MARASHI

PLAN YOUR WORK AND WORK ON YOUR PLAN BUT, WHEN YOU FAIL TO PLAN, YOU PLAN TO FAIL

Sunday, June 21, 2009

Lwakatare awashukia viongozi wa CUF

Salim Said
ALIYEKUWA Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Tanzania bara, Wilfred Lwakatare amewashushia tuhuma nzito baadhi ya viongozi wa wa Chama hicho akidai kuwa jina lake liliachwa kwenye uteuzi wa kutetea nafasi yake kwa fitina na majungu yaliyojaa CUF.

Alisema, hiyo ndiyo sababu kuu iliyomfanya aandike barua ya kujiuzulu nafasi zote katika chama hicho na kubaki kama mwanachama wa kawaida.

Rwakatare alitoa shutuma hizo kupitia mtandao wa Bidii, ambapo alidai maelezo hayo ndiyo aliyoyawasilisha katika kikao cha Baraza Kuu la Taifa la CUF kilichofanyika tarehe 09/06/2009.

Alisema licha ya chama hicho kuyumbishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), pia kuna baadhi ya wanachama na viongozi wenye tabia mbaya ya majungu na fitina dhidi ya wenzao.

Akieleza alisema maelezo ya Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba kwamba uteuzi aliofanya katika nafasi hiyo bara na Zanzibar ulizingatia kifungu na 68,(l)(i) cha katiba ya Chama sio sahihi, jambo ambalo Lwakatare alisema si kweli.

“Majina hayo yaliteliwa kwa kusikiliza majungu, fitina, njama za unafiki, roho mbaya, uchoyo na mtimanyongo wa baadhi ya wanachama na viongozi wa chama hicho,” alisema Lwakatare.

Lwakatare alimtuhumu Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar ambaye pia ni Mkurugenzi wa Chumi na Fedha Juma Duni Haji kuwa anampikia majungu na ndiye aliyesababisha jina lake kuachwa.

Hata hivyo akijibu tuhuma hizo Duni alisema CUF haina kawaida ya kujibizana na viongozi wake walioacha au kuachwa kupitia vyombo vya habari.

“Sisi CUF hatuna kawaida ya kujibizana na viongozi tuliokuwa nao katika chama na baada ya kujitoa au kuachia ngazi nyadhifa zao kupitia vyombo vya habari,” alisema Duni.

Hata hivyo juhudi za kumtafua profesa Lipumba na Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho Ashura Mustafa ambaye alituhumiwa na Lwakatare kwa madai ya kumpakazia kuwa aliangushwa katika unaibu kwa sababu uwezo wake kiutendaji umedidimia (amefulia), hazikufanikiwa.

No comments:

Post a Comment