Lolila alisema Mufti Simba bado yuko Ankara Uturukia katika hospitali Bingwa akiendelea na uchunguzi wa afya yake na kwamba anaendelea vizuri.

“Na hivi karibuni anakusudia kukutana na viongozi wa serikali ya nchi hiyo pamoja na viongozi mbalimbali wa taasisi za kiislaam za Uturuki, kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya waislaam wa Tanzania likiwamo la elimu,” alisema sheikh Lolila.

Kabla ya sheikh Mzee kufukuzwa kazi Masheikh na waumini mkoani Arusha, walishampinga Mzee, kuendelea kuongoza baraza hilo kwa madai kuwa hana sifa.

Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Arusha, Mahmoud Salum, alisema katika tamko lao mara baada ya kikao kilichofanyika katika Msikiti wa Ngarenaro Arusha kuwa, kwa kauli moja wanaunga mkono mapendekezo na uamuzi wa Halmashauri ya Ulamaa Mkoa wa Arusha kumfukuza ustadhi Mzee.

''Tuhuma zilizomkabili ustadhi Mzee ni nzito, hivyo haturidhishwi na utendaji wake na pia kupewa jukumu kubwa la Katibu Mkuu wa Bakwata kwani, hana sifa stahiki,'' alisema Sheikh Salum.

Aidha Mwananchi imebaini kuwa ustadhi Mzee anakabiliwa na tuhuma za kutumia mapato ya msikiti huo na kusababisha hasara kwa baraza.

Thursday, June 4, 2009

Mjomba Obama please translate this dramatic speech into practical

Cairo Egypt

Good afternoon. I am honored to be in the timeless city of Cairo and to be hosted by two remarkable institutions. For over a thousand years, Al-Azhar has had stood as a beacon of Islamic learning. And for over a century, Cairo University has been a source of Egypt's advancement.

Together, you represent the harmony between tradition and progress.

I'm grateful for your hospitality and the hospitality of the people of Egypt. And I'm also proud to carry with me the good will of the American people and a greeting of peace from Muslim communities in my country: Assalamu-alaikum.

(APPLAUSE)

We meet at a time of great tension between the United States and Muslims around the world, tension rooted in historical forces that go beyond any current policy debate.

The relationship between Islam and the West includes centuries of coexistence and cooperation but also conflict and religious wars.

More recently, tension has been fed by colonialism that denied rights and opportunities to many Muslims and a Cold War in which Muslim majority countries were too often treated as proxies without regard to their own aspirations. Moreover, the sweeping change brought by modernity and globalization led many Muslims to view the West as hostile to the traditions of Islam.

Violent extremists have exploited these tensions in a small but potent minority of Muslims.

The attacks of September 11, 2001, and the continued efforts of these extremists to engage in violence against civilians has led some in my country to view Islam as inevitably hostile not only to America and western countries but also to human rights.

All this has bred more fear and more mistrust. So long as our relationship is defined by our differences, we will empower those who sow hatred rather than peace, those who promote conflict rather than the cooperation that can help all of our people achieve justice and prosperity. And this cycle of suspicion and discord must end.

I've come here to Cairo to seek a new beginning between the United States and Muslims around the world, one based on mutual interest and mutual respect, and one based upon the truth that America and Islam are not exclusive and need not be in competition. Instead, they overlap and share common principles, principles of justice and progress, tolerance and the dignity of all human beings.

I do so recognizing that change cannot happen overnight. I know there's been a lot of publicity about this speech, but no single speech can eradicate years of mistrust nor can I answer in the time that I have this afternoon all the complex questions that brought us to this point.

But I am convinced that in order to move forward, we must say openly to each other the things we hold in our hearts and that too often are said only behind closed doors. There must be a sustained effort to listen to each other, to learn from each other, to respect one another, and to seek common ground.

As the Holy Quran tells us, Be conscious of God and speak always the truth.

(APPLAUSE)

That is what I will try to do today, to speak the truth as best I can. Humbled by the task before us and firm in my belief that the interests we share as human beings are far more powerful than the forces that drive us apart.

Now, part of this conviction is rooted in my own experience. I'm a Christian. But my father came from a Kenyan family that includes generations of Muslims. As a boy, I spent several years in Indonesia and heard the call of the azaan at the break of dawn and at the fall of dusk.

As a young man, I worked in Chicago communities where many found dignity and peace in their Muslim faith. As a student of history, I also know civilization's debt to Islam.

It was Islam at places like Al-Azhar that carried the light of learning through so many centuries, paving the way for Europe's renaissance and enlightenment. It was innovation in Muslim communities...

(APPLAUSE)

It was innovation in Muslim communities that developed the order of algebra, our magnetic compass and tools of navigation, our mastery of pens and printing, our understanding of how disease spreads and how it can be healed. Islamic culture has given us majestic arches and soaring spires, timeless poetry and cherished music, elegant calligraphy and places of peaceful contemplation. And throughout history, Islam has demonstrated through words and deeds the possibilities of religious tolerance and racial equality.

(APPLAUSE)

I also know that Islam has always been a part of America's story. The first nation to recognize my country was Morocco. In signing the Treaty of Tripoli in 1796, our second president, John Adams, wrote,

The United States has in itself no character of enmity against the laws, religion or tranquility of Muslims. And since our founding, American Muslims have enriched the United States.

They have fought in our wars. They have served in our government. They have stood for civil rights. They have started businesses. They have taught at our universities. They've excelled in our sports arenas.


They've won Nobel Prizes, built our tallest building and lit the Olympic torch. And when the first Muslim American was recently elected to Congress, he took the oath to defend our Constitution using the same holy Quran that one of our founding fathers, Thomas Jefferson, kept in his personal library.

(APPLAUSE)

So I have known Islam on three continents before coming to the region where it was first revealed. That experience guides my conviction that partnership between America and Islam must be based on what Islam is, not what it isn't. And I consider it part of my responsibility as president of the United States to fight against negative stereotypes of Islam wherever they appear.

(APPLAUSE)

But that same principle must apply to Muslim perceptions of America. Just as...

(APPLAUSE)

Just as Muslims do not fit a crude stereotype, America is not the crude stereotype of a self-interested empire. The United States has been one of the greatest sources of progress that the world has ever known. We were born out of revolution against an empire.

We were founded upon the ideal that all are created equal. And we have shed blood and struggled for centuries to give meaning to those words, within our borders and around the world.

We are shaped by every culture. Drawn from every end of the Earth, and dedicated to a simple concept, E pluribus unum: Out of many, one.

Now much has been made of the fact that an African-American with the name Barack Hussein Obama could be elected president.

(APPLAUSE)

But my personal story is not so unique. The dream of opportunity for all people has not come true for everyone in America, but its promise exists for all who come to our shores. And that includes nearly 7 million American Muslims in our country today who, by the way, enjoy incomes and educational levels that are higher than the American average.

Moreover, freedom in America is indivisible from the freedom to practice one's religion. That is why there is a mosque in every state in our union and over 1,200 mosques within our borders. That's why the United States government has gone to court to protect the right of women and girls to wear the hijab, and to punish those who would deny it.

So let there be no doubt...

(APPLAUSE)

... let there be no doubt, Islam is a part of America. And I believe that America holds within her the truth that regardless of race, religion, or station in life, all of us share common aspirations: to live in peace and security, to get an education and to work with dignity, to love our families, our communities, and our God. These things we share. This is the hope of all humanity.

Of course, recognizing our common humanity is only the beginning of our task."Words alone cannot meet the needs of our people. These nåeds will be mat only if we act boldly in the years ahead. And if we understand that the cèallenges we face are shared and our failure to meet them will hurt us all.

Foò we have learned from recent experience that when a financial system weakens in one country, prosperity is hurt everywhere. When a new flu infects one human being, all are at risk. When one nation pursues a nuclear weapon, the risk of nuclear attack rises for all nations.

When violent extremists operate in one stretch of mountains, people are endangered across an ocean. When innocents in Bosnia and Darfur are slaughtered, that is a stain on our collective conscience.

(APPLAUSE)

That is what it means to share this world in the 21st Century. That is the responsibility we have to one another as human beings. This is a difficult responsibility to embrace, for human history has often been a record of nations and tribes, and<>

They have killed people of different faiths but, more than any other, they have killed Muslims. Their actions are irreconcilable with the rights of human beings, the progress of nations, and with Islam.

The Holy Quran teaches that whoever kills an innocent is as -- it is as it if has killed all mankind.

(APPLAUSE)

And the Holy Quran also says whoever saves a person, it is as if he has saved all mankind.

(APPLAUSE)

The enduring faith of over a billion people is so much bigger than the narrow hatred of a few. Islam is not part of the problem in combating violent extremism; it is an important part of promoting peace.

Now, we also know that military power alone is not going solve the problems in Afghanistan and Pakistan. That's why we plan to invest $1.5 billion each year over the next five years to partner with Pakistanis to build schools and hospitals, roads and businesses, and hundreds of millions to help those who've been displaced.

That's why we are providing more than $2.8 billion to help Afghans develop their economy and deliver services that people depend on.

Now, let me also address the issue of Iraq. Unlike Afghanistan, Iraq was a war of choice that provoked strong differences in my country and around the world. Although I believe that the Iraqi people are ultimately better off without the tyranny of Saddam Hussein, I also believe that events in Iraq have reminded America of the need to use diplomacy and build international consensus to resolve our problems whenever possible.

(APPLAUSE)

Indeed, we can recall the words of Thomas Jefferson, who said, I hope that our wisdom will grow with our power and teach us that the less we use our power, the greater it will be. Today America has a dual responsibility to help Iraq forge a better future and to leave Iraq to Iraqis.

I have made it clear to the Iraqi people...

(APPLAUSE)

I have made it clear to the Iraqi people that we pursue no basis and no claim on their territory or resources. Iraq's sovereignty is its own. And that's why I ordered the removal of our combat brigades by next August. That is why we will honor our agreement with Iraq's democratically-elected government to remove combat troops from Iraqi cities by July and to remove all of our troops from Iraq by 2012.

(APPLAUSE)

We will help Iraq train its security forces and develop its economy. But we will support a secure and united Iraq as a partner and never as a patron.

And finally, just as America can never tolerate violence by extremists, we must never alter or forget our principles. 9/11 was an enormous trauma to our country. The fear and anger that it provoked was understandable. But in some cases, it led us to act contrary to our traditions and our ideals.

We are taking concrete actions to change course. I have unequivocally prohibited the use of torture by the United States. And I have ordered the prison at Guantanamo Bay closed by early next year.

(APPLAUSE)

So America will defend itself, respectful of the sovereignty of nations and the rule of law. And we will do so in partnership with Muslim communities, which are also threatened. The sooner the extremists are isolated and unwelcome in Muslim communities, the sooner we will all be safer.

Now, the second major source of tension that we need to discuss is the situation between Israelis, Palestinians and the Arab world. America's strong bonds with Israel are well-known. This bond is unbreakable. It is based upon cultural and historical ties and the recognition that the aspiration for a Jewish homeland is rooted in a tragic history that cannot be denied.

Around the world the Jewish people were persecuted for centuries. And anti-Semitism in Europe culminated in an unprecedented holocaust. Tomorrow I will visit Buchenwald, which was part of a network of camps where Jews were enslaved, tortured, shot and gassed to death by the Third Reich.

Six million Jews were killed, more than the entire Jewish population of Israel today. Denying that fact is baseless. It is ignorant, and it is hateful.

It's about preventing a nuclear arms race in the Middle East that could lead this region and the world down a hugely dangerous path.

Now, I understand those who protest that some countries have weapons that others do not. No single nations should pick and choose which nation holds nuclear weapons. And that's why I strongly reaffirmed America's commitment to seek a world in which no nations hold nuclear weapons.

(APPLAUSE)

And any nation, including Iran, should have the right to access peaceful nuclear power if it complies with its responsibilities under the Nuclear Non-Proliferation Treaty. That commitment is at the core of the treaty. And it must be kept for all who fully abide by it. And I am hopeful that all countries in the region can share in this goal.

The fourth issue that I will address is democracy.

(APPLAUSE)

I know there has been controversy about the promotion of democracy in recent years. And much of this controversy is connected to the war in Iraq. So let me be clear. No system of government can or should be imposed by one nation by any other. That does not lessen my commitment, however, to governments that reflect the will of the people.

Each nation gives life to this principle in its own way, grounded in the traditions of its own people. America does not presume to know what is best for everyone, just as we would not presume to pick the outcome of a peaceful election.

But I do have an unyielding belief that all people yearn for certain things: the ability to speak your mind and have a say in how you are governed, confidence in the rule of law and the equal administration of justice, government that is transparent and doesn't steal from the people, the freedom to live as you choose. These are not just American ideas. They are human rights. And that is why we will support them everywhere.

(APPLAUSE)

Now, there is no straight line to realize this promise. But this much is clear. Governments that protect these rights are ultimately more stable, successful and secure. Suppressing ideas never succeeds in making them go away. America respects the right of all peaceful and law-abiding voices to be heard around the world, even if we disagree with them. And we will welcome all elected, peaceful governments, provided they govern with respect for all their people.

This last point is important because there are some who advocate for democracy only when they're out of power. Once in power, they are ruthless in suppressing the rights of others.

(APPLAUSE)

So no matter where it takes hold, government of the people and by the people sets a single standard for all who would hold power. You must maintain your power through consent, not coercion. You must respect the rights of minorities and participate with a spirit of tolerance and compromise. You must place the interests of your people and the legitimate workings of the political process above your party.

Without these ingredients, elections alone do not make true democracy.

(AUDIENCE MEMBER SHOUTS)

Thank you.

(APPLAUSE)

The fifth issue that we must address together is religious freedom. Islam has a proud tradition of tolerance. We see it in the history of Andalusia and Cordoba during the Inquisition. I saw it firsthand as a child in Indonesia where devote Christians worshipped freely in an overwhelmingly Muslim country.

That is the spirit we need today. People in every country should be free to choose and live their faith based upon the persuasion of the mind and the heart and the soul.

This tolerance is essential for religion to thrive. But it's being challenged in many different ways. Among some Muslims, there's a disturbing tendency to measure one's own faith by the rejection of somebody else's faith.

The richness of religious diversity must be upheld, whether it is for Maronites in Lebanon or the Copts in Egypt.

(APPLAUSE)

And if we are being honest, fault lines must be closed among Muslims as well as the divisions between Sunni and Shia have led to tragic violence, particularly in Iraq.

Freedom of religion is central to the ability of peoples to live together. We must always examine the ways in which people protect it. For instance, in the United States, rules on charitable giving have made it harder for Muslims to fulfill their religious obligation.

That's why I'm committed to work with American Muslims to ensure that they can fulfill zakat. Likewise, it is important for Western countries to avoid impeding Muslim citizens from practicing religion as they see fit, for instance, by dictating what clothes a Muslim woman should wear.

We can't disguise hostility towards any religion behind the pretense of liberalism. In fact, faith should bring us together. And that's why we're forging service projects in America to bring together Christians, Muslims, and Jews.

That's why we welcome efforts like Saudi Arabian King Abdullah's interfaith dialogue and Turkey's leadership in the Alliance of Civilizations.

Around the world, we can turn dialogue into interfaith service so bridges between peoples lead to action, whether it is combating malaria in Africa or providing relief after a natural disaster.

The sixth issue -- the sixth issue that I want to address is women's rights.

(APPLAUSE)

I know...

(APPLAUSE)

I know, and you can tell from this audience, that there is a healthy debate about this issue. I reject the view of some in the West that a woman who chooses to cover her hair is somehow less equal. But I do believe that a woman who is denied an education is denied equality.

(APPLAUSE)

And it is no coincidence that countries where women are well- educated are far more likely to be prosperous.

Now let me be clear, issues of women's equality are by no means simply an issue for Islam. In Turkey, Pakistan, Bangladesh, Indonesia, we've seen Muslim-majority countries elect a woman to lead.

Meanwhile, the struggle for women's equality continues in many aspects of American life and in countries around the world. I am convinced that our daughters can contribute just as much to society as our sons.

(APPLAUSE)

Our common prosperity will be advanced by allowing all humanity, men and women, to reach their full

Mkulo: Mfumko wa bei haudhibitiki

Salim Said

SERIKALI haiwezi kudhibiti kushuka au kupanda kwa thamani ya Shilingi kwa kuwa thamani ya fedha, inategemea nguvu ya uchumi wa nchi.

Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkulo, aliwaeleza wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Fedha na Uchumi kuwa, tatizo hilo halizuiliki kwa sababu ni la kimfumo.

“Mheshimiwa Mwenyekiti tutake tusitake, tatizo la kupanda na kushuka kwa sarafu ya Tanzania lipo na serikali haiwezi kulizuia kwa sababu ni la kimfumo,” alisema Mkulo.

Alifafanua, kinachofanya serikali kukabiliana na tatizo hilo ni kuangalia iwapo mzunguko wa Shilingi ya Tanzania unaendana na uchumi wa soko au vinginevyo.

“Kama mzunguko ni mbaya tunaweza kuingilia na kurekebisha lakini, kama unaendana na uchumi wa soko, hatuwezi kuingilia hata kidogo,” alisisitiza Mkulo.

Alisema, kupanda na kushuka kwa sarafu ya Tanzania kunategemea nguvu ya uchumi wa soko, mfumuko wa bei za bidhaa muhimu na upatikanaji wa fedha za kigeni kwa msimu.

“Upatikanaji wa fedha za kigeni nchini unategemea kuanza Juni hadi Disemba lakini pia tukiweza kudhibiti mfumko wa bei ya bidhaa muhimu tunaweza kudhibiti thamani ya Shilingi yetu, ” alieleza.

Kwa mujibu wa Mkulo, thamani ya Shilingi ya Tanzania imeshuka hadi kufikia wastani wa Sh1,280.30 kwa Dola ya Marekani Desemba mwaka jana ikilinganishwa na Sh1,132.09 Desemba 2007.

Alisema, mfumko wa bei kwa mwaka 2008, ulikua kwa asilimia 10.3 ikilinganishwa na asilimia 7.0 mwaka 2007. Kiwango cha chini cha kasi ya mfumko huo 2008, ilikuwa Januari kilipopanda kwa asilimia 8.6 na kiwango cha juu asilimia 13.5 Disemba mwaka huohuo.

“Lengo letu la mfumko lilikuwa asilimia 5.0 Juni 2008, lakini halikufikiwa kutokana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji hasa baada ya kupanda kwa bei ya nishati ya mafuta na umeme,” alisema Mkulo na kuongeza:

“Hadi April 2009, mfumko ulifikia asilimia 12.0 kutokana na hali hiyo, ambapo awali lengo la mfumko huo lilitarajiwa liwe chini ya asilimia 7.5 ifikapo Juni 2009, lakini sasa tunatarajia asilimia 11.0.”


Tuesday, June 2, 2009

Rais kuhutubia Bunge la Bajeti

Salim Said
RAIS Jakaya Kikwete anatarajia kulihutubia Bunge la Bajeti linalotarajiwa kuanza Juni 9 mwaka huu.

Katika hotuba yake, rais Kikwete anatarajia kuzaungumzia athari za mtikisiko wa kiuchumi nchini, baada ya kupokea ripoti ya timu ya wataalamu, aliyoiunda miezi mitatu iliyopita kwa ajili ya kutathmini athari za mtikisiko huo.

Tume hiyo iliyofanya kazi chini ya mwenyekiti Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Professa Benno Ndulu itawasilisha ripoti yake kwa Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkullo Juni 4 mwaka huu.

Akitoa majumuisho ya semina ya Hali ya uchumi wa Tanzania, kwa wabunge wa Kamati ya kudumu ya Fedha na Uchumi, waziri Mkullo alisema, tume ya rais ya kutathmini athari za mtikisiko wa kiuchumi imemaliza kazi yake na itawasilisha kwake ripoti ya kazi hiyo, Juni 4 mwaka huu.

“Baada ya kwangu kuwasilisha hiyo, nitaifikisha kwa rais ambaye ataitisha kikao cha dharura cha baraza la Mawaziri ili kuijadili na hapo itakuwa ni ya serikali na si ya wizara tena,” alisema Waziri Mkullo na kuongeza:

“Kutokana na unyeti na uzito wa ripoti hiyo rais ataomba rasmi ruhusa ya kulihutubia bunge la bajeti linalotarajiwa kuanza Juni 9 mwaka huu.”

Alisema, pamoja na mambo mingine, rais anatarajiwa kuzungumzia athari za mtikisiko wa kiuchumi duniani na Tanzania kwa upekee.

“Rais ataelezea mwelekeo wa nchi kiuchumi, tuko wapi, tunaelekea wapi na serikali ina mkakati gani katika kuhakikisha inainua uchumi wake baada ya kukumbwa na mtikisiko huo,” alisema Mkullo.

Alisema, athari za kiuchumi nchini ni tofauti kabisa na zile za Marekani na Ulaya, hivyo hata jina la mtikisiko huo linaweza kubadilika katika ripoti ya profesa Ndulu.

Waziri Mkullo alisema, serikali imeandaa miradi mitatu mikubwa ya kuhakikisha inaboresha bandari yake ya Dar es Salaam kwa ajili ya kukuza uchumi na pato la taifa.

“Tunao mradi wa kwanza wa kuboresha reli ya kati kutoka Isaka hadi Kigali na kutoka Isaka, Shinyanga kuja Dar es Salaam ambayo itakuwa reli ya kisasa yenye geji kubwa,” alisema Mkullo.

Alisema, mradi mwingine ni ule wa Kanda ya kusini na kaskazini (North-South Coridor) ambao utajumuisha Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, SADC na Comesa.

“Mradi wa tatu ni upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam kieneo na kina cha maji ili meli kubwa zaidi ziweze kuja kwa sababu hivi sasa mfano ukisema ushushe tani 15 milioni kwa siku unatafuta ugomvi,” alisema Mkullo.

Alisema, wafadhili wa miradi hiyo tayari wameshapatikana na wataalamu wanaendelea na kazi ya kufanya usanifu wa miradi hiyo na kwamba baada ya miezi mitatu watakutana nao.

Waziri Mkullo alisema, uundwaji wa tume ya mipango tayari umekamilika kimfumo na kwamba muda wowote kuanzia sasa rais Kikwete atatangaza timu ya wataalamu watakaoiendesha.

“Timu hii ni tofauti kabisa na ile ya mwanzo tangu enzi ya wizara ya mipango, itakuwa tume ya wataalamu na wala hamtakuwa na wanasiasa kwa sababu za kiufanisi,” alisema Mkullo.

Kwa upande wao, wabunge wingi wa kamati hiyo walioneshwa kutoridhishwa kwao na utendaji wa bandari ya Dar es Salaam na kuendelea kuwepo kwa mwekezaji wa kupakia na kupakua makontena (Tics) wakidai kuwa ni donda ndugu na serikali imeshindwa kumchukulia hatua.

Bonyokwa walia na barabara

Bonyokwa walilia barabara

Salim Said
CHAMA cha Madereva na Makondakta wa daladala zinazotoa huduma za usafiri kati ya Bonyokwa na Kimara Mwisho, kimeiomba serikali kukarabati barabara inayotumiwa magari hayo, ili kuepushia adha wananchi.

Chama hicho kimesema hali ya barabara hiyo ni mbaya na haipitiki kwa urahisi.

Wakizungumza na Mwananchi katika ofisi za chama hicho jana, baadhi ya viongozi walisema barabara inayounganisha Bunyokwa na Kimara Miwsho, imeharibiwa na mvua zilizomalizika hivi karibuni.

Mwenyekiti wa chama hicho, Shaaban Yussuf, alisema hali hiyo imekuwa ikisababisha magari kuharibika na hivyo kuwa kero kwa wananchi.

“Njia hii ina abiria wingi lakini utakuta gari ni chache, kwa sababu matajiri hawataki kupeleka gari zao kwa sababu ya ubovu wa barabara,” alisema Yussuf.

Alisema kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hiyo, kuna haja kwa mamlaka zinazohusika kuifanyia matengenezo ya haraka.

Shaban pia alikanusha madai kuwa chama hicho kimekuwa kikikusanya fedha kwa ajili matengenezo ya barabara hiyo.

“Madai hayo hayana ukweli, nadhani yakuzwa na watu wanaotaka kuwania uongozi katika serikali za mitaa,” alinena.

Kwa upande wake, Katibu wa chama hicho, Peter Mbuya, alisema wao kama wadau, wameamua kurekebisha baadhi ya maeneo korofi katika barabara hiyo, ili kurahisisha usafiri kwa wananchi.

Monday, June 1, 2009

TFDA kubadili maduka 9,000 ya dawa baridi kuwa ya dawa muhimu

Salim Said

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), imesema inatarajia kubadilisha maduka 9,000 ya dawa baridi kuwa ya dawa muhimu (ADDO) hadi kufikia mwaka 2010 nchini kote.

Pamoja na lengo hilo, hadi sasa mamlaka hiyo tayari imeboresha na kubadilisha maduka 1200 ya dawa baridi na kuwa ya dawa muhimu katika mikoa minne ya Tanzania.

Kaimu Mkurugenzi wa Dawa na Vipodozi wa TFDA Hiiti Sillo aliiambia Mwananchi mwisho wa wiki iliyopita, kwamba pamoja na kuwaagiza wamiliki wa maduka ya dawa baridi kuyaboresha maduka yao ili yawe ya dawa muhimu, pia wanatoa mafunzo ya bure kwa watoa huduma wa maduka hayo, na kuwatunuku vyeti.

“Kwanza tunawaagiza wamiliki waboreshe maduka yao ya dawa baridi ili tuwapatie leseni za maduka ya dawa muhimu, wakikataa tunayafungia,” alisema Sillo.

Sillo alizungumza na Mwananchi Kibaha mkoani Pwani, mara baada ya kuwatunuku vyeti wahitimu 486 vya kuhitimu mafunzo ya siku 35 ya kutoa huduma katika maduka ya dawa muhimu.

“Tunashukuru leo tumewakabidhi vyeti wahitimu hawa ambao asilimia 99 ni wanawake na wameweza kushona unifomu za kutoa huduma za dawa zenye nembo ya TFDA,” alisema Sillo.

Alisema, TFDA kwa sasa imefanikiwa kubadilisha maduka ya dawa baridi 1200 na kuwa ya dawa muhimu, katika mikoa minne ambapo lengo ni kufikia mikoa 10 hadi mwisho wa mwaka huu.

Sillo aliitaja mikoa hiyo, ni Ruvuma, Morogoro, Rukwa, Mtwara, Pwani, Lindi, Mbeya, Tanga, Kigoma na Singida.

“Tumewafundisha utaalamu wa kutunza na kuhifadhi dawa, mawasiliano na wagonjwa, namna ya kutoa dozi na hasara zake ikiwa haitokamilishwa au ikizidishwa,” alisema Sillo.

Alisema, mafunzo hayo yalifadhiliwa kwa ushirikiano wa TFDA na Mfuko wa dunia wa kupambana na Ukimwi, Malaria na Kifua kikuu (Global Fund), Shirika la Misaada la Denmark (Danida), Serikali ya Tanzania na washiriki wenyewe.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Dk Eligreta Mzava alisema mafunzo hayo, yatausaidia mkoa wa Pwani kuondokana na tatizo la vioski vya dawa baridi.

Dk. Mzava, alisema, TFDA imewasaidia kuondokana na ‘vioski’ vya madawa kwa kuwapatia mafunzo ya ufamasia watoa huduma katika maduka ya dawa mkoani mwake.

“Mafunzo haya kwa watoa huduma katika maduka ya dawa mkoani mwetu yatatusaidia kuondokana na tatizo la watoa huduma wasio na taaluma ya ufamasia na pia itatusaidia kuondokana na ‘vioski’ vya madawa,” alisema Dk Mzava na kuongeza:

“Kwa muda mrefu tulikuwa hatuna maduka ya dawa bali tulikuwa na ‘vioski’ vya madawa, lakini baada ya mafunzo haya tunashukuru na tunaamini sasa tutapunguza kama si kumaliza kabisa tatizo hilo.”

Lize Mwampasha, ambaye ni mmoja wa wahitimu alisema, mafunzo hayo yatawasaidia wao kuaminika katika jamii, kwa sababu walikuwa wanapata matatizo ya kutotambulika na kuaminika kama wao ni watoa huduma za dawa.

“Mtu anakuja anakuuliza we umesomea, unajaribu kumuelewesha, lakini ni kazi kweli mpaka akuelewe. Hivi sasa akija ananikuta na nguo za kiuguzi zenye nembo ya TFDA na cheti ninacho basi, itasaidia kuniamini,” alisema Mwampasha.