Salim Said na Ellen Manyangu
SIKU moja baada ya mjane Shamsa Nassor kuhamishwa nyumbani mwake kikatili, Kiluvya jijini Dar es Salaam, Mahakama ya Ardhi Wilaya ya Kinondoni imeamrisha mama huyo arudishwe nyumbani mwake.
Aidha, Kampuni ya Namic Auction Mart ilipewa kazi ya kumrudisha nyumbani mwake mjane huyo chini ya usimamizi mkali wa Polisi kutoka Wilaya ya kipolisi Kimara.
Amri hiyo, nakala tunayo, ilitolewa jana na kusainiwa na Mwenyekiti wa Mahakama ya Ardhi Kinondini Joseph Kaale na kukabidhiwa kwa kampuni ya Namic kwa ajili ya utekelezaji.
“Mahakama imeamrisha kwamba muombaji katika ombi hili arudishwe nyumbani mwake ambamo alitolewa bila ya sababu za msingi, haraka iwezekanavyo” alisema Kaale katika nakala ya amri hiyo.
Safari ya kwenda kumrudisha nyumbani mwake mjane huyo, ilianzia Kinondoni kupitia kituo cha polisi Mbezi, ofisi ya serikali ya Mtaa Kiluvya na Mjumbe wa Shina la eneo hilo.
Ilichukua takriban masaa mawili hadi juhudi za Mkurugenzi Mtendaji wa Namic Michael Mwenda kufanikiwa kuopata asakari wawili kwa ajili ya kulinda amani na usalama wakati wa urudishwaji wa mjane huyo.
Aidha baada ya kufika eneo la tukio, askari wa Kampuni ya Ulinzi ya General na mwakilishi wa Abdallah Malik aliyejitambulisha kwa jina la Abdu Mkata waligoma kufungua lango la kuingilia licha ya askari waliotumwa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kimara (OCD) N. Ndaki.
“Mimi sipo tayari kufungua nipo tayari hata kufa, kufungwa au kukamatwa na polisi. Subirini niwasiliane na Malik au turudini kwa OCD” alisema Mkata.
“Usikubali, usikubali bora tukalale ndani kuliko kumwachia huyu mama aingie humu ndani kwa kuwa Malik hatatuelewa,” alisistiza kumueleza Mkuu wa General Guard Haroub Mbelwa.
Hata hivyo, Mwenda aliamua kuwasiliana na OCD na kumueleza kwamba amri iliyotumika kumtoa mama huyo haikufuata utaratibu na kwamba amri kumrudisha ni halali na kwa hiyo atakaekaidi atashitakiwa.
Baada ya majibizano marefu kati ya askari hao na Viongozi wa Namic hatimae waliachia ngazi bila ya kutoa funguo na wao kuamua kurudi kituo cha polisi Mbezi kwa ajili ya kumuona OCD kwa majadiliano zaidi.
Baada ya wao kuondoka uamuzi wa kuvunja kufuli na minyororo katika milango ya kuingia ndani ya eneo na nyumba ya mjane huyo ulipitishwa na kufanywa na viongozi wa Namic.
Kwa upande wake Shamsa alilishukuru sana gazeti la Mwananchi kwa kuandika habari hiyo pamoja na mahakama ya ardhi kwa kumpatia amri ya kurudishwa ndani ya nyumba yake.
“Nimefurahi sana, pia natoa shukurani zangu kwa gazeti la Mwananchi maana leo (jana) tangu asubuhi napokea simu za pole kutoka na habari hiyo. Lakini nawaomba muendele kufuatilia, serikali nayo ifuatilie ili ijue ukweli wa kesi,” alisema Shamsa na kuongeza:
“Lakini hofu yangu ni usalama na amani yangu kwa kuwa tukio hili limenitisha sana na chochote kinaweza kikanitokea kutokana na vitisho nilivyopewa na shemeji yangu Malik.”
Hadi Mwenanchi inaondoka eneo la tukio jana majira ya saa 11:05 OCD Ndaki alipiga simu na kumtaka Shamsa kuripoti Polisi Kimara kwa taratibu zaidi za kipolisi.
Shamsa alihamishwa nyumbani mwake kwa nguvu juzi na kampuni ya Yono Auction Mart, kitendo ambacho kilimsababishia hasara na majeraha mwilini.
MARASHI
PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL
Thursday, May 28, 2009
Wednesday, May 27, 2009
TFDA yateketeza tani 34 za Maziwa hatari kutoka China
Salim Said
HATIMAYE Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeteketeza tani 34 za maziwa ya unga aina ya Golden Bell-Instant Full Cream kutoka nchini China yenye thamani ya sh150 milioni, ambayo yamechanganywa na Kemikali aina ya ‘Melamine’.
Uteketezaji wa maziwa hayo, ulifanyika jana chini ya uangalizi mkali wa polisi wenye silaha katika Dampo la Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam eneo la Pugu Kinyamwezi.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya uteketezaji huo, Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula wa TFDA Raymond Wigenge alisema, Maziwa hayo yalikamatwa Septemba mwaka jana lakini yalichelewa kuteketezwa kutokana na taratibu za kimaabara baina ya mmiliki na TFDA.
Alisema, taarifa za kuwepo kwa maziwa yaliyochanganywa kemikali ya ‘Melamine’ walizipata kutoka kwa Mtandao wa Mamlaka za Udhibiti wa Usalama wa Vyakula Duniani (Inforsan) na walipofanya uchunguzi waligundua kuwapo kwa maziwa hayo nchini.
“Hatua ya kwanza baada ya kupata taarifa hiyo tulisitisha uingizaji na pili tulifanya ukaguzi nchini kote na kukamata tani nyingi za maziwa hayo. Tatu tulipeleka ‘sampo’ vigezo katika maabara za Afrika ya Kusini na za TFDA kwa ajili ya vipimo,” alisema Wigenge na kuongeza:
“Tulichukua aina 94 za bidhaa nyengine za maziwa zilizomo ndani ya soko nchini kwa ajili ya vipimo, lakini hatukubaini maziwa yaliyochanganywa ‘melamine’ zaidi ya huyo mtu mmoja ambaye alikuwa anaingiza kihalali.”
Alifafanua kuwa, Mmiliki wa maziwa hayo ambaye ni Kampuni ya Vin Mart Ltd hakuridhika na vipimo hivyo na alitaka kupelekwa vigezo vya maziwa hayo katika maabara za Ubeligiji na Ufaransa, ambako pia matokeo yake yalilingana na ya TFDA na ya Afrika ya Kusini.
“Leo ndio tumeamua kuyateketeza baada ya mmiliki kujiridhisha na vipimo vilivyofanywa katika maabara nne zikiwa ni ya TFDA, Afrika ya Kusini, Ufaransa na Ubeligiji ambako majibu yalilingana,” alisema Wigenge.
Alisema, mmiliki huyo hakuwa na kosa, kwa sababu maziwa hayo yaliingizwa kemikali hiyo kiwandani nchini China, ikiwa ni mbinu ya kuongeza virubitisho vya Protini kutokana na tabia ya wafugaji wa nchi hiyo kuweka maji katika maziwa baada ya kuyakamua.
“Kama mmiliki atataka kudai fidia kutoka kwa kampuni iliyotengeneza maziwa haya, sisi tunaweza kutoa ushirikiano kwa kuthibitisha kuwa tuliyaharibu kwa kuwa yalikuwa na kemikali yenye madhara kwa afya ya binadamu,” alisema Wigenge.
Hata hivyo Wigenge alithibitisha kuwa, mmiliki wa maziwa hayo hana kosa kwa sababu kemikali ya ‘melamine’ ambayo inasababisha ugonjwa wa figo hasa kwa watoto haikuwa kigezo cha kupima ubora wa maziwa hapo awali.
Uteketezaji huo ulifanyika chini ushuhuda wa maafisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), TFDA, Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC), polisi, na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
Afisa Mkuu wa Forodha kutoka TRA Tmeke Peles Mwaipopo alisema, wao kazi yao ni kushuhudia tu na kuthibitisha kwamba uteketezaji umefanyika na si vyenginevyo.
“Baada ya hapa tutaandika ripoti kwa ajili ya kuiwasilisha kwa wakuu wetu kama kumbukumbu ili siku yoyote mmiliki akilalamika tunatoa ushahidi kuwa kitendo hicho kilifanyika,” alisema Mwaipopo.
Kwa mujibu wa sheria anayekamatwa na bidhaa bandia hupaswa kugharamia hasara yote ya uteketezaji wa bidhaa hiyo ikiwa ni pamoja na usafiri, posho za maofisa na wabebaji.
HATIMAYE Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeteketeza tani 34 za maziwa ya unga aina ya Golden Bell-Instant Full Cream kutoka nchini China yenye thamani ya sh150 milioni, ambayo yamechanganywa na Kemikali aina ya ‘Melamine’.
Uteketezaji wa maziwa hayo, ulifanyika jana chini ya uangalizi mkali wa polisi wenye silaha katika Dampo la Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam eneo la Pugu Kinyamwezi.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya uteketezaji huo, Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula wa TFDA Raymond Wigenge alisema, Maziwa hayo yalikamatwa Septemba mwaka jana lakini yalichelewa kuteketezwa kutokana na taratibu za kimaabara baina ya mmiliki na TFDA.
Alisema, taarifa za kuwepo kwa maziwa yaliyochanganywa kemikali ya ‘Melamine’ walizipata kutoka kwa Mtandao wa Mamlaka za Udhibiti wa Usalama wa Vyakula Duniani (Inforsan) na walipofanya uchunguzi waligundua kuwapo kwa maziwa hayo nchini.
“Hatua ya kwanza baada ya kupata taarifa hiyo tulisitisha uingizaji na pili tulifanya ukaguzi nchini kote na kukamata tani nyingi za maziwa hayo. Tatu tulipeleka ‘sampo’ vigezo katika maabara za Afrika ya Kusini na za TFDA kwa ajili ya vipimo,” alisema Wigenge na kuongeza:
“Tulichukua aina 94 za bidhaa nyengine za maziwa zilizomo ndani ya soko nchini kwa ajili ya vipimo, lakini hatukubaini maziwa yaliyochanganywa ‘melamine’ zaidi ya huyo mtu mmoja ambaye alikuwa anaingiza kihalali.”
Alifafanua kuwa, Mmiliki wa maziwa hayo ambaye ni Kampuni ya Vin Mart Ltd hakuridhika na vipimo hivyo na alitaka kupelekwa vigezo vya maziwa hayo katika maabara za Ubeligiji na Ufaransa, ambako pia matokeo yake yalilingana na ya TFDA na ya Afrika ya Kusini.
“Leo ndio tumeamua kuyateketeza baada ya mmiliki kujiridhisha na vipimo vilivyofanywa katika maabara nne zikiwa ni ya TFDA, Afrika ya Kusini, Ufaransa na Ubeligiji ambako majibu yalilingana,” alisema Wigenge.
Alisema, mmiliki huyo hakuwa na kosa, kwa sababu maziwa hayo yaliingizwa kemikali hiyo kiwandani nchini China, ikiwa ni mbinu ya kuongeza virubitisho vya Protini kutokana na tabia ya wafugaji wa nchi hiyo kuweka maji katika maziwa baada ya kuyakamua.
“Kama mmiliki atataka kudai fidia kutoka kwa kampuni iliyotengeneza maziwa haya, sisi tunaweza kutoa ushirikiano kwa kuthibitisha kuwa tuliyaharibu kwa kuwa yalikuwa na kemikali yenye madhara kwa afya ya binadamu,” alisema Wigenge.
Hata hivyo Wigenge alithibitisha kuwa, mmiliki wa maziwa hayo hana kosa kwa sababu kemikali ya ‘melamine’ ambayo inasababisha ugonjwa wa figo hasa kwa watoto haikuwa kigezo cha kupima ubora wa maziwa hapo awali.
Uteketezaji huo ulifanyika chini ushuhuda wa maafisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), TFDA, Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC), polisi, na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
Afisa Mkuu wa Forodha kutoka TRA Tmeke Peles Mwaipopo alisema, wao kazi yao ni kushuhudia tu na kuthibitisha kwamba uteketezaji umefanyika na si vyenginevyo.
“Baada ya hapa tutaandika ripoti kwa ajili ya kuiwasilisha kwa wakuu wetu kama kumbukumbu ili siku yoyote mmiliki akilalamika tunatoa ushahidi kuwa kitendo hicho kilifanyika,” alisema Mwaipopo.
Kwa mujibu wa sheria anayekamatwa na bidhaa bandia hupaswa kugharamia hasara yote ya uteketezaji wa bidhaa hiyo ikiwa ni pamoja na usafiri, posho za maofisa na wabebaji.
Mahakama ya Ardhi K,ndoni yamwokoa mjane Kiluvya
Salim Said na Ellen Manyangu
SIKU moja baada ya mjane Shamsa Nassor kuhamishwa nyumbani mwake kikatili, Kiluvya jijini Dar es Salaam, Mahakama ya Ardhi Wilaya ya Kinondoni imeamrisha mama huyo arudishwe nyumbani mwake.
Aidha, Kampuni ya Namic Auction Mart ilipewa kazi ya kumrudisha nyumbani mwake mjane huyo chini ya usimamizi mkali wa Polisi kutoka Wilaya ya kipolisi Kimara.
Amri hiyo, nakala tunayo, ilitolewa jana na kusainiwa na Mwenyekiti wa Mahakama ya Ardhi Kinondini Joseph Kaale na kukabidhiwa kwa kampuni ya Namic kwa ajili ya utekelezaji.
“Mahakama imeamrisha kwamba muombaji katika ombi hili arudishwe nyumbani mwake ambamo alitolewa bila ya sababu za msingi, haraka iwezekanavyo” alisema Kaale katika nakala ya amri hiyo.
Safari ya kwenda kumrudisha nyumbani mwake mjane huyo, ilianzia Kinondoni kupitia kituo cha polisi Mbezi, ofisi ya serikali ya Mtaa Kiluvya na Mjumbe wa Shina la eneo hilo.
Ilichukua takriban masaa mawili hadi juhudi za Mkurugenzi Mtendaji wa Namic Michael Mwenda kufanikiwa kuopata asakari wawili kwa ajili ya kulinda amani na usalama wakati wa urudishwaji wa mjane huyo.
Aidha baada ya kufika eneo la tukio, askari wa Kampuni ya Ulinzi ya General na mwakilishi wa Abdallah Malik aliyejitambulisha kwa jina la Abdu Mkata waligoma kufungua lango la kuingilia licha ya askari waliotumwa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kimara (OCD) N. Ndaki.
“Mimi sipo tayari kufungua nipo tayari hata kufa, kufungwa au kukamatwa na polisi. Subirini niwasiliane na Malik au turudini kwa OCD” alisema Mkata.
“Usikubali, usikubali bora tukalale ndani kuliko kumwachia huyu mama aingie humu ndani kwa kuwa Malik hatatuelewa,” alisistiza kumueleza Mkuu wa General Guard Haroub Mbelwa.
Hata hivyo, Mwenda aliamua kuwasiliana na OCD na kumueleza kwamba amri iliyotumika kumtoa mama huyo haikufuata utaratibu na kwamba amri kumrudisha ni halali na kwa hiyo atakaekaidi atashitakiwa.
Baada ya majibizano marefu kati ya askari hao na Viongozi wa Namic hatimae waliachia ngazi bila ya kutoa funguo na wao kuamua kurudi kituo cha polisi Mbezi kwa ajili ya kumuona OCD kwa majadiliano zaidi.
Baada ya wao kuondoka uamuzi wa kuvunja kufuli na minyororo katika milango ya kuingia ndani ya eneo na nyumba ya mjane huyo ulipitishwa na kufanywa na viongozi wa Namic.
Kwa upande wake Shamsa alilishukuru sana gazeti la Mwananchi kwa kuandika habari hiyo pamoja na mahakama ya ardhi kwa kumpatia amri ya kurudishwa ndani ya nyumba yake.
“Nimefurahi sana, pia natoa shukurani zangu kwa gazeti la Mwananchi maana leo (jana) tangu asubuhi napokea simu za pole kutoka na habari hiyo. Lakini nawaomba muendele kufuatilia, serikali nayo ifuatilie ili ijue ukweli wa kesi,” alisema Shamsa na kuongeza:
“Lakini hofu yangu ni usalama na amani yangu kwa kuwa tukio hili limenitisha sana na chochote kinaweza kikanitokea kutokana na vitisho nilivyopewa na shemeji yangu Malik.”
Hadi Mwenanchi inaondoka eneo la tukio jana majira ya saa 11:05 OCD Ndaki alipiga simu na kumtaka Shamsa kuripoti Polisi Kimara kwa taratibu zaidi za kipolisi.
Shamsa alihamishwa nyumbani mwake kwa nguvu juzi na kampuni ya Yono Auction Mart, kitendo ambacho kilimsababishia hasara na majeraha mwilini.
SIKU moja baada ya mjane Shamsa Nassor kuhamishwa nyumbani mwake kikatili, Kiluvya jijini Dar es Salaam, Mahakama ya Ardhi Wilaya ya Kinondoni imeamrisha mama huyo arudishwe nyumbani mwake.
Aidha, Kampuni ya Namic Auction Mart ilipewa kazi ya kumrudisha nyumbani mwake mjane huyo chini ya usimamizi mkali wa Polisi kutoka Wilaya ya kipolisi Kimara.
Amri hiyo, nakala tunayo, ilitolewa jana na kusainiwa na Mwenyekiti wa Mahakama ya Ardhi Kinondini Joseph Kaale na kukabidhiwa kwa kampuni ya Namic kwa ajili ya utekelezaji.
“Mahakama imeamrisha kwamba muombaji katika ombi hili arudishwe nyumbani mwake ambamo alitolewa bila ya sababu za msingi, haraka iwezekanavyo” alisema Kaale katika nakala ya amri hiyo.
Safari ya kwenda kumrudisha nyumbani mwake mjane huyo, ilianzia Kinondoni kupitia kituo cha polisi Mbezi, ofisi ya serikali ya Mtaa Kiluvya na Mjumbe wa Shina la eneo hilo.
Ilichukua takriban masaa mawili hadi juhudi za Mkurugenzi Mtendaji wa Namic Michael Mwenda kufanikiwa kuopata asakari wawili kwa ajili ya kulinda amani na usalama wakati wa urudishwaji wa mjane huyo.
Aidha baada ya kufika eneo la tukio, askari wa Kampuni ya Ulinzi ya General na mwakilishi wa Abdallah Malik aliyejitambulisha kwa jina la Abdu Mkata waligoma kufungua lango la kuingilia licha ya askari waliotumwa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kimara (OCD) N. Ndaki.
“Mimi sipo tayari kufungua nipo tayari hata kufa, kufungwa au kukamatwa na polisi. Subirini niwasiliane na Malik au turudini kwa OCD” alisema Mkata.
“Usikubali, usikubali bora tukalale ndani kuliko kumwachia huyu mama aingie humu ndani kwa kuwa Malik hatatuelewa,” alisistiza kumueleza Mkuu wa General Guard Haroub Mbelwa.
Hata hivyo, Mwenda aliamua kuwasiliana na OCD na kumueleza kwamba amri iliyotumika kumtoa mama huyo haikufuata utaratibu na kwamba amri kumrudisha ni halali na kwa hiyo atakaekaidi atashitakiwa.
Baada ya majibizano marefu kati ya askari hao na Viongozi wa Namic hatimae waliachia ngazi bila ya kutoa funguo na wao kuamua kurudi kituo cha polisi Mbezi kwa ajili ya kumuona OCD kwa majadiliano zaidi.
Baada ya wao kuondoka uamuzi wa kuvunja kufuli na minyororo katika milango ya kuingia ndani ya eneo na nyumba ya mjane huyo ulipitishwa na kufanywa na viongozi wa Namic.
Kwa upande wake Shamsa alilishukuru sana gazeti la Mwananchi kwa kuandika habari hiyo pamoja na mahakama ya ardhi kwa kumpatia amri ya kurudishwa ndani ya nyumba yake.
“Nimefurahi sana, pia natoa shukurani zangu kwa gazeti la Mwananchi maana leo (jana) tangu asubuhi napokea simu za pole kutoka na habari hiyo. Lakini nawaomba muendele kufuatilia, serikali nayo ifuatilie ili ijue ukweli wa kesi,” alisema Shamsa na kuongeza:
“Lakini hofu yangu ni usalama na amani yangu kwa kuwa tukio hili limenitisha sana na chochote kinaweza kikanitokea kutokana na vitisho nilivyopewa na shemeji yangu Malik.”
Hadi Mwenanchi inaondoka eneo la tukio jana majira ya saa 11:05 OCD Ndaki alipiga simu na kumtaka Shamsa kuripoti Polisi Kimara kwa taratibu zaidi za kipolisi.
Shamsa alihamishwa nyumbani mwake kwa nguvu juzi na kampuni ya Yono Auction Mart, kitendo ambacho kilimsababishia hasara na majeraha mwilini.
Mjane ahamishwa 'kinyama Kiluvya
Salim Said
KAMPUNI ya Yono Auction Mart imeihamisha kwa nguvu familia ya Shamsa Nassor katika nyumba yake iliyopo Kiluvya Mtaa wa Gogoni, Kinondoni jijini Dar es Salaam na kasababisha hasara ya mali na kujeruhi.
Nymba hiyo ambayo ni mali ya marehemu mume wa Shamsa aitwae Salim Aklan, ilivamiwa jana na kampuni hiyo kwa madai kuwa wamepewa amri na mahakama ya mwanzo Magomeni ya kuwahamisha huku kukiwa hakuna notisi.
Akizungumza na Mwananchi mara baada ya tukio hilo lililotokea mapema asubuhi ya jana Shamsa alisema, kundi la watu zaidi ya 30 walivamia nyumba yake na kumtoa kwa nguvu yeye na watoto wake na kumsababishia hasara ya mali na majeraha ya mwili.
“Walikuja na mjumbe wa shina, wakaniambia kuwa wametumwa na mahakama, nikawaomba kabla ya kuanza kunitoa tukae chini kwanza kwa sababu wao wana nyaraka na mimi ninazo, halafu sina notisi, ndipo waliponisukuma na kuanza kuvunja vitu na kuviburuza nje,” alisimulia Shamsa huku akibubujikwa na machozi na kuongeza:
“Nilipoona hivyo nikachukua gari ili niende polisi kituo cha Kiluvya Gogoni kutoa taarifa na wakati gari liko katika mwendo wakaniwekea mtungi uliokuwa na bustani kwenye tairi na gari ilikakosa mwelekeo na kugonga mti na baadae kupinduka huku ndani nikiwa na mwanangu wa msichana.”
Alisema kutokana na ajali hiyo, wamepata majeraha yeye na mwanawe ambapo baadae alipiga simu kituo cha polisi Ostabey ambapo askari wa usalama barabarani walifika katika eneo hilo kupima ajali hiyo.
“Dhabu zangu zote zenye thamani ya 15 milioni sizioni, wameniibia saa ya aina ya Rado, fedha taslimu 5.9 milioni, wamenivunjia vitu vya jikoni, vitu vya samani na vitabu na madaftari ya shule ya watoto wangu,” alilalamika Shamsa.
Shamsa alidai kuwa, tukio hilo lilishinikizwa na shemgi yake aitwae Abdallah Malik kwa madi kuwa anataka kurithi mali hiyo kwa nguvu.
Alipoulizwa Malik kuhusiana na tukio hilo alijibu kwa jeuri na kutoa vitisho kwa mwandishi.
“Ahaa! Kama ni mwandishi andika unachojua na ukiandika vibaya likikuripukia utajijua, maana mimi nitakuchukulia hatua na wala sitokuachia,” alisema Malik na kuongeza:
“Andika tu wewe kama huyo unayemsikiliza (Shamsa) ni Bibi yako lakini litakalokufika utajua mwenyewe eneo hili lipo chini ya mahakama. Askari asiingie mtu humu, sawa.”
Mara baada ya kumalizika kazi ya kumuhamisha mama huyo, Malik alileta askari wa Kampuni ya Ulinzi ya General (General Guard) na kuwapa kazi hiyo licha ya kudai kuwa eneo hilo lipo chini ya mahakama ya Mwanzo ya Magomeni jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Peter Yohana alithibitisha kuletwa hapo na Malik kwa kazi moja tu ya kuhakikisha kuwa haingii mtu ndani ya eneo hilo hata mama huyo aliyehamishwa au mtoto wake.
“Sisi tumeletwa leo (jana) asubuhi na Malik na ametutaka asiingie mtu na hata wewe kama si mwandishi usingeingia humu. Ametuthibitishia kuwa eneo hili lipo chini ya mahakama na vitu vya yule mama vyote vipo nje ya geti kule,” alisema Yohana.
Kwa upande wake mjumbe wa shina la Gogoni Kiluvya mama Mramba alisema yeye hakuwa na taarifa ya kazi hiyo na alikwenda kugongewa asubuhi wakati akichoma vitumbua vyake ili kuwasindikiza wafanyakazi wa Yono.
“Mimi nilipoona vuru nikakimbia polisi na nilipofika sijakuta hata askari mmoja nikaamua kwenda kuendelea kuchoma vitumbua vyangu kwa kuwa ndio kazi ninayoitegemea na biashara ni asubuhi,” alisema mama Mramba.
Hata hivyo Polisi Wilaya ya kipolisi Kimara ilisema haina taarifa za hamishahamisha hiyo na kwamba kitaratibu shughuli kama hizo hutakiwa kusimamiwa na polisi kwa ajili ya amani na uslama.
“Mimi sina taarifa ya tukio hilo wala sina taarifa ya amri ya mahakama kuhusu kuhamishwa kwa watu hao lakini wewe nenda mahakamani ili ujue kama ‘order’ amri ya mahakama ilitoka au la,” alisema Mkuu wa kituo cha polisi Mbezi J.K Ndaki.
KAMPUNI ya Yono Auction Mart imeihamisha kwa nguvu familia ya Shamsa Nassor katika nyumba yake iliyopo Kiluvya Mtaa wa Gogoni, Kinondoni jijini Dar es Salaam na kasababisha hasara ya mali na kujeruhi.
Nymba hiyo ambayo ni mali ya marehemu mume wa Shamsa aitwae Salim Aklan, ilivamiwa jana na kampuni hiyo kwa madai kuwa wamepewa amri na mahakama ya mwanzo Magomeni ya kuwahamisha huku kukiwa hakuna notisi.
Akizungumza na Mwananchi mara baada ya tukio hilo lililotokea mapema asubuhi ya jana Shamsa alisema, kundi la watu zaidi ya 30 walivamia nyumba yake na kumtoa kwa nguvu yeye na watoto wake na kumsababishia hasara ya mali na majeraha ya mwili.
“Walikuja na mjumbe wa shina, wakaniambia kuwa wametumwa na mahakama, nikawaomba kabla ya kuanza kunitoa tukae chini kwanza kwa sababu wao wana nyaraka na mimi ninazo, halafu sina notisi, ndipo waliponisukuma na kuanza kuvunja vitu na kuviburuza nje,” alisimulia Shamsa huku akibubujikwa na machozi na kuongeza:
“Nilipoona hivyo nikachukua gari ili niende polisi kituo cha Kiluvya Gogoni kutoa taarifa na wakati gari liko katika mwendo wakaniwekea mtungi uliokuwa na bustani kwenye tairi na gari ilikakosa mwelekeo na kugonga mti na baadae kupinduka huku ndani nikiwa na mwanangu wa msichana.”
Alisema kutokana na ajali hiyo, wamepata majeraha yeye na mwanawe ambapo baadae alipiga simu kituo cha polisi Ostabey ambapo askari wa usalama barabarani walifika katika eneo hilo kupima ajali hiyo.
“Dhabu zangu zote zenye thamani ya 15 milioni sizioni, wameniibia saa ya aina ya Rado, fedha taslimu 5.9 milioni, wamenivunjia vitu vya jikoni, vitu vya samani na vitabu na madaftari ya shule ya watoto wangu,” alilalamika Shamsa.
Shamsa alidai kuwa, tukio hilo lilishinikizwa na shemgi yake aitwae Abdallah Malik kwa madi kuwa anataka kurithi mali hiyo kwa nguvu.
Alipoulizwa Malik kuhusiana na tukio hilo alijibu kwa jeuri na kutoa vitisho kwa mwandishi.
“Ahaa! Kama ni mwandishi andika unachojua na ukiandika vibaya likikuripukia utajijua, maana mimi nitakuchukulia hatua na wala sitokuachia,” alisema Malik na kuongeza:
“Andika tu wewe kama huyo unayemsikiliza (Shamsa) ni Bibi yako lakini litakalokufika utajua mwenyewe eneo hili lipo chini ya mahakama. Askari asiingie mtu humu, sawa.”
Mara baada ya kumalizika kazi ya kumuhamisha mama huyo, Malik alileta askari wa Kampuni ya Ulinzi ya General (General Guard) na kuwapa kazi hiyo licha ya kudai kuwa eneo hilo lipo chini ya mahakama ya Mwanzo ya Magomeni jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Peter Yohana alithibitisha kuletwa hapo na Malik kwa kazi moja tu ya kuhakikisha kuwa haingii mtu ndani ya eneo hilo hata mama huyo aliyehamishwa au mtoto wake.
“Sisi tumeletwa leo (jana) asubuhi na Malik na ametutaka asiingie mtu na hata wewe kama si mwandishi usingeingia humu. Ametuthibitishia kuwa eneo hili lipo chini ya mahakama na vitu vya yule mama vyote vipo nje ya geti kule,” alisema Yohana.
Kwa upande wake mjumbe wa shina la Gogoni Kiluvya mama Mramba alisema yeye hakuwa na taarifa ya kazi hiyo na alikwenda kugongewa asubuhi wakati akichoma vitumbua vyake ili kuwasindikiza wafanyakazi wa Yono.
“Mimi nilipoona vuru nikakimbia polisi na nilipofika sijakuta hata askari mmoja nikaamua kwenda kuendelea kuchoma vitumbua vyangu kwa kuwa ndio kazi ninayoitegemea na biashara ni asubuhi,” alisema mama Mramba.
Hata hivyo Polisi Wilaya ya kipolisi Kimara ilisema haina taarifa za hamishahamisha hiyo na kwamba kitaratibu shughuli kama hizo hutakiwa kusimamiwa na polisi kwa ajili ya amani na uslama.
“Mimi sina taarifa ya tukio hilo wala sina taarifa ya amri ya mahakama kuhusu kuhamishwa kwa watu hao lakini wewe nenda mahakamani ili ujue kama ‘order’ amri ya mahakama ilitoka au la,” alisema Mkuu wa kituo cha polisi Mbezi J.K Ndaki.
Monday, May 25, 2009
DC akiri vyama vya upinzani kuimarika
Salim Said
MKUU wa Wilaya ya Makete mkoani Iringa, Hawa Ng’humbi amewataka viongozi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kujipanga vizuri, ili kuhakikisha wanapata ushindi mkubwa katika chaguzi za serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu, kwa kuwa upinzani umekuwa mkubwa sasa.
Akizungumza mara baada ya kutawazwa kuwa Mlezi Mkuu wa Jumuiya hiyo, kata ya Mabibo jijini Dar es Salaam jana, Ng’humbi alisema matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu ndiyo utakaotoa taswira ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 nchini kote.
“Tujipange vizuri katika uchaguzi za serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka, ili kujenga mazingira ya CCM kutwaa tena dola mwakani katika uchaguzi mkuu na pia kuzuia jimbo la Ubungo lisichukuliwe na upinzani” alisema Ng’humbi.
Ng’humbi ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro kabla ya kuhamishiwa Makete, alisema upinzani kwa sasa ni mkubwa na kila chama cha upinzani kinajaribu kujiimarisha ili kuhakikisha kwamba kinashika dola.
“Ndugu zangu mimi ni mchapa kazi mzuri, nitahakikisha kwamba tunashirikiana katika kuhakikisha tunashinda uchaguzi wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu katika kata yetu na taifa kwa ujumla,” aliahidi Ng’humbi.
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo kata ya Mabibo Bononi Mlowe aliwataka, wanajumuiya kutokubali kurubuniwa kwa fedha na kuchaguwa wafadhili badala ya viongozi.
Alisema, watanzania wamekuwa wakichagua viongozi kwa miaka mingi lakini viongozi hao hawawajali wapiga kura wao na badala yake wanaamua kutajirisha matumbo yao.
Alisema katika awamu yake, atahakikisha kuwa anawashawishi viongozi wa jumuiya hiyo kutafuta kazi nyingine kwa ajili ya kupata fedha na kuifanya kazi ya uongozi kuwa huduma badala ya biashara.
“Wakipata kazi nyingine ya kutafutia fedha watakuwa waaminifu katika mali za chama na ada za watoto wetu, hii itatusaidia kunyanyua maendeleo na kuimarisha Chama chetu,” alisema Mlowe.
MKUU wa Wilaya ya Makete mkoani Iringa, Hawa Ng’humbi amewataka viongozi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kujipanga vizuri, ili kuhakikisha wanapata ushindi mkubwa katika chaguzi za serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu, kwa kuwa upinzani umekuwa mkubwa sasa.
Akizungumza mara baada ya kutawazwa kuwa Mlezi Mkuu wa Jumuiya hiyo, kata ya Mabibo jijini Dar es Salaam jana, Ng’humbi alisema matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu ndiyo utakaotoa taswira ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 nchini kote.
“Tujipange vizuri katika uchaguzi za serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka, ili kujenga mazingira ya CCM kutwaa tena dola mwakani katika uchaguzi mkuu na pia kuzuia jimbo la Ubungo lisichukuliwe na upinzani” alisema Ng’humbi.
Ng’humbi ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro kabla ya kuhamishiwa Makete, alisema upinzani kwa sasa ni mkubwa na kila chama cha upinzani kinajaribu kujiimarisha ili kuhakikisha kwamba kinashika dola.
“Ndugu zangu mimi ni mchapa kazi mzuri, nitahakikisha kwamba tunashirikiana katika kuhakikisha tunashinda uchaguzi wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu katika kata yetu na taifa kwa ujumla,” aliahidi Ng’humbi.
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo kata ya Mabibo Bononi Mlowe aliwataka, wanajumuiya kutokubali kurubuniwa kwa fedha na kuchaguwa wafadhili badala ya viongozi.
Alisema, watanzania wamekuwa wakichagua viongozi kwa miaka mingi lakini viongozi hao hawawajali wapiga kura wao na badala yake wanaamua kutajirisha matumbo yao.
Alisema katika awamu yake, atahakikisha kuwa anawashawishi viongozi wa jumuiya hiyo kutafuta kazi nyingine kwa ajili ya kupata fedha na kuifanya kazi ya uongozi kuwa huduma badala ya biashara.
“Wakipata kazi nyingine ya kutafutia fedha watakuwa waaminifu katika mali za chama na ada za watoto wetu, hii itatusaidia kunyanyua maendeleo na kuimarisha Chama chetu,” alisema Mlowe.
Katibu Mkuu Bakwata ashushwa madaraka
Mwandishi Wetu
MUFTI wa Tanzania sheikh Issa Shaban Simba ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislaam Tanzania (Bakwata) ustadhi Ally Juma Mzee na kumteua sheikh Suleiman Said kukaimu nafasi hiyo.
Mabadiliko hayo yamefanyika kimya kimya bila ya kutangazwa kabla ya Mufti Simba kusafiri kuelekea nchini Uturuki, ambako ameenda kufanya uchunguzi wa kawaida wa afya yake.
Habari ambazo Mwananchi imezipata zinasema kwamba, Mufti amechukua hatua hiyo kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa mali za Bakwata zinazomkabili aliyekuwa Kaibu Mkuu wake ustadhi Mzee.
Utenguzi huo unafanyika wakati uchaguzi mkuu wa baraza hilo unaendelea kufanyika katika ngazi mbalimbali kuanzia Msikiti hadi taifa.
Kabla ya Mufti kufanya utenguzi huo Masheikh na waumini mkoani Arusha, walishampinga ustadhi Mzee, kuendelea kuongoza baraza hilo kwa madai kuwa hana sifa.
Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Arusha, Mahmoud Salum, alisema katika tamko lao mara baada ya kikao kilichofanyika katika Msikiti wa Ngarenaro Arusha kuwa, kwa kauli moja wanaunga mkono mapendekezo na uamuzi wa Halmashauri ya Ulamaa Mkoa wa Arusha kumfukuza ustadhi Mzee.
''Tuhuma zilizomkabili ustadhi Mzee ni nzito, hivyo haturidhishwi na utendaji wake na pia kupewa jukumu kubwa la Katibu Mkuu wa Bakwata kwani, hana sifa stahiki,'' alisema Sheikh Salum.
Aidha, Bakwata Mkoa huo ilitoa onyo kali Mei 21 mwaka huu kwa ustadhi Mzee, ambaye sasa ni katibu wa Bakwata mkoa kwa madai anawarubuni waumini ili kuibua upya mgogoro wa kidini ambao walishaupatia ufumbuzi.
Aidha Mwananchi imebaini kuwa ustadhi Mzee anakabiliwa na tuhuma za kutumia mapato ya msikiti huo na kusababisha hasara kwa baraza.
Pamoja na uamuzi huo mzito wa Mufti bado baadhi wa maafisa wa ngazi za juu wa Bakwata hawajaridhika na wanasema licha ya Mufti kutengua uteuzi wa ustadhi Mzee na kumteua kuwa Katibu wa Mkoa wa Arusha wa baraza hilo, ni kwamba bado hajatatua tatizo.
“Tatizo la mwenzetu ni kubwa kwa sababu anakabiliwa na tuhuma za ufisadi lakini Mufti analichukulia suala kijujuu jambo ambalo ni hatari na linaweza kuligawa Bakwata,” alisema Afisa mmoja na kuongeza:
“Kwa nini waumini ambao unawaongoza wakukatae? Lazima kutakuwa na matatizo tu unachaguliwa kuwa katibu wa Mkoa wa Bakwata halafu unafukuza viongozi na kuchagua unaoona watafanyakazi kukulinda unapofanya maovu yako. Hata ukatibu wa msikiti unautaka wewe.”
“Mufti ni bora akaunda tume huru kwanza kuchunguza tuhuma za ustadhi mzee na siyo kulichukulia suala hili zito juu juu,” alisema.
Uchunguzi unaonesha kuwa Msikiti Mkuu wa mkoa wa Arusha una vitega uchumi vingi vikiwamo milango mingi ya maduka ambayo inakodishwa kwa wafanyabiashara na kuliingizia mapato Baraza.
“Sio siri bwana, mwenzetu anakabiliwa pia na tuhuma za kuuza viwanja vya Wakfu vya Bakwata, lazima watu wakukatae kwa hali hiyo,” alisema Afisa mwengine na kusisitiza:
“Mufti bado hajatatua tatizo kwa sababu ustadhi Mzee anakabiliwa na tuhuma za ufisadi Arusha na waumini wa mkoa huo wameshamkataa, halafu unamrudisha tena kuwa katibu wa mkoa, haingii akilini.”
MUFTI wa Tanzania sheikh Issa Shaban Simba ametengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislaam Tanzania (Bakwata) ustadhi Ally Juma Mzee na kumteua sheikh Suleiman Said kukaimu nafasi hiyo.
Mabadiliko hayo yamefanyika kimya kimya bila ya kutangazwa kabla ya Mufti Simba kusafiri kuelekea nchini Uturuki, ambako ameenda kufanya uchunguzi wa kawaida wa afya yake.
Habari ambazo Mwananchi imezipata zinasema kwamba, Mufti amechukua hatua hiyo kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa mali za Bakwata zinazomkabili aliyekuwa Kaibu Mkuu wake ustadhi Mzee.
Utenguzi huo unafanyika wakati uchaguzi mkuu wa baraza hilo unaendelea kufanyika katika ngazi mbalimbali kuanzia Msikiti hadi taifa.
Kabla ya Mufti kufanya utenguzi huo Masheikh na waumini mkoani Arusha, walishampinga ustadhi Mzee, kuendelea kuongoza baraza hilo kwa madai kuwa hana sifa.
Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Arusha, Mahmoud Salum, alisema katika tamko lao mara baada ya kikao kilichofanyika katika Msikiti wa Ngarenaro Arusha kuwa, kwa kauli moja wanaunga mkono mapendekezo na uamuzi wa Halmashauri ya Ulamaa Mkoa wa Arusha kumfukuza ustadhi Mzee.
''Tuhuma zilizomkabili ustadhi Mzee ni nzito, hivyo haturidhishwi na utendaji wake na pia kupewa jukumu kubwa la Katibu Mkuu wa Bakwata kwani, hana sifa stahiki,'' alisema Sheikh Salum.
Aidha, Bakwata Mkoa huo ilitoa onyo kali Mei 21 mwaka huu kwa ustadhi Mzee, ambaye sasa ni katibu wa Bakwata mkoa kwa madai anawarubuni waumini ili kuibua upya mgogoro wa kidini ambao walishaupatia ufumbuzi.
Aidha Mwananchi imebaini kuwa ustadhi Mzee anakabiliwa na tuhuma za kutumia mapato ya msikiti huo na kusababisha hasara kwa baraza.
Pamoja na uamuzi huo mzito wa Mufti bado baadhi wa maafisa wa ngazi za juu wa Bakwata hawajaridhika na wanasema licha ya Mufti kutengua uteuzi wa ustadhi Mzee na kumteua kuwa Katibu wa Mkoa wa Arusha wa baraza hilo, ni kwamba bado hajatatua tatizo.
“Tatizo la mwenzetu ni kubwa kwa sababu anakabiliwa na tuhuma za ufisadi lakini Mufti analichukulia suala kijujuu jambo ambalo ni hatari na linaweza kuligawa Bakwata,” alisema Afisa mmoja na kuongeza:
“Kwa nini waumini ambao unawaongoza wakukatae? Lazima kutakuwa na matatizo tu unachaguliwa kuwa katibu wa Mkoa wa Bakwata halafu unafukuza viongozi na kuchagua unaoona watafanyakazi kukulinda unapofanya maovu yako. Hata ukatibu wa msikiti unautaka wewe.”
“Mufti ni bora akaunda tume huru kwanza kuchunguza tuhuma za ustadhi mzee na siyo kulichukulia suala hili zito juu juu,” alisema.
Uchunguzi unaonesha kuwa Msikiti Mkuu wa mkoa wa Arusha una vitega uchumi vingi vikiwamo milango mingi ya maduka ambayo inakodishwa kwa wafanyabiashara na kuliingizia mapato Baraza.
“Sio siri bwana, mwenzetu anakabiliwa pia na tuhuma za kuuza viwanja vya Wakfu vya Bakwata, lazima watu wakukatae kwa hali hiyo,” alisema Afisa mwengine na kusisitiza:
“Mufti bado hajatatua tatizo kwa sababu ustadhi Mzee anakabiliwa na tuhuma za ufisadi Arusha na waumini wa mkoa huo wameshamkataa, halafu unamrudisha tena kuwa katibu wa mkoa, haingii akilini.”
FemAct dola imetekwa na mafisadi
Salim Sai
MTANDAO wa asasi za kiraia nchini, FemaAct, jana umeeleza kuwa dola ya Tanzania imetekwa na kundi la mafisadi.
Tamko hilo, lilosainiwa na viongozi kutoka asasi 14 za kiraia na lililowakilisha asasi 50 wanachama wa mtandao huo, lilisomwa na msemaji wa FemAct, Buberwa Kaiza mbele ya waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) yaliyo Mabibo jijini Dar es Salaam.
Kaiza, ambaye anatoka taasisi ya Fordia, alisema wameamua kutoa tamko hilo kali kwa kuwa wameguswa na kuchukizwa na mwenendo wa kushughulikia matukio ya ufisadi na ukwapuaji wa mali za umma nchini, ambao unaendelea kushamiri nchini.
“Kushamiri kwa ufisadi kunabainisha jambo moja kubwa na lenye kutia shaka. Ni kwamba dola ya Tanzania tayari imetekwa na mafisadi,” alisema Bubelwa.
“Tumetathmini kwa muda mrefu na kubaini kuwa kushamiri kwa ufisadi nchini kunasababishwa na kutekwa kwa dola, sera ya uchumi wa soko holela, kutokuwepo kwa misingi endelevu ya utawala bora, ulafi wa madaraka na ubinafsi wa viongozi.”
Pia alisema kitendo cha wananchi kutodai uwajibikaji; kuendelea kutumika kwa baadhi ya sheria za kikoloni; katiba iliyopitwa na wakati na serikali kulea kundi la ‘wateule’ wasioguswa na sheria, ni ushahidi tosha wa kutekwa nyara kwa dola ya Tanzania na mafisadi wachache.
“Ushahidi mwingine wa dola kutekwa na mafisadi ni serikali na bunge kutumikia maslahi ya watu wachache; kutawala kwa rushwa kubwa; kulegalega kwa dola katika kuwachukulia hatua za haraka za kinidhamu na kisheria watuhumiwa wa ufisadi; kucheleweshwa kwa kesi za wakubwa za tuhuma za ufisadi na sheria kutumikia wachache,” alisema Bubelwa.
Bubelwa alifafanua kuwa kushamiri kwa ufisadi na sera za uchumi wa soko holela nchini kumesababisha madhara makubwa kwa Watanzania masikini.
Alisema madhara hayo pia yanasababishwa na hali ya serikali kukosa msimamo thabiti katika kutetea maslahi ya taifa.
Alisema madhara mengine ni kuyumba kwa uchumi wa taifa; utumishi wa umma kugeuzwa daraja la kujipatia utajiri; mgawanyo mbovu wa mapato ambao umesababisha pengo kubwa la kipato; kuongezeka kwa ufukara; kuporomoka kwa ubora wa huduma za jamii na ukosefu wa ajira.
Awali Bubelwa alianisha baadhi ya kashfa za ufisadi zilizotikisa nchi kuwa ni pamoja na ujenzi wa jengo la minara pacha ya Benki Kuu (BoT), wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), mikataba ya madini ya Buzwagi, Kiwira, Kagoda, Tangold, Meremeta ununuzi wa vifaa vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kufilisika kwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), ununuzi wa rada na ndege ya Rais.
MTANDAO wa asasi za kiraia nchini, FemaAct, jana umeeleza kuwa dola ya Tanzania imetekwa na kundi la mafisadi.
Tamko hilo, lilosainiwa na viongozi kutoka asasi 14 za kiraia na lililowakilisha asasi 50 wanachama wa mtandao huo, lilisomwa na msemaji wa FemAct, Buberwa Kaiza mbele ya waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) yaliyo Mabibo jijini Dar es Salaam.
Kaiza, ambaye anatoka taasisi ya Fordia, alisema wameamua kutoa tamko hilo kali kwa kuwa wameguswa na kuchukizwa na mwenendo wa kushughulikia matukio ya ufisadi na ukwapuaji wa mali za umma nchini, ambao unaendelea kushamiri nchini.
“Kushamiri kwa ufisadi kunabainisha jambo moja kubwa na lenye kutia shaka. Ni kwamba dola ya Tanzania tayari imetekwa na mafisadi,” alisema Bubelwa.
“Tumetathmini kwa muda mrefu na kubaini kuwa kushamiri kwa ufisadi nchini kunasababishwa na kutekwa kwa dola, sera ya uchumi wa soko holela, kutokuwepo kwa misingi endelevu ya utawala bora, ulafi wa madaraka na ubinafsi wa viongozi.”
Pia alisema kitendo cha wananchi kutodai uwajibikaji; kuendelea kutumika kwa baadhi ya sheria za kikoloni; katiba iliyopitwa na wakati na serikali kulea kundi la ‘wateule’ wasioguswa na sheria, ni ushahidi tosha wa kutekwa nyara kwa dola ya Tanzania na mafisadi wachache.
“Ushahidi mwingine wa dola kutekwa na mafisadi ni serikali na bunge kutumikia maslahi ya watu wachache; kutawala kwa rushwa kubwa; kulegalega kwa dola katika kuwachukulia hatua za haraka za kinidhamu na kisheria watuhumiwa wa ufisadi; kucheleweshwa kwa kesi za wakubwa za tuhuma za ufisadi na sheria kutumikia wachache,” alisema Bubelwa.
Bubelwa alifafanua kuwa kushamiri kwa ufisadi na sera za uchumi wa soko holela nchini kumesababisha madhara makubwa kwa Watanzania masikini.
Alisema madhara hayo pia yanasababishwa na hali ya serikali kukosa msimamo thabiti katika kutetea maslahi ya taifa.
Alisema madhara mengine ni kuyumba kwa uchumi wa taifa; utumishi wa umma kugeuzwa daraja la kujipatia utajiri; mgawanyo mbovu wa mapato ambao umesababisha pengo kubwa la kipato; kuongezeka kwa ufukara; kuporomoka kwa ubora wa huduma za jamii na ukosefu wa ajira.
Awali Bubelwa alianisha baadhi ya kashfa za ufisadi zilizotikisa nchi kuwa ni pamoja na ujenzi wa jengo la minara pacha ya Benki Kuu (BoT), wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), mikataba ya madini ya Buzwagi, Kiwira, Kagoda, Tangold, Meremeta ununuzi wa vifaa vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kufilisika kwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), ununuzi wa rada na ndege ya Rais.
Subscribe to:
Posts (Atom)